Shangazi kaja na mchumba kutoka kijijini...Mwenzenu nipo dillema!

Yaani huyu ni Afisa Utumushi wa wapi anashindwa kuamua jambo kama hilo ambalo maamuzi yake yako wazi?mfano akiletewa kesi kuna mfanyakazi hapo ofisini kwake anatembea na mke wa mfanyakazi mwenzake ataenda kumuuliza nani? Ina maana hajui moyo wake unachokipenda? Huyo uamuzi anao mwenyewe na sio wewe umshauri aoe yupi katika hao wawili
Ananiamin ktk ushauri, nadhan anamaamuzi yake bt anatemea ushauri kujustify maamuz yake!
 
Hivi ni kwa nini ndugu hupenda kuingilia mahusiano ya wenzao? kuna faida gani ya kuoa/kuolewa kwa mtu wa kabila lako/kabila moja?
 
Hivi ni kwa nini ndugu hupenda
kuingilia mahusiano ya wenzao? kuna
faida gani ya kuoa/kuolewa kwa mtu
wa kabila lako/kabila moja? Kuna mambo yanachanganya sana hapa!
 
Ni mwaka mmoja sasa umepita toka rafiki yangu kipenzi wa tokea primaly, sekondary mpaka chuo alipopata ajira ktk halmashauri fulani (sitaitaja jina) kama Afisa Utumishi. Takribani mwezi wa 6 sasa tangu rafiki yangu huyu anitake ushauri kwani amekua akisisitiziwa na ndugu zake wa pande zote wa upande wa baba na mama yake juu ya kuoa. Anamchumba wa kichaga aliyepo masomoni chuoni dsm mwaka wa 2 sasa akisomea mambo ya habari pale SJMC, Kifupi wanapendana na mimi pia nampenda shemeji yangu huyu kwa mapenzi ya dhati aliyonayo kwa rafiki yangu, siku zote nimekuwa nikiwatakia mema afikie lengo lao la kuishi pamoja(ndoa), majuzi kanipigia simu, kanipa taarifa kua shangazi yake mkubwa amekuja kutoka kijijini na binti ambaye amechaguliwa na ukoo kama mchumba/mke wake, shangazi yake amedai ujio wake ni kutimiza wajibu kama alivyoamuliwa na kikao cha ukoo pia akasema huko kijijini taratibu nyingine za ndoa zinaendelea. Jamaa kachanganyikiwa, ananiomba ushauri juu ya hili jambo, mimi nimeshindwa kumpa jibu coz sijui niegemee upande gani, shemeji yangu wa chuo namkubali, jamaa yangu sipendi agombane na ndugu zake pia.. Nimemwambia anipe muda then nitamjuza nin chakufanya.. Hapa alipo anasubiri ushauri wangu kwani tunaaminiana, tumeshirikiana, kusaidiana na kushauriana ktk mengi. Hapa nilipo nipo dillema ktk kutoa huo ushauri, jamani tusaidiane ktk hili, nini kifanyike hapo? Nimshaurije? Nawategemea sana ktk hili. Asanteni...
Kuna mambo mawilli ambayo naona nyote ninyi ukiwemo wewe hamyajui na sio kosa lako. Hata mimi nilikuwa kama ninyi. Kwanza yaonesha kuwa hao sio wachumba ni marafiki wa siku nyingi sema kwamba sasa wanapanga kuwa wachumba kisha wafunge ndoa! wewe na hao tafuteni vitabu vinavyoweza kuwasaidia kujua nini maana ya ndoa na je, wafanyeje kujua kuwa mpongo wa Mungu katika kufunga kwao ndoa ni upi? kitabu kama UCHUMBA NA NDOA, kilichoandikwa na Padri dk Mbiku wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na pia NDOA YANGU, NINGEJUA kilichpoandikwa na mwandishi Charles Misango, kitawasaidia kufikia maamuzi mema. Pili, sheria nya nchi ya ndoa, ya mwaka 1971 inatoa ruhusa kwa kijana wa kiume ama wa kike kuoa yule anayemtaka. Ni makosa makubwa na mzazi anaweza kushitakiwa na akaadhibiwa ikiwa atamlazimisha kijana wake wa kike ama kiume kutooana na yule aliyefikia naye maamuzi wa kuishi kama mke na mume
 
Kuna mambo mawilli ambayo naona nyote ninyi ukiwemo wewe hamyajui na sio kosa lako. Hata mimi nilikuwa kama ninyi. Kwanza yaonesha kuwa hao sio wachumba ni marafiki wa siku nyingi sema kwamba sasa wanapanga kuwa wachumba kisha wafunge ndoa! wewe na hao tafuteni vitabu vinavyoweza kuwasaidia kujua nini maana ya ndoa na je, wafanyeje kujua kuwa mpongo wa Mungu katika kufunga kwao ndoa ni upi? kitabu kama UCHUMBA NA NDOA, kilichoandikwa na Padri dk Mbiku wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na pia NDOA YANGU, NINGEJUA kilichpoandikwa na mwandishi Charles Misango, kitawasaidia kufikia maamuzi mema. Pili, sheria nya nchi ya ndoa, ya mwaka 1971 inatoa ruhusa kwa kijana wa kiume ama wa kike kuoa yule anayemtaka. Ni makosa makubwa na mzazi anaweza kushitakiwa na akaadhibiwa ikiwa atamlazimisha kijana wake wa kike ama kiume kutooana na yule aliyefikia naye maamuzi wa kuishi kama mke na mume
 
Jamaa ni msukuma kutokea huko shinyanga, kwao ni ngokolo shy-town!

Hahahaaa, najua hapo kwa mchaga msukuma kakolea na rangi ya ngozi tu. By the way, wasukuma sio wabishi kwa wazazi. Akae na huyo aliyeletwa na shangazi, amwambie kuwa bana we umeletwa kwangu na ndugu ila mi nina niliyekwishakutana naye, na tunapendana, so nisadie ili nisikwaruzane na ndgu zangu. So amwambie huyu mgole amkatae kwa nguvu zake zote na kama hataki, amwambie kuwa, ok nitakuchukua lakini utakuwa tu ndani ila mimi nitakuwa na huyo nimpendaye.

Game will be over...
 
Hahahaaa, najua hapo kwa mchaga msukuma kakolea na rangi ya ngozi tu. By the way, wasukuma sio wabishi kwa wazazi. Akae na huyo aliyeletwa na shangazi, amwambie kuwa bana we umeletwa kwangu na ndugu ila mi nina niliyekwishakutana naye, na tunapendana, so nisadie ili nisikwaruzane na ndgu zangu. So amwambie huyu mgole amkatae kwa nguvu zake zote na kama hataki, amwambie kuwa, ok nitakuchukua lakini utakuwa tu ndani ila mimi nitakuwa na huyo nimpendaye.Game will be over...
Wasukuma wanapenda sana wanawake weupe sana! Km ujuavyo, mila ya kisukuma humfanya mtu subjective kwa wakubwa wake hapa ndipo utata ujapo!
 
Hahahaaa, najua hapo kwa mchaga msukuma kakolea na rangi ya ngozi tu. By the way, wasukuma sio wabishi kwa wazazi. Akae na huyo aliyeletwa na shangazi, amwambie kuwa bana we umeletwa kwangu na ndugu ila mi nina niliyekwishakutana naye, na tunapendana, so nisadie ili nisikwaruzane na ndgu zangu. So amwambie huyu mgole amkatae kwa nguvu zake zote na kama hataki, amwambie kuwa, ok nitakuchukua lakini utakuwa tu ndani ila mimi nitakuwa na huyo nimpendaye.Game will be over...
Nikweli kabisa kuna mambo mengi sana nisiyoyajua juu ya uchumba na ndoa, upeo wangu ktk masuala haya ni mdogo thats why nashindwa kutoa ushauri ktk haya. Mwl. wangu wa tuition enzi hizo za advanced level alishawah kunishauri tukiwa ktk mazungumzo ya kirafiki, alisema "Gagurito ktk maisha kuna mambo ya kufanya maamuzi ya haraka na kuna mambo yanayoitaji muda wa ziada yaweze tolewa maamuzi", akaendelea kwa kusema "ogopa kutoa maamuzi ya haraka ktk mapenzi au kumshauri na kumsisitiza mtu kufanya uamuzi" hz kauli zimekua km mwongozo wangu ktk utoaji wa ushauri hususani unaohusu mapenzi. Nahisi kuna haja ya mimi kuvitafuta hivyo vitabu mzee!
 
Ni dini gani?manake dini zingine zinaruhusu wake zaidi ya mmoja kwa hiyo kama dini yake inaruhusu achukue wote ili apate kurizisha roho yake na ukoo,halafu kwa nini ukoo wamchagulie huyo inabidi afanye uchunguzi manake unaweza kukuta wameshamchakachua sasa wanatafuta mahali pakumdump.
 
Ni dini gani?manake dini zingine zinaruhusu wake zaidi ya mmoja kwa hiyo kama dini yake inaruhusu achukue wote ili apate kurizisha roho yake na ukoo,halafu kwa nini ukoo wamchagulie huyo inabidi afanye uchunguzi manake unaweza kukuta wameshamchakachua sasa wanatafuta mahali pakumdump.
Hivi ni kwa nini ndugu hupendakuingilia mahusiano ya wenzao? kunafaida gani ya kuoa/kuolewa kwa mtuwa kabila lako/kabila moja?Jamaa yangu ni mkatoliki wkt mchumba wake wa dar ni mluthelani, wakijijini nadhan ni mpagani!
 
argggggghhhh.bwana mambo ya kutafutiwa mke yalipitiwa na wakati ....afanye moyo wake unalotaka....siku maji yakishinda unga huko mbeleni hao ndugu zake watamsaidia????????
 
Nikweli kabisa kuna mambo mengi sana nisiyoyajua juu ya uchumba na ndoa, upeo wangu ktk masuala haya ni mdogo thats why nashindwa kutoa ushauri ktk haya. Mwl. wangu wa tuition enzi hizo za advanced level alishawah kunishauri tukiwa ktk mazungumzo ya kirafiki, alisema "Gagurito ktk maisha kuna mambo ya kufanya maamuzi ya haraka na kuna mambo yanayoitaji muda wa ziada yaweze tolewa maamuzi", akaendelea kwa kusema "ogopa kutoa maamuzi ya haraka ktk mapenzi au kumshauri na kumsisitiza mtu kufanya uamuzi" hz kauli zimekua km mwongozo wangu ktk utoaji wa ushauri hususani unaohusu mapenzi. Nahisi kuna haja ya mimi kuvitafuta hivyo vitabu mzee!
.nampa.pongezi.sana.huyo.mzee.na.wewe.kwa.nasaha.hizo .unajua.suala.la.ndoa.ni.gumu.na.nyeti.sana twahitaji.hekima.ya.Mungu.kupata.wenzetu.iwe.kwa.kuchagua.ama.kuchaguliwa.na.ndugu .ktk.kitabu.cha.Ndoa.yangu.kimeonyesha.kuwa.wanandoa.wengi.hawana.hamu.tena.ya.kuishi.na.wenzao.na.wanaishi.shingo.upande .why.iwe.hivyo
 
Hivi ni kwa nini ndugu hupenda kuingilia mahusiano ya wenzao? kuna faida gani ya kuoa/kuolewa kwa mtu wa kabila lako/kabila moja?
kuharibiana maisha tu, ndoa ikibuma hawachelewi kusema 'ujinga wake, alikubalije mke wa kuletewa!'
 
Mkuu Gagurito mwambie rafiki yako afanye kile ambacho atakisimamia mbele ya Mungu Kwani ndiye pekee anayejua yote. nidhamu za woga kwa Shangazi, mjomba, bibi, babu zimeshapitwa na wakati, hata Kama watatishia kumtenga asimamie ukweli Wa moyo wake Kwani ndiyo true love.
 
.nampa.pongezi.sana.huyo.mzee.na.wewe.kwa.nasaha.hizo .unajua.suala.la.ndoa.ni.gumu.na.nyeti.sana twahitaji.hekima.ya.Mungu.kupata.wenzetu.iwe.kwa.kuchagua.ama.kuchaguliwa.na.ndugu .ktk.kitabu.cha.Ndoa.yangu.kimeonyesha.kuwa.wanandoa.wengi.hawana.hamu.tena.ya.kuishi.na.wenzao.na.wanaishi.shingo.upande .why.iwe.hivyo
Asante sana mkuu, ktk hii field kunahaja ya kujifunza mengi!
 
argggggghhhh.bwana mambo ya kutafutiwa mke yalipitiwa na wakati ....afanye moyo wake unalotaka....siku maji yakishinda unga huko mbeleni hao ndugu zake watamsaidia????????
Kweli bwana, jamaa anastahili kuwa makini kwa hili, nitamwelekeza vizuri!
 
Mkuu Gagurito mwambie rafiki yako afanye kile ambacho atakisimamia mbele ya Mungu Kwani ndiye pekee anayejua yote. nidhamu za woga kwa Shangazi, mjomba, bibi, babu zimeshapitwa na wakati, hata Kama watatishia kumtenga asimamie ukweli Wa moyo wake Kwani ndiyo true love.
Kweli mkuu, nitamshahuri kwa hili.. Asante sana!
 
Najua anampenda sana mchaga bt shinikizo la ndugu ndio tatizo!

Mkuu moja kwa moja hapa kuna kitu unaficha, hivi kwenye red ulipoandika unamaanisha nini? Jamaa yako na ndugu zake ni wakabila, sema na wewe hapa unajaribu kuficha watu wasikushambulie tu...Hapo hakuna cha kufikiria wala nini moja kwa moja kama jamaa ako kweli ni mtu mzima I mean Over 18 swala la kuoa liko juu yake na sio juu ya wazazi wako maana huyo ni mke sio rafiki wala room mate au mfanyakazi mwenzio kuwa unachaguliwa...Mwambie aoe mapema, anaweza Oa hata yuko chuo...siku ya siku wazazi hawatakuwepo kukiwa nyumbani hakuivi ni yeye na mke wake.....
 
Back
Top Bottom