She is attracted to a co-worker.. mgogoro na jamaa

mwanamke huwezi kumwambia mume wako hivyo not that easy otherwise you dont need him any more and dont know where she got that carage of telling his husband those painfully words .but loving somebody is cryz thing mapenzi nahisi yanaushetani hayahekeweki hata kidogo mtu anaweza akakufanyia tukio ukaona uko ndotoni .my advice jipende mwenyewe kwanza kabla ya kupenda coz utajua value ya thamani yako coz mapenzi kigeugeu
 
Ndo dunia ilivyo, unaye mpenda hakupendi anampenda mwingine ambaye hana mda nae, ama hayuko kivile kwake.
 
Ni kisa cha weekend kwa kweli; jamaa yangu mmoja kaja juu dhidi ya mke wake kwa sababu mkewe ka-admit kwake kuwa ni kweli yuko attracted to a co-worker japo huyo co-coworker hajajua kabisa kinachoendelea. Mke kaadmit akiaini kuwa ni bora kusema mapema kabla mambo hayajaenda pabaya. Sasa kumwambia jamaa jamaa kaja juu na maswali lukuki akijihoji kuwa labda yeye ndiye sababu au kuna vitu hafanyi japo mwanamke anasema kabisa wala haihusiani na yeye (mume) ni kitu ambacho hata mwanamke hakielewi kwanini yuko attracted na huyo mtu mwingine - tumuite John.

Sasa, shemeji yetu hamwelezi mshikaji kwa sababu anasema kama angekuwa na nia mbaya asingemwambia (jamaa anasema labda amesema ili kuhalalisha). Lakini she swears hajafanya lolote lakini alikuwa anajihisi kama amecheat maana yuko comfortable sana na huyo John na ana enjoy sana company yake. Hajui kama anampenda au anamtamani

Mshikaji anaamini yuko sahihi kukasirika na sasa hivi amekuwa more than insecure kwani shemeji yetu kwa kweli wamo. Imeanza kuleta mgogoro usio wa lazima...

Kweli kuwa attracted bila kufanyia kazi ni kucheat na je kuna hekima kumwambia mwenzio majaribu unayoyapata huko kazini na usipomwambia yakafikia pabaya nani wa kulaumiwa?

Mzee Mwanakijiji. Shukran kwa kutuletea kisa hiki.
Nina imani kabisa hiki kisa kimetokea US na huyo mwanamke atakuwa ni mmarekani manake wanawake hawa ndo wenye kuwa open hata kama huo uwazi wenyewe unamuumiza mwenzake. Wanawake wetu wa kiafrika huwa wanakuwa na busara ya kutambua kuwa akiweka wazi habari kama hii itamuumiza mwenza wake.
Jamaa anayo kila haki ya kuumia rohoni na hapana shaka ataji-feel insecured. Nadhani huyu dada alitakiwa afe kizungu na siri yake hiyo akae nayo rohoni. Cha msingi kama kweli anampenda jamaa yake, alitakiwa amkalie mbali huyo jamaa wa kule kazini.
Emotional connection with another person other than your partner is nothing more than just cheating on your partner. Period! Hapo nahisi kama wasipokuwa makini kitakachoendelea hapo ni emotional disconnection kati ya huyo mdada na kaka yetu na eventually wataachana.
Ama kweli mapenzi ni kizungumkuti na ukiyaendekeza yatakutia uchizi
 
mwanamke ndio ni Mmarekani lakini mwanamme ni Mbongo... i don't know if that matters. Mwenyewe amehalalisha ati kuwa kuwa attracted na mtu mwingine na hata kujikuta una enjoy hivyo ni 'emotional cheating' tena mwenyewe kadai ni ya 'hatari zaidi'...
 
Hii imekaa vibaya. Huyo jamaa atakuwa very insecure, atamchukia huyo mwenzi wake pamoja na huyo co-worker wake! Ni vizuri watu tukajifunza kuheshimu hisia za wenzetu. Huyo dada tayari amemuumiza mumewe kihisia. Hakuwa na sababu ya kumwambia. By the way, usikute hata huyo co-worker mwenyewe mumewe wala hamfahamu..
 
mwanamke ndio ni Mmarekani lakini mwanamme ni Mbongo... i don't know if that matters. Mwenyewe amehalalisha ati kuwa kuwa attracted na mtu mwingine na hata kujikuta una enjoy hivyo ni 'emotional cheating' tena mwenyewe kadai ni ya 'hatari zaidi'...



That explains it.... whole lot of different culture....
 
huyo "John" sio kama hajui, anamlia timing, kuchinja kobe lazima unajua mahesabu!, dada kiukweli kateleza kumuambia mpenzi wake, though somehow pia katengeneza mazingira ya jamaa ku-upgrade OS yake...ajue ana competitor mwenye 'absolute advantage'
 
jamani,huo uzungu wa ku admit hivyome naona haufai!ataua mwenzie huyo
 
Sasa kama huyo dada asingesema kitu halafu popole hizo hisia zingeanza kukua na kukomaaa ingekuwaje? Mmewahi kuona filamu ya "Last Night"?
 
mwanamke ndio ni Mmarekani lakini mwanamme ni Mbongo... i don't know if that matters. Mwenyewe amehalalisha ati kuwa kuwa attracted na mtu mwingine na hata kujikuta una enjoy hivyo ni 'emotional cheating' tena mwenyewe kadai ni ya 'hatari zaidi'...
Nilijua tu!.......Tena huyo mdada atakuwa mnugu huyoooo. Hovyo kabisa hawa wanugu, yaani hawana hata utu wala huruma ama imani. They are soooooo selfish, na wanachojali ni wao na nafsi zao, ili mradi yeye yuko poa, mengineyo they don't care.
Mungu amsaidie kaka yetu ktk kipindi hiki kigumu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom