Inaonekana Mawazi wengi waliojiuzulu wameonewa na hata watendaji wengine wa Serikali. Rais wetu anafahamu tatizo liko wapi lakini anawakingia kifua wahalifu kwa sababu anazojua mwenyewe lakini sisi wananchi tuliompa dhamana ya kuilinda katiba ya JMT kwa kumwapisha mbele ya Mungu leo tunaambiwa ni upepo utakaopita tu. Nasema hata kama sheria haisemi kitu au wabunge wakaogopa kupiga hizo kura lakini kiapo alichokula kwa kumnyooshea Mwenyezi Mungu Kuruan itamtafuna yeye na familia yake kwani Mungu hadhihakiwi, Rais anakiuka katiba makusudi huku wananchi wanalia na kulalamika maisha magumu kutokana na watawala kukiuka kiapo chao na kujinufaisha wenyewe. Mwenyezi Mungu hatawaacha.