Shelukindo katikisa Taifa kwa dakika 10 tu.

Kwa kifupi, Beatrice Shellukindo kawaambia wabunge wa CCM kuwa wanachofanya wabunge wa upinzani ni sahihi kabisa, wako hapo kukosoa chama tawala na ndivyo wanatakiwa kufanya kama wabunge wa upinzani. Badala ya kukwashambulia wangechukuwa yale mazuri wanayoambiwa na upinzani.

Pia kasema wabunge wa upinzani wanapenda sana chama tawala na wanachofanya ni kukosoa ili chama tawala kijirekebishe na hivyo kuendelea kubaki madarakani.

Kwa maoni yangu Beatrice Shellukindo ameonesha uelewa mzuri sana wa siasa za vyama vingi ndani ya bunge. Ameonesha kuwa na ngozi mungu jambo ambalo ni muhimu kwenye ulingo wa siasa. Wabunge wa CCM wanaoshambulia wapinzani ni kutoelewa nini kazi za ya wapinzani. Kuna utoto wa hali ya juu CCM!

...amesoma alama za nyakati!
 
OKEY! ANGALAU TUNAPATA wanasisim wa tofauti kidogo. ila wanaweza kumuita wamuonye
 
Mama huo ndio ukomavu wa kisiasa na usomi,utapita 2015,maana wabunge hao wanaohangaika kuwajibu wapinzani,kweli hawaelewi maana ya upinzani,maana umeongea dakika kumi tu,na umekuna taifa zima,kwa maneno ya kujenga nchi,we ni mzalendo,endelea hivyo mama achana na hao wanaoshinda kujibu upinzani na kupiga makofi,machozi ya watanzania watayalipa siku moja kwa unafiki na uovu wanaoufanya.

Hebu tupe brief ya alichokisema mkuu maana wengine hatuko kwenye TV kwa muda wa bunge. Asante.
 
kweli kaongea ukweli,maana wengi humo bungeni wenye kijani wanapiga kampeni na kuchambuo bajeti ambayo ni maoni ya kambi ya upinzani.is she among viti maalim??maana viti maalum wengi wameenda kulinda nafasi zao ili wapewe next time,ndiyo maana nikasema wabunge wetu sio watanzania maana hawajui hata maisha halisi ya mtanzania.mh.mkono pia kaomgea na kuhoji vitu vya msingi kabisa.shinda wabunge wa nyinyiem,wanajenga ngome ya wanamipasho.badala ya kujibi hoja zenye manufaa kwa wananchi wanaonge upuuzi.na akiri zao wanaona eti wananchi tunawashangaa wapinzani,kumbe wao ndi wanaotushangaza na kutubore.

Upepo wa changes unavuma kwa kasi kubwa mno .Muulize Masha anajua hili na hata JK he knows .Shelukindo katumia ujinga wa Komba na Chembe ku score points na kwa kweli atakuwa kawamaliza mno wana CCM.Now ataitwa mpinzani kwa akili za CCM .
 
Ndugu yangu Chilipamwao pamoja na kukosea "spelling" ulinielewa? Nimewahi kufanya kazi na wakubwa ambao taarifa ikimfikia mezani badala ya kusahihisha mada iliyomo ndani ya taarifa (facts) yeye muda mwingi ni kusahihisha "The, is, an, a"; ndio mfano wako
Hata mimi huwa nafanya hivyo hivyo, siwezi kusoma taarifa nikafurahia kama matumizi ya "The, is, an a" hayajakaa sawa. Lazima nianzie na hivyo kwanza then tunaenda kwenye facts (technical).
 
Nimesikilza kidogo nilichopata kazungumzia umuhimu wa wapinzani katka mfumo wa vyama vingi na kasema wanaopoteza muda kupambana bungeni na kambi ya upinzani ni wasioelewa maana ya upinzani.Hoja zianzotakiwa kujadiliwa bungeni ni taarifa ya mzee wa gombe, hotuba ya waziri wa fedha na mpango wa maendeleo 5yrs kwisha.Mambo ya kujadili hotuba ya kambi ya upinzani huo ni uzezeta ni nje ya mada.AMEWATAKA WAPINZANI WAONGEZE NGUVU KUIPINGA NA KUIKOSOA SERIKALI YA CCM ILI IENDELEEE KUTAWALA.Mama kapinga mwenendo wa wabunge wa ccm kushambulia upinzani

hapo kwenye red nimepapenda
 
Hata mimi huwa nafanya hivyo hivyo, siwezi kusoma taarifa nikafurahia kama matumizi ya "The, is, an a" hayajakaa sawa. Lazima nianzie na hivyo kwanza then tunaenda kwenye facts (technical).

Ndugu yangu wa WA-UKENYENGE kama unaangalia technical ni sawa mimi bosi wangu alikuwa haangalii technical kabisa zaidi ya kuweka maneno ya Kingereza chake alichojifunza UK akichukua ACCA
 
Last edited by a moderator:
Nice comments in a silly session.

However, the problem with this lady is her unpredictable hypocrisy!! She is indifferent and largely inconsistent.

I used to understand her better when Mzee Shelukindo was by her side there, but now it's a futile execrice.
 
Ndugu yangu Chilipamwao pamoja na kukosea "spelling" ulinielewa? Nimewahi kufanya kazi na wakubwa ambao taarifa ikimfikia mezani badala ya kusahihisha mada iliyomo ndani ya taarifa (facts) yeye muda mwingi ni kusahihisha "The, is, an, a"; ndio mfano wako

Mkuu utanivunja mbavu na hizo the, is, an, a maana umenikumbusha mzee Bushiri naye hiyo ndo ilikuwa kazi yake na kienglish chake cha Oxford!
 
Last edited by a moderator:
hata peter silukamba mbunge wa Kigoma aliongea vizuri sana "...mheshimiwa spika, tunachotakiwa kuchangia katika bajeti ni kutoa maoni yetu, kambi ya upinzani wametoa maoni yao, na wabunge wengine pia wametoa maoni yao, huwezi ukasimama kama mbunge kujadili au kukosoa maoni ya wenzio au kila mmoja aliyetoa huko ni kulipotezea bunge muda wake!...." then alianza kuchangia......
 
Back
Top Bottom