Ukweli utabaki kuwa ukweli hata kama mamia ya watu wataupinga au hakuna yeyote ataeukiri hadharani kuwa ni ukweli. Wakati wanaharakati wengine wakiitwa kuwa wanaharakati kutokana na majina ya taasisi wanazozitumikia kuwa za kiharakati, SHEIKH ISSAH PONDA ni mwanaharakati kutokana na matokeo chanya ya vitendo vyake.
Ni juzi tu ametoka kudhihilisha hili tena kwa kuwezesha jamii kubwa ya waislam kuridhia kuwa sensa lazima iweke kipengele cha dini kwani itasaidia sana kujua idadi za watu kulingana na makundi yao (umri, jinsia, dini n.k)
Kama hiyo haitoshi amekuwa shupavu kupambana na tamaduni za magharibi zinazokinzana na matendo safi mbele za Mungu na Binadamu, mfano mzuri ni pale alipotetea kwa ujasiri kitendo cha Rais Mstaafu Alhaji Ally Hasan Mwinyi kupigwa kofi kwa kosa la kutangaza kwenye maulid kuwa Kondom ni njia sahihi ya kupambana na maambukizi ya ukimwi.
Kwa hayo machache pamoja na mengine mengi Sheikh Issah Ponda amejipambanua kuwa mwanaharakati halisi asiye na hata chembe ya woga katika kutetea kile anachokiamini.
Ni juzi tu ametoka kudhihilisha hili tena kwa kuwezesha jamii kubwa ya waislam kuridhia kuwa sensa lazima iweke kipengele cha dini kwani itasaidia sana kujua idadi za watu kulingana na makundi yao (umri, jinsia, dini n.k)
Kama hiyo haitoshi amekuwa shupavu kupambana na tamaduni za magharibi zinazokinzana na matendo safi mbele za Mungu na Binadamu, mfano mzuri ni pale alipotetea kwa ujasiri kitendo cha Rais Mstaafu Alhaji Ally Hasan Mwinyi kupigwa kofi kwa kosa la kutangaza kwenye maulid kuwa Kondom ni njia sahihi ya kupambana na maambukizi ya ukimwi.
Kwa hayo machache pamoja na mengine mengi Sheikh Issah Ponda amejipambanua kuwa mwanaharakati halisi asiye na hata chembe ya woga katika kutetea kile anachokiamini.