Junius
JF-Expert Member
- Mar 11, 2009
- 3,181
- 139
Mkuu Halisi, KeilNina maswali kidogo kuhusu hiyo quote hapo juu na uchaguzi wa mwaka huu.
Mara ya mwisho kwenye reconciliation walisema kwamba Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), wajumbe wake pia watateuliwa kutoka CUF ili kuhakikisha kwamba haki inatendeka kwenye chaguzi zitakazofuata. Na kumbukumbu yangu inasema kwamba Karume alimteua mjumbe mmoja akidai kwamba ni mwanachama wa CUF, lakini CUF walisema Karume hakutakiwa kuteua yeye moja kwa moja, alitakiwa awaambie CUF ili wampe jina maana wao CUF ndiyo wanawajua wanachama wao vizuri. Sikumbuki sakata hilo liliishia wapi. Maswali:
1. Je, kuna any developments kuhusu kuhakikisha kamba ZEC inajumuisha pia wana CUF ili kuondoa hisia za kuibiwa kura ama udanganyifu wa kura za maruhani?
2. CUF wamefanya maandalizi gani kuhakikisha kwamba mwaka huu wizi hauwezi kufanyika tena?
3. Kuna dalili zote za CCM kuanza njama za kuiba kura?
Najua unaweza usiwe na majibu ya kutosheleza, lakini hata hint tu zinatosha ili kupata feeling what is on the ground na tujue mapema kama mchezo mchafu utaendelea as usual ama mwaka CUF watashangilia badala kulia.
Ni hayo tu Mkuu, usiwe unapotea sana maana msimu wa news muhimu na za uhakika umewadia.
Wapo watu wanaweza kutusaidia kitaalamu zaidi. Ila ninachoweza kudadavua katika maswali hayo ni kama ifuatavyo:
Itakumbukwa katika muafaka wa mwanzo au wapili ilitakiwa pawepo mabadiliko ya tume kwa kuingiza wajumbe kutoka vyama vya siasa na hili lilifanyika kwa CUF kuingiza wajumbe wawili na CCM kadhalika. CUF iliwapeleka ndg. Nassor Khamis Mohammed(mwanasheria) na ndg.Ayoub Bakar na CCM ikawakilishwa na ndg. Khatib Mwinchande na Said Bakari Jecha ambaye amewahi kuwa kitengo cha usalama wa taifa na waziri katika wa SMZ kama sikosei na bado ni mjumbe wa tume.
Cha ajabu licha ya kuwa wajumbe wa CUF wamo humo lakini bado ZEC imekuwa ikiongozwa na makada wa chama cha Mapinduzi na usalama wa taifa. Tokea tume iundwe Wenyeviti wake wote wamekuwa ni makada wa CCM kuanzia jaji Zubeir Juma Mzee, Mzee Masauni (baba yake Masauni aliyefukuzwa ubosi UVCCM)...na huyu wa sasa Khatibu Mwinchande ambaye awali alikuwa mjumbe wa tume hiyo kwa tiketi ya CCM sasa ndo mwenyekiti wake. Uadilifu wa tume bado una mashaka na wajumbe wawili wa CUF humo hawawashi wala hawazimi.
Kuhusu maandalizi ya kuzuia wizi wa kura kwa CUF hali imekuwa ngumu, kwa sababu moja kubwa, CCM wana mbinu nyingi za kuiba kura, hawaibi kwa kuziongeza zao, wanaanza kuzipunguza za CUF...mfano kuwakataa kuandikisha wapiga kura wake ,ukizingatia tume ni yao wao na mchakato wa kupandikiza wapiga kura hewa huwa ni rahisi kwao, bila shaka haya yote tumeyashuhudia katika hatua ya ku up date daftari la wapiga kura.
Ilichofanya CUF,kama kawaida ya Maalim Seif, ambaye ni ukweli usiofichika kuwa hakuna mwanasiasa yeyote anaeziweza siasa za visiwani kama Maalim Seif, amecheza karata yake ambayo mimi naiita "confusion card" nyinyi iiteni "MARIDHIANO BAINA YAKE NA KARUME". Karata hii tayari inafanya kazi yake vizuri sasa hivi, kwakuwa imeshakigawa chama cha mapinduzi vipande vipande. Ni triki ambayo imeshakigawa chama cha mapinduzi Zanzibar na kumchanganya mwenyekiti wake Kikwete.
Hapa binafsi nayakumbuka maneno ya Maalim Seif aliyosema katika mkutano wa hadhara Kibandamaiti,baadha ya kutanganza kumtambua karume,alisema"wanaosema injini ya Maalim Seif imechemsha wanajidanganya....injini ya Maalim haijachemsha bado ipo fit na subirini mtaona..." nakweli sasa tunaona, kirusi cha MARIDHIANO kinaichachafya CCM yote.
Hapa CUF wanafaidika vipi?
Kama DR.Shein atalazimishwa kupita basi hivyo hivyo atalazimishwa kuwa rais Zanzibar na serikali ya mseto itaundwa hata kama kura ya maoni itasema HAPANA. Kwa hiyo maalim kurudi ikulu ni suala la kusubiri tu,ukizingatia CUF inaweza kum KNOCK OUT,Dr.sheni kwa kumuwekea pingamizi kugombea, ambayo ipo wazi kuwa hana sifa yakuwa mgombea baada ya kupoteza ile ya kuwa mwakilishi.
Kama Bilal atapitishwa itachukuwa mda kidogo CCM kupotea kwa kuwa migogoro ya siasa haita kwisha iwapo kura ya maoni italazimishwa kuwa HAPANA, nikimaanisha karata ya CUF itabaki kwa kura ya maoni tu na mkakati mweingine ambao ni siri ya chama.
Nafikiri kwa suala la tatu litakuw limejibika kwa lapili.