Sheria inasema nini kuhusu hili

Freddy81

Member
Feb 3, 2009
99
3
Habari ya leo ndugu wana jf,
Mimi ndugu zangu napenda kusikia na kusoma maoni yenu kuhusu hili jambo ninalotaka kulizungumzia... Lahusu maeneo yanayopaswa kujengwa mabaa, misikiti na makanisa,
Sheria inasemaje kuhusu hili? mana naona kama hakuna utaratibu mzuri unaosimamia mambo haya, siku hizi makanisa, mabaa na misikiti inajengwa katika makazi ya watu bila hata kujali jamii inayowazunguka.
Kwa mfano hili la mabaa, tena utakuta wanafungua muziki mkuubwa hadi watu wanaona kero,lakini pia sio baa tu.. kwa mfano makanisa pia.. utakuta wamefunga maspika makuuubwa utadhani wanaendesha ibada ya mtaa mzima..hata misikiti pia nayo wameweka maspika yao na kila baada ya muda utasikia wakiswali..tena ile mbaya ni ile ya alfajiri..
Sasa wadau embu niambieni hivi hawa wanaopima na kupanga miji huwa wanafikiria vitu kama hivi? au hawajui ni kero gani zinazotokea?
 
Habari ya leo ndugu wana jf,
Mimi ndugu zangu napenda kusikia na kusoma maoni yenu kuhusu hili jambo ninalotaka kulizungumzia... Lahusu maeneo yanayopaswa kujengwa mabaa, misikiti na makanisa,
Sheria inasemaje kuhusu hili? mana naona kama hakuna utaratibu mzuri unaosimamia mambo haya, siku hizi makanisa, mabaa na misikiti inajengwa katika makazi ya watu bila hata kujali jamii inayowazunguka.
Kwa mfano hili la mabaa, tena utakuta wanafungua muziki mkuubwa hadi watu wanaona kero,lakini pia sio baa tu.. kwa mfano makanisa pia.. utakuta wamefunga maspika makuuubwa utadhani wanaendesha ibada ya mtaa mzima..hata misikiti pia nayo wameweka maspika yao na kila baada ya muda utasikia wakiswali..tena ile mbaya ni ile ya alfajiri..
Sasa wadau embu niambieni hivi hawa wanaopima na kupanga miji huwa wanafikiria vitu kama hivi? au hawajui ni kero gani zinazotokea?


Mkuu ziraili hayuko mbali na wewe. Yaani unagroup pamoja bar na nyumba za ibada? Mbona hujachanganya magereji, filling stations nk? Piga magoti mwombe Mungu radhi. Makanisa na misikiti inatakiwa ijengwe sehemu yoyote ili watu wasicheze mbali na Mwenyezi Mungu.
 
Mkuu ziraili hayuko mbali na wewe. Yaani unagroup pamoja bar na nyumba za ibada? Mbona hujachanganya magereji, filling stations nk? Piga magoti mwombe Mungu radhi. Makanisa na misikiti inatakiwa ijengwe sehemu yoyote ili watu wasicheze mbali na Mwenyezi Mungu.
Kaka hii imani au ndo sheria inavyosema? Bila kua na mtu ka presda Kagame Bongo haiendi? Ki msingi bongo hakuna plani watu wanajifanyia ka watakavyo!!
 
Kaka hii imani au ndo sheria inavyosema? Bila kua na mtu ka presda Kagame Bongo haiendi? Ki msingi bongo hakuna plani watu wanajifanyia ka watakavyo!!

Imani binamu. Kwenye kumcha Bwana hamna kufuata sheria za wajingawajinga binadamu.
 
Mkuu ziraili hayuko mbali na wewe. Yaani unagroup pamoja bar na nyumba za ibada? Mbona hujachanganya magereji, filling stations nk? Piga magoti mwombe Mungu radhi. Makanisa na misikiti inatakiwa ijengwe sehemu yoyote ili watu wasicheze mbali na Mwenyezi Mungu.
Sio kihivyo mjomba,
Sasa kama mi nimelala halafu nikasikia muazana alfajiri na mimi si muisilamu hiyo si kero? au umepumzika ukasikia watu wanaimba kwa sauti sana kanisani na wewe si mkristo na unahitaji utulivu, si kero hiyo? Hiyo ni mifano tu..hayo magereji na filling station zote zinaingia kwenye mada hii... Je sheria inasema nini? achana na suala la imani
 
Misikiti na makanisa ninavyojua mimi inatakiwa ijengwe karibu na makzi ya watu ili watu waweze kuhudhuria kiurahisi. Mfano muislamu wa swala tano atawezaje kwenda umbali mrefu kutoka makazi au kazi yake kwa ajili ya ibada yake kila anapotakiwa kufanya hivyo? Ndiyo maana kila maeneo mapya yanavyogawiwa,huwa kunatengwa sehemu ya misikiti na makanisa.

Ila hii isiwe sababu ya kuleta karaha kwa wakazi wengine. Makanisa yanatakiwa kuweka udhibit wa sauti za vipoza sauti vyao.

Bar zinatakiwa kuwa mbali na makazi ya watu kwani mara nyingi zinafunguliwa usiku watu wakiwa wanapumzika majumbani mwao. Muziki bar tunategemea uwe mkubwa mara nyingi halafu zinachelewa kufungwa.
 
Sasa misikiti na makanisa yakijengwa mbali na makazi ya watu nani atakwenda huko kusali? Nafikiri tatizo si ukaribu wa nyumba za ibada na makazi ya watu bali matumizi ya vipaza sauti. Unakuta vipaza sauti vimefungwa mpaka nje na kuwahubiria hata wasiohusika. Hili ndilo tatizo. Vipaza sauti vilipaswa kufungwa ndani ya kanisa au msikiti ili kurahisha usikivu wa ujumbe kwa waliohudhuria ibada. Na si zaidi ya hapo.

Watu wanapofunga vipaza sauti mpaka nje wanawakosea wale ambao hawahitaji ujumbe huo unaotolewa kanisani au msikitini. Kwani wenye haja na ujumbe huo ni hao waliofika kanisani au msikitini. Hao ndo wanaotakiwa kuhudumiwa na vipaza sauti vyenye kusikika ndani tu.
 
Sheria ziko wazi isipokuwa utekelezaje wake ndugu yangu! Wabunge wetu huwa wanapata shida sana kutunga Sheria ambazo baadaye zinakuja kuwa hazina msimamizi! Sasa kama 75% ya Jiji la Dar es Salaam ina makazi holela (yasiyofuata Sheria za Mipango Miji), sasa jiulize kuna usimamizi wa Sheria hapo? Kuna maeneo yakishika moto au kuvamiwa na majambazi hakuna gari inayoweza kufika kutoa msaada. Hata uzoaji taka wa maeneo hayo ni mgumu mno! Hiyo ndiyo nchi yetu! Mimi simlaumu anayejenga msikiti, baa, gereji, n.k. kwenye makazi ya watu, wapo wa kulaumu!
 
Sio kihivyo mjomba,
Sasa kama mi nimelala halafu nikasikia muazana alfajiri na mimi si muisilamu hiyo si kero? au umepumzika ukasikia watu wanaimba kwa sauti sana kanisani na wewe si mkristo na unahitaji utulivu, si kero hiyo? Hiyo ni mifano tu..hayo magereji na filling station zote zinaingia kwenye mada hii... Je sheria inasema nini? achana na suala la imani

Eee Mungu, msamehe Mtumishi huyu kwakuwa hajui alisemalo. Anataka sheria za binadamu zitumike kuhamisha watumishi tusikuabudu katika maeneo uliyoyaumba wewe mwenyewe kwa uweza wako. Amesahau hata hizo sheria anazosema, zimetungwa na binadamu uliowaumba wewe mwenyewe kwa nkono wako. Halafu kwa kiburi ananiambia eti niachane na imani yangu juu yako ili nifuate sheria aliyotunga binadamu .Msamehe baba, saba mara sabini.

Amina.
 
Back
Top Bottom