Ruhazwe JR
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 3,403
- 920
Ndugu zangu wana JamiiForums,
Ninaomba kufahamishwa juu ya kesi za madai kuanzia procedure za kufungua kesi. Ninadaiwa milion 3 ambazo niliazimwa na rafiki yangu wa karibu, wakati tunakopeshana tulienda kuandikiana kwa wakili wa kujitegemea na tulipofka pale wakili alidai hata kama tunapeana kindugu lazima tuweke kiwango cha riba endapo siku itazidi kwa siku ya marejesho.
Baadaye mambo yakaeniendea vibaya ambapo hadi sasa sijaweza kurejesha mkopo na nipo namuuguza mke wangu ambaye ana mtoto wa miezi tisa.
Napigiwa simu na mtu ambaye simjui, anadai yeye ni ndugu wa anayenidai ananitafuta akiwa na RB ya kunikamata.
Naomba kujua haki zangu ni zipi ingawaje nadaiwa katika hili, nielimisheni sina ufahamu wowote juu ya Elimu ya Sheria na nifanye nini maana nipo mbali na natafutwa kwa RB ukizingatia itakua ni mara ya kwanza kwenda Polisi na Mahakamani.
Ninaomba kufahamishwa juu ya kesi za madai kuanzia procedure za kufungua kesi. Ninadaiwa milion 3 ambazo niliazimwa na rafiki yangu wa karibu, wakati tunakopeshana tulienda kuandikiana kwa wakili wa kujitegemea na tulipofka pale wakili alidai hata kama tunapeana kindugu lazima tuweke kiwango cha riba endapo siku itazidi kwa siku ya marejesho.
Baadaye mambo yakaeniendea vibaya ambapo hadi sasa sijaweza kurejesha mkopo na nipo namuuguza mke wangu ambaye ana mtoto wa miezi tisa.
Napigiwa simu na mtu ambaye simjui, anadai yeye ni ndugu wa anayenidai ananitafuta akiwa na RB ya kunikamata.
Naomba kujua haki zangu ni zipi ingawaje nadaiwa katika hili, nielimisheni sina ufahamu wowote juu ya Elimu ya Sheria na nifanye nini maana nipo mbali na natafutwa kwa RB ukizingatia itakua ni mara ya kwanza kwenda Polisi na Mahakamani.