Shangingi La Serikali "Overtime"

M

MegaPyne

Guest
i466_UJAMBAZI2.JPG


Yaelekea ni katika ile mbuzi ula kwa urefu wa kamba yake au pengine ni katika kujiongezea kipato cha ziada pale dereva wa Shangingi hili mali ya serikali chini ya Wizara ya Viwanda na Biashara kule EPZA Bw Geofrey Ernest Barweta alipoamua kupiga ka-overtime kidogo kwa kutumia mshangingi huo pamoja na wenzie watatu kwenda kupora fweza katika kituo kimoja cha mafuta na kwa bahati mbaya kwao siku hiyo (sidhani kama hii ni mara ya kwanza) gemu likabumbuluka na kutiwa mbaloni (From Bongo Pix)

The Picture says it all.
 
Hii ni jokes au kweli?

Huenda ni kweli, lakini pia tujiulize hali halisi, dereva analipwa mshahara 100,000 kwa mwezi, na kakabidhiwa gari la milioni 200.

Niliwahi shuhudia mwingine akipiga debe 'live', magome 100, mwenge 200, akasanya abiria wake ambapo nami nilikuwa mmojawapo wa abiria. Mle ndani akawa sincere kabisa kwamba jamani sasa mi nifanyeje, gari kuuubwa, lakini hata 100 mfukoni sina.

Well, sishabikii kwamba wafanye uharifu, lakini malipo ya watu kama hawa wanaopewa dhamana ya vitu vya mamilioni inabdi yasiwe ya kusuasua namna hii ili pia kusaidia kuwaepusha na vishawishi kama hivi.
 
Huenda ni kweli, lakini pia tujiulize hali halisi, dereva analipwa mshahara 100,000 kwa mwezi, na kakabidhiwa gari la milioni 200.

Niliwahi shuhudia mwingine akipiga debe 'live', magome 100, mwenge 200, akasanya abiria wake ambapo nami nilikuwa mmojawapo wa abiria. Mle ndani akawa sincere kabisa kwamba jamani sasa mi nifanyeje, gari kuuubwa, lakini hata 100 mfukoni sina.

Well, sishabikii kwamba wafanye uharifu, lakini malipo ya watu kama hawa wanaopewa dhamana ya vitu vya mamilioni inabdi yasiwe ya kusuasua namna hii ili pia kusaidia kuwaepusha na vishawishi kama hivi.

Tatizo utamlipa kiasi gani asiwe na tamaa? hahaha. Maana gari ndiyo hivyo la bei ghali na hata umlipe vipi bado kiwango cha mshahara hakiwezi kuwiana na gari lenyewe. Kama wabunge wenyewe hulipwa milioni 12 kwa mwezi na bado wanataka kuongezewa unategemea kuna anaye ridhika mkuu?
 
Tatizo utamlipa kiasi gani asiwe na tamaa? hahaha. Maana gari ndiyo hivyo la bei ghali na hata umlipe vipi bado kiwango cha mshahara hakiwezi kuwiana na gari lenyewe. Kama wabunge wenyewe hulipwa milioni 12 kwa mwezi na bado wanataka kuongezewa unategemea kuna anaye ridhika mkuu?

Nijuavyo mimi wabunge bwanalipwa karibu million 7 na kwa sasa mipango ipo ya kudai walipe 12! Chakushangaza 150,000/= inakatwa kodi lakini million 7 hazikatwi koko huu ni ukora mkubwa.
Viongozi wangekuwa mfano wa kulipa kodi hata walalahoi wasingelalamika sana!
 
Kuna dereva mmoja wa iliyokuwa RTD,alikuwa ktk kipindi cha twende na wakati yeye aliuza gari la RTD akiwa amelipaki pale CCM TANDALE na kusingizia limeibiwa.Walinzi wa CCM wako jela hadi leo wakati yule dereva amestaafishwa na kulipwa marupurupu yake na sasa anaishi maisha yanayomfaa Mbagala.Jamani hawa madereva wakuwaangalia sana wanaweza kukuuza hata wewe mwajiri.
 
Gazeti: Uhuru


Magari ya serikali yapigwa marufuku kulazwa mitaani


* Ni baada ya moja kutumika katika ujambazi

NJUMAI NGOTA NA TUMAINI KAWOGO, RCT

JESHI la Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limepiga marufuku magari ya wizara na taasisi za serikali kuegeshwa na kulazwa mitaani, badala yake kutafuta maeneo rasmi ya kuyaegesha.

Hatua hiyo inatokana na kukamatwa kwa gari la serikali linalomilikiwa na Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, likishiriki kwenye tukio la ujambazi lililotokea juzi katika kituo cha mafuta cha GAPCO mjini Dar es Salaam.

Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam Suleiman Kova, ametoa wiki mbili kwa wizara na taasisi za serikali kutafuta maeneo rasmi ya kuegesha magari hayo na kuwa baada ya muda huo, magari yatakayokiuka amri hiyo yatakamatwa na madereva wake kuchukuliwa hatua.

Alitaja gari lililokamatwa katika tukio hilo kuwa ni lenye namba za usajili STK 4431 aina ya Toyota Land Cruiser GX mali ya wizara hiyo, chini ya kitengo cha maeneo ya uzalishaji kwa ajili ya uuza nje (EPZ). Hata hivyo, taarifa za awali za polisi zilisema gari hilo ni la Tume ya Mipango.

Kova alisema hadi Julai 10, mwaka huu, gari litakalokutwa limeegeshwa au kulazwa holela, dereva wake atachukuliwa hatua na kulikamata.

"Tukikuta magari ya serikali yameegeshwa ovyo au sehemu zisizo rasmi tutayashika, ikiwemo kumkamata dereva wake na kumchukulia hatua," alisema Kova.

Alisema magari mengi yamekuwa hayafuati utaratibu wa uegeshaji, hivyo kuchochea madereva kufanya uhalifu au kuibwa.

Kova aliwataka watafute sehemu ya kuegesha magari yao na kuweka ulinzi wa kutosha, kwani yamekuwa yakiibwa sana. Alitoa mfano hivi karibuni kuwa, gari la serikali liliibwa likiwa na kompyuta.

Alisema baada ya wiki mbili, wataanza kuyakamata magari hayo kwani kazi yao ni kulinda usalama wa raia na mali zao.

Kuhusu sakata la wizi katika kituo cha mafuta, aliwataja watuhumiwa waliokamatwa saa 6.15 usiku wakiwa na gari hilo wakifanya uhalifu katika kituo kilichopo mtaa wa India, mali ya Ghulam Chakaar (55).

Kova alisema watuhumiwa hao walivunja kasiki kwa kutumia mitungi miwili ya gesi na vifaa vingine, vikiwemo bisibisi, koleo na panga.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa dereva wa gari hilo ambaye awali alikuwa askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) namba MT. 68050 wa 701 KJ-Kigamboni aliyeacha kazi mwaka 1998, Geoffrey Barweta (38), mfanyabiashara wa vyuma chakavu Edwin Bitesigilwe (21) na fundi wa kuchomea vyuma Mbwana Shemumea (22).

Kova alisema watuhumiwa walikula njama na watuhimiwa wengine ambao wanaendelea kutafutwa na kwamba upelelezi wa tukio hilo unaendelea na wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika



Magari ya serikali ndiyo mzigo mkubwa kwa uchumi wa nchi yetu. Napenda kuishauri serikali ifanye mambo yafuatayo katika kudhibiti matumizi ya hovyo hovyo ya mali za Watanzania:-
  • Magari ya Serikali yatumike kwa kazi za kiserikali peke yake.
  • Magari ya Serikali yaegeshwe kwenye maegesho ya ofisi za serikali muda wa kazi unapofika isipokuwa kama kuna sababu maalum .
  • Watumishi wote wa wizara, mashirika na taasisi za serikali watumie magari yao binafsi wanapoenda kazini na kurudi nyumbani.Watumishi hawa hawalipi kodi wanapoingiza magari yao binafsi, pia mabenki yote yanatoa mikopo ya muda mrefu kwa watumishi hawa kwa dhamana ya ajira yao kama watumishi wa umma.
  • Viongozi wanaoweza kurudishwa nyumbani na kuchukuliwa asubuhi iwe ni kwa mawaziri, waziri mkuu, makamu wa raisi na rais peke yao. Wengine watumie usafiri wa umma au magari yao.
 
Hii ni big challenge kwa MAMA HAWA GHASIA, Waziri mwenye dhaman ya mishahara kwa Madereva na wafanyakazi wote wa sector ya umma.

JE, MISHAHARA INATOSHA KWA WAFANYAKAZI?????????????????
 
Magari ya serikali ndiyo mzigo mkubwa kwa uchumi wa nchi yetu. Napenda kuishauri serikali ifanye mambo yafuatayo katika kudhibiti matumizi ya hovyo hovyo ya mali za Watanzania:-
  • Magari ya Serikali yatumike kwa kazi za kiserikali peke yake.
  • Magari ya Serikali yaegeshwe kwenye maegesho ya ofisi za serikali muda wa kazi unapofika isipokuwa kama kuna sababu maalum .
  • Watumishi wote wa wizara, mashirika na taasisi za serikali watumie magari yao binafsi wanapoenda kazini na kurudi nyumbani.Watumishi hawa hawalipi kodi wanapoingiza magari yao binafsi, pia mabenki yote yanatoa mikopo ya muda mrefu kwa watumishi hawa kwa dhamana ya ajira yao kama watumishi wa umma.
  • Viongozi wanaoweza kurudishwa nyumbani na kuchukuliwa asubuhi iwe ni kwa mawaziri, waziri mkuu, makamu wa raisi na rais peke yao. Wengine watumie usafiri wa umma au magari yao.

Mkuu MajiM..., hapo umegonga pale panapo penye kabisaaaa..... Unajua hapa nyumbani wafanyakazi wa Serikali hawalipi Kodi waingizapo magari lakini still tunawapa tena gari ya ofisi...... sasa ule msamaha wa kodi ni kwa manufaa gani??

Mimi nadhani inabidi tuangalie hizo pointi zako mbili muhimu hapo juu na kujaribu kujipanga kuelekea kwenye ufanisi.....
 
Ndugu wa Jamii forum, nimeshidwa kuleta nyeti zozote kwa mda mrefu kutokana na mambo mawili; kwanza sijaona jina lolote jenuine kwanye list ya members. Sijajua nini maana yake, na kwasababu mimi nilijiandikisha nikiwa nje ya nchi kuna vitu nilikuwa sivielewi saaana. Jambo la pili ni jinsi maada zilivyokuwa zikienda, kwangu niliona kama kuna-kucheza na hatari hasa kwa wakati huu ambapo vigogo wetu hawapendi kukosolewa. Mambo niliyotaka kufanya ni either kuondoa identity yangu halisi na kuwa kama 1. Invisible, 2. kikongwa, 3. Mzee wa kijijini etc.

That said, I would like you to provide some directives on how to edit some personal particulars in Jamii Forum. I hope there are many people who would like to contribute, especially those in the diaspora, but its a bit scary seeing that all members have nicknames.

Nataraji kupata maelekezo yenu
 
Magari ya serikali ndiyo mzigo mkubwa kwa uchumi wa nchi yetu. Napenda kuishauri serikali ifanye mambo yafuatayo katika kudhibiti matumizi ya hovyo hovyo ya mali za Watanzania:-
  • Magari ya Serikali yatumike kwa kazi za kiserikali peke yake.
  • Magari ya Serikali yaegeshwe kwenye maegesho ya ofisi za serikali muda wa kazi unapofika isipokuwa kama kuna sababu maalum .
  • Watumishi wote wa wizara, mashirika na taasisi za serikali watumie magari yao binafsi wanapoenda kazini na kurudi nyumbani.Watumishi hawa hawalipi kodi wanapoingiza magari yao binafsi, pia mabenki yote yanatoa mikopo ya muda mrefu kwa watumishi hawa kwa dhamana ya ajira yao kama watumishi wa umma.
  • Viongozi wanaoweza kurudishwa nyumbani na kuchukuliwa asubuhi iwe ni kwa mawaziri, waziri mkuu, makamu wa raisi na rais peke yao. Wengine watumie usafiri wa umma au magari yao.
Geoffrey Barweta dereva anayemwendesha Mkurugenzi Mkuu wa EPZ kwa wanaomjua humuita "Kagame" inasemekana hata mazingira yake ya kuacha kazi jeshini ya utata na pia anahisiwa kuwa ni raia wa Rwanda (uraia wake una mashaka).

Pamoja na yote hayo magari ya serikali sasa yapewe amri ya kutekeleza agizo la kuyaandika Majina ya idara/wizara/taasisi ubavuni.

Hili litasaidia sana, vile vile utumiaji wa magari haya kwa shughuli binafsi umekithiri siku za kawaida hata weekend. Unaweza kukutana na gari la serikali asubuhi limebeba watoto wa bosi likiwapeleka shule wakiwa wao na dereva tu. Mamalaka sijui hazioni uozo huu? Hayo nayo ni matumizi ya ovyo sawa na kwenda kuibia gari la serikali.

 
Hii thread mbona ni ya miaka mingi sana?????? Kweli watu waishiwa idea
 
Back
Top Bottom