Sheikh Ponda amezitoa wapi hizi takwimu?

Ukoo Flani

Senior Member
Sep 1, 2011
156
41
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu imepanga kwenda mahakamani kuzuia zoezi la sensa na kupinga kauli iliyotolewa na Sheikh Mkuu wa Baraza la Waislamu (Bakwata), Mufti Issa Shaban Simba, kwamba Waislamu wamekubali kuhesabiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa jumuiya hizo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema kauli ya Mufti Simba, inaashiria kwamba Bakwata limekiuka makubaliano yaliyofikiwa mjini Dodoma na jumuiya zote za waumini wa dini hiyo.

Alisema kauli hiyo haitakuwa na athari kubwa kwa msimamo wa Waislamu wengi ambao hawatashiriki zoezi la sensa.

"Waislamu tumepanga tarehe hiyo ya sensa kufanya maandamano ya amani nchi nzima kwani sensa inayokusudiwa haitakuwa na matokeo sahihi kwakuwa asilimia 80 ya Waislamu ambao ni zaidi ya nusu ya Watanzania hawatahesabiwa," alisema Shekh Ponda.

Hivi karibuni Mufti Simba, alitoa msimamo wa Bakwata, akiwataka Waislamu wote nchini kushiriki Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.

Chanzo: Nipashe

Huyu Sheikh amezipata wapi hizo takwimu kwamba 80% ya Waislamu TZ ni zaidi ya nusu ya Watanzania wote? Halafu baada ya Sensa ya dini ikajulikana waumini wa dini fulani ndio majority italisaidiaje Taifa? Ninaamini kuwa wapo waislamu wengi Tanzania wasioyumbishwa na kauli na misimamo ya viongozi wao, lakini viongozi wa aina hii wana mchango gani kwenye ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla?
 
mi napendekeza waweke huo udini wao, ili tufuatilie nyendo zao. nimechoka na kelele zao. kuna mmoja alitoa ufafanuzi kuwa, eneo la kiseke mwanza, maeneo ya huduma za jamii, wakati wakristo wametengewa zaidi ya hekata 1,000 kufanya shughuli za kijamii kujenga makanisa na mambo memngine yanayowahusu, waislamu wametengewa hekata 100 tu. sina hakika na takwimu hizi, lakini akasisitiza, kilichosababisha utofauti wa ukubwa wa maeneo, ni kwa kuwa serikali ina takwimu za idadi ya watu kwa kuzingatia dini zao kitu ambacho hakijawahi kufanyiwa kazi tanzania.

mimi nilimjibu nikamweleza kuwa, waislamu kuna madhehebu makubwa manne, wakati wakristo utahesabu madhehebu hadi utachoka. kiukweli sijui idadi ya madhehebu kwani yaliyopo si chini ya 50 kwa yale ninayoyafahamu. kwa hiyo iwapo kila dhehebu litaomba kiwanja huko kiseke, hata hizo hekata 1,000/ hazitatosha, lakini waislam kwa idadi ya madhehebu yao, wana uhakika wa kupata kila dhehebu hekta 25, ambalo ni eneo kubwa mno.

sasa kama wanahisi wananyanyaswa katika kugawa rasilimali za taifa, tuhesabiwe kwa dini zetu ili tuone mwishoni itakuwaje
 
80% ya waislamu ni tofauti na kusema 80% ya watanzania ni waislamu. nadhani yeye alimaanisha ile ya kwanza. Ila kasema zaidi ya 50% ya watanzania ndio waislamu ikimaanisha kuwa asilimia ni kati ya 50%-59.5
 
mi napendekeza waweke huo udini wao, ili tufuatilie nyendo zao. nimechoka na kelele zao. kuna mmoja alitoa ufafanuzi kuwa, eneo la kiseke mwanza, maeneo ya huduma za jamii, wakati wakristo wametengewa zaidi ya hekata 1,000 kufanya shughuli za kijamii kujenga makanisa na mambo memngine yanayowahusu, waislamu wametengewa hekata 100 tu. sina hakika na takwimu hizi, lakini akasisitiza, kilichosababisha utofauti wa ukubwa wa maeneo, ni kwa kuwa serikali ina takwimu za idadi ya watu kwa kuzingatia dini zao kitu ambacho hakijawahi kufanyiwa kazi tanzania.

mimi nilimjibu nikamweleza kuwa, waislamu kuna madhehebu makubwa manne, wakati wakristo utahesabu madhehebu hadi utachoka. kiukweli sijui idadi ya madhehebu kwani yaliyopo si chini ya 50 kwa yale ninayoyafahamu. kwa hiyo iwapo kila dhehebu litaomba kiwanja huko kiseke, hata hizo hekata 1,000/ hazitatosha, lakini waislam kwa idadi ya madhehebu yao, wana uhakika wa kupata kila dhehebu hekta 25, ambalo ni eneo kubwa mno.

sasa kama wanahisi wananyanyaswa katika kugawa rasilimali za taifa, tuhesabiwe kwa dini zetu ili tuone mwishoni itakuwaje

Kwani wewe ni dini ipi?
 
Hivi idadi kubwa ya waumini wa dini bila kuwa na uwezo kiakili inasaidia nini katika Dunia hii? Hivi idadi kubwa ya wapalestina imesaidiaje kuwaondoa katika makucha kandamizi na utwala wa waisraeli? Hivi bado hatuwaoni wamasai na wasukuma mtu mmoja avyoswaga kundi la makumi ya ng'ombe?
Ndugu zangu tuache ujinga wakujitambulisha na kutengana kwa kufuata dini za wakandamizaji na wanyanyasaji. Kila siku najiuliza itakuaje babu zetu wale walio hasiwa kwenye bandari za bara Arab wakiamka na kuwakuta wakina sheikh Ponda na misimamo Yao ya KUWATENGA ndugu zao waafrika weusi na kuwakumbatia waarabu na dini yao?
 
Hivi cheo cha usheikh amepewa na nani? Sheikh ponda ameishia darasa la ngapi?

Hivi huyu ni sheikh au muuni?
 
Hii Nchi sasa kila mtu anajisemea la kwake huu uchokozi ipo siku watashindwa kuuvumilia na watatoka kama inavyostahili.
 
Izo Zama za Kutangaza Dini kwa kutumia Energy (nguvu) zishapitwa na wakati..hasitake kuwafanya waislam wote wajinga..Kama kweli Mshika Dini kwa asiendelee Mawaidha yenye kujenga Dini..

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Kwa nini msimpuuze mtu huyu
jumuiya na taasisi za kiislamu imepanga kwenda mahakamani kuzuia zoezi la sensa na kupinga kauli iliyotolewa na sheikh mkuu wa baraza la waislamu (bakwata), mufti issa shaban simba, kwamba waislamu wamekubali kuhesabiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini dar es salaam jana, katibu mkuu wa jumuiya hizo, sheikh ponda issa ponda, alisema kauli ya mufti simba, inaashiria kwamba bakwata limekiuka makubaliano yaliyofikiwa mjini dodoma na jumuiya zote za waumini wa dini hiyo.

Alisema kauli hiyo haitakuwa na athari kubwa kwa msimamo wa waislamu wengi ambao hawatashiriki zoezi la sensa.

"waislamu tumepanga tarehe hiyo ya sensa kufanya maandamano ya amani nchi nzima kwani sensa inayokusudiwa haitakuwa na matokeo sahihi kwakuwa asilimia 80 ya waislamu ambao ni zaidi ya nusu ya watanzania hawatahesabiwa," alisema shekh ponda.

Hivi karibuni mufti simba, alitoa msimamo wa bakwata, akiwataka waislamu wote nchini kushiriki sensa ya watu na makazi itakayofanyika agosti 26, mwaka huu.

Chanzo: Nipashe

huyu sheikh amezipata wapi hizo takwimu kwamba 80% ya waislamu tz ni zaidi ya nusu ya watanzania wote? Halafu baada ya sensa ya dini ikajulikana waumini wa dini fulani ndio majority italisaidiaje taifa? Ninaamini kuwa wapo waislamu wengi tanzania wasioyumbishwa na kauli na misimamo ya viongozi wao, lakini viongozi wa aina hii wana mchango gani kwenye ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla?
 
Nafikir sio jambo baya kujua idadi na sio kujua idadi tu bali ni kuweka takwimu za nchi sawa ,ili kujua majority ya idadi ya wenye dini na hata wale wasio na dini. Tunaelewa kuwa serikali yetu ni ya kipagani lakini utaona imeikataa OIC na kuikubali Vatican ,ni kosa la kikatiba nchi nyingi tu hata kwenye passport zao unaweza kuona sehemu inayokutaka kubainisha dini yako.NA KWA NINI JAMBO HILI LIKATALIWE KUNAOGOPWA NINI ? au ni sawa kama vile CCM wanacyokataa kuweka tume huru ya Uchaguzi inayoshirikisha wadau wote ??
 
Nafikir sio jambo baya kujua idadi na sio kujua idadi tu bali ni kuweka takwimu za nchi sawa ,ili kujua majority ya idadi ya wenye dini na hata wale wasio na dini. Tunaelewa kuwa serikali yetu ni ya kipagani lakini utaona imeikataa OIC na kuikubali Vatican ,ni kosa la kikatiba nchi nyingi tu hata kwenye passport zao unaweza kuona sehemu inayokutaka kubainisha dini yako.NA KWA NINI JAMBO HILI LIKATALIWE KUNAOGOPWA NINI ? au ni sawa kama vile CCM wanacyokataa kuweka tume huru ya Uchaguzi inayoshirikisha wadau wote ??

Vatican ni nchi . Je oic ni nchi?
 
When one wants to deceive people they try and convince them that their opinions are facts.
Kama ameweza kujua kuwa 80% ya Waislamu ambao anadai ni zaidi ya nusu ya Watanzania anashindwaje kujua idadi ya Waislamu Tanzania?
 
Jumuiya na Taasisi za Kiislamu imepanga kwenda mahakamani kuzuia zoezi la sensa na kupinga kauli iliyotolewa na Sheikh Mkuu wa Baraza la Waislamu (Bakwata), Mufti Issa Shaban Simba, kwamba Waislamu wamekubali kuhesabiwa.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa jumuiya hizo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema kauli ya Mufti Simba, inaashiria kwamba Bakwata limekiuka makubaliano yaliyofikiwa mjini Dodoma na jumuiya zote za waumini wa dini hiyo.

Alisema kauli hiyo haitakuwa na athari kubwa kwa msimamo wa Waislamu wengi ambao hawatashiriki zoezi la sensa.

"Waislamu tumepanga tarehe hiyo ya sensa kufanya maandamano ya amani nchi nzima kwani sensa inayokusudiwa haitakuwa na matokeo sahihi kwakuwa asilimia 80 ya Waislamu ambao ni zaidi ya nusu ya Watanzania hawatahesabiwa," alisema Shekh Ponda.

Hivi karibuni Mufti Simba, alitoa msimamo wa Bakwata, akiwataka Waislamu wote nchini kushiriki Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.

Chanzo: Nipashe

Huyu Sheikh amezipata wapi hizo takwimu kwamba 80% ya Waislamu TZ ni zaidi ya nusu ya Watanzania wote? Halafu baada ya Sensa ya dini ikajulikana waumini wa dini fulani ndio majority italisaidiaje Taifa? Ninaamini kuwa wapo waislamu wengi Tanzania wasioyumbishwa na kauli na misimamo ya viongozi wao, lakini viongozi wa aina hii wana mchango gani kwenye ustawi wa jamii na taifa kwa ujumla?

Hivi hawa wanaojiita viongozi wa waislam hawana "seniority" kwenye uongozi wao? Inakuwaje Shehe Mkuu wa Tanzania anatoa tamko halafu Shehe mwingine ambaye siyo mkuu anapingana naye hadharani. Anachosahau huyu Ponda ni kuwa kuna watu wangependa sana sensa ionyeshe makabila ya watu ili tujue kabila gani ni kubwa kuliko jingine na raslimali zigawanywe kwa kuzingatia ukabila.

Kama alifuatilia mjadala wa bunge jana kuna mbunge wa jimbo mojawapo la kanda ya ziwa alikuwa anahoji, pamoja na mambo mengine ya kijimbo, kuwa inakuwaje kanda ya ziwa pamoja na kuwa na raslimali nyingi haina mawaziri wa kutosha kwenye baraza jipya. Ninachosema hapa ni kuwa ukiruhusu sensa kwa misingi ya dini za watu hutakuwa na hoja ya msingi ya kuzuia sensa kwa misingi ya makabila ya watanzania. Kwa waafrika ukabila unawaunganisha watu kuliko udini na ni hatari sana kuchochea hilo kwa nchi yetu. Waafrika tunaamini zaidi katika ukabila kuliko udini na ndio maana siyo ajabu kumkuta mwafrika anaingia kwenye hizo dini za kigeni huku bado akendelea na imani zake za kijadi. Ukabila ni chanzo cha mauaji makubwa kwa majirani zetu - Kenya, Rwanda, Burundi, Conco n.k.
 
Nafikir sio jambo baya kujua idadi na sio kujua idadi tu bali ni kuweka takwimu za nchi sawa ,ili kujua majority ya idadi ya wenye dini na hata wale wasio na dini. Tunaelewa kuwa serikali yetu ni ya kipagani lakini utaona imeikataa OIC na kuikubali Vatican ,ni kosa la kikatiba nchi nyingi tu hata kwenye passport zao unaweza kuona sehemu inayokutaka kubainisha dini yako.NA KWA NINI JAMBO HILI LIKATALIWE KUNAOGOPWA NINI ? au ni sawa kama vile CCM wanacyokataa kuweka tume huru ya Uchaguzi inayoshirikisha wadau wote ??

Akili za madrassa hizo! kulinganisha chungwa na nanasi! Vatican na OIC wapi na wapi? Ungeniambia Vatican na Iran ningekuelewa. Kwa akili hizi hata mkiwa 80% mtaendelea kuburuzwa tu na 20%
 
Nafikir sio jambo baya kujua idadi na sio kujua idadi tu bali ni kuweka takwimu za nchi sawa ,ili kujua majority ya idadi ya wenye dini na hata wale wasio na dini. Tunaelewa kuwa serikali yetu ni ya kipagani lakini utaona imeikataa OIC na kuikubali Vatican ,ni kosa la kikatiba nchi nyingi tu hata kwenye passport zao unaweza kuona sehemu inayokutaka kubainisha dini yako.NA KWA NINI JAMBO HILI LIKATALIWE KUNAOGOPWA NINI ? au ni sawa kama vile CCM wanacyokataa kuweka tume huru ya Uchaguzi inayoshirikisha wadau wote ??

Sio kila kinachofanywa na nchi nyingine ni sahihi kufanyika na hapa kwetu. Huo ni ukasuku wa kuiga mambo bila kujua msingi wake na faida zake kwa nchi yetu. Hakuna mtu anayeogopa kuhesabu watu kwa misingi ya dini, kabila, rangi, asili ya mtu, "sexual preferences" - kama ni shoga au wa kawaida na kadhalika. Haya ni mambo binafsi ya wananchi ambayo taifa halina haja ya kujua. Maswali ya msingi ya kujibu, ambayo kwa bahati mbaya hayajapata majibu ya maana, ni kwa nini tunataka kuhesabu watu kwa misingi hiyo? Je ni kwa maslahi ya nani? Je taifa litafaidika nini kwa kuhesabu watu kwa misingi hiyo? Je misingi ya taifa letu kama inavyoelekezwa kwenye katiba yetu inasemaje kuhusu suala la kuhesabu watu kwa misingi mingine yeyote zaidi ya utaifa wao?
 
Bora waende tu mahakamani ila kwa taarifa yao kwa sasa madodoso yapo tayari kwa hiyo hakuna mtu atakubali kuingia gharama kubwa ya kuaandaa upya kwani kuongeza swali moja tu kuna cost implication ya mamilioni ya shilingi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom