Kwa muda mrefu nimekuwa nikitatizwa sana na vyombo vya habari kumwita sheikh Yahaya kuwa mtabiri maarufu wa Afrika Mashariki na kati. Utabiri wake mwingi naona unatokana na hali halisi ya maisha katika dunia yetu hivyo ambayo hata mtu ambaye hajaingia darasa anaweza ku analyse. Nimemsikia juzi akisema tawala nyingi za ki afrika zitapata misukosuko. Ninachojiuliza hapa huo ni utabiri au ni mwenendo mzima wa binadamu kuamua kumaliza utawala wa kimabavu wa serikali zetu? Kuelekea uchaguzi wa Tanzania alisema mmoja wa viongozi wagombe atakufa-kwa kuwa kila binadamu lazima afe sioni kama anatabiri bali naona kama ansema kitu kipo obvious kutokea. Anachokifanya hata profesor Baregu au Lwaitama ukimwuliza anaweza kukupa majibu yanayofanana. Iko haja ya kutofautisha kati ya mchambuzi na mtabiri vinginevyo tutakuwa tunadanganyana-nawakilisha