Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Date::10/2/2009Kamati kumhoji waziri kuhusu operesheni Loliondo
Exuper Kachenje
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga, atalazimika kutoa ufafanuzi mbele ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, kuhusu operesheni ya kuhamisha wananchi huko Loliondo, wilayani Ngorongoro.
Hatua hiyo inafuatia taarifa zinazohusu mkanganyiko kuhusu operesheni hiyo ya kuwahamisha wananchi kutoka katika pori tengefu ambalo linadaiwa kuwa sasa amepewa mwekezaji wa kigeni.
Pia kuna madai kuwa mwekezaji huyo amekuwa akiendesha vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wananchi wa eneo hilo, vikiwemo vinavyokiuka haki za binadamu, bila kuchukuliwa hatua.
Ratiba ya vikao vya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliyotolewa na ofisi ya Bunge Ijuma lililopita, inaonyesha waziri amepangiwa kutoa ufafanuzi wa opersheni hiyo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Mwangunga amepangiwa kufanya hivyo Oktoba 10 mwaka huu wakati kamati hiyo itakapokutana katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam.
"Ijumaa 09/10/09, Waziri kutoa ufafanuzi kuhusu operesheni inayoendelea Loliondo," inaonyesha ratiba hiyo ambayo Mwananchi ina nakala yake.
Hivi karibuni waziri Mwangunga alikaririwa akisema kuwa waliohamishwa katika pori hilo si Watanzania na kwamba jamii ya Wamasai kutoka Kenya.
Kwa mujibu wa waziri huyo, watu hao walifuata malisho, kufuatia ukame uliikumba nchi yao na kusababisha mifugo kukosa malisho.
Waziri wa Maliasili na Utalii, pia alisemahakuna ukiukwaji wa haki za ubinadamu uliofanyika katika operesheni hiyo.
Alisema wizara yake kwa kushirikiana na Tume ya Upangaji wa Matumizi ya Ardhi, imeazimia kutenga maeneo ya pori tengefu, ardhi ya vijiji kwa njia shirikishi.
Katika eneo hilo kuna zaidi ya taasisi 30 zinazofanya kazi huku baadhi zikitajwa kuhusika na mvutano uliopo.
Mwangunga amezielezea tatsisi hizo kuwa zinashindana kibiashara. Alisema wafugaji wana haki ya kuendelea kuishi katika maeneo mengine ya pori la Loliondo, ambayo si tishio kwa usalama wao.
Facebook
Exuper Kachenje
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga, atalazimika kutoa ufafanuzi mbele ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, kuhusu operesheni ya kuhamisha wananchi huko Loliondo, wilayani Ngorongoro.
Hatua hiyo inafuatia taarifa zinazohusu mkanganyiko kuhusu operesheni hiyo ya kuwahamisha wananchi kutoka katika pori tengefu ambalo linadaiwa kuwa sasa amepewa mwekezaji wa kigeni.
Pia kuna madai kuwa mwekezaji huyo amekuwa akiendesha vitendo vya unyanyasaji dhidi ya wananchi wa eneo hilo, vikiwemo vinavyokiuka haki za binadamu, bila kuchukuliwa hatua.
Ratiba ya vikao vya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliyotolewa na ofisi ya Bunge Ijuma lililopita, inaonyesha waziri amepangiwa kutoa ufafanuzi wa opersheni hiyo.
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, Mwangunga amepangiwa kufanya hivyo Oktoba 10 mwaka huu wakati kamati hiyo itakapokutana katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ndogo ya Bunge jijini Dar es Salaam.
"Ijumaa 09/10/09, Waziri kutoa ufafanuzi kuhusu operesheni inayoendelea Loliondo," inaonyesha ratiba hiyo ambayo Mwananchi ina nakala yake.
Hivi karibuni waziri Mwangunga alikaririwa akisema kuwa waliohamishwa katika pori hilo si Watanzania na kwamba jamii ya Wamasai kutoka Kenya.
Kwa mujibu wa waziri huyo, watu hao walifuata malisho, kufuatia ukame uliikumba nchi yao na kusababisha mifugo kukosa malisho.
Waziri wa Maliasili na Utalii, pia alisemahakuna ukiukwaji wa haki za ubinadamu uliofanyika katika operesheni hiyo.
Alisema wizara yake kwa kushirikiana na Tume ya Upangaji wa Matumizi ya Ardhi, imeazimia kutenga maeneo ya pori tengefu, ardhi ya vijiji kwa njia shirikishi.
Katika eneo hilo kuna zaidi ya taasisi 30 zinazofanya kazi huku baadhi zikitajwa kuhusika na mvutano uliopo.
Mwangunga amezielezea tatsisi hizo kuwa zinashindana kibiashara. Alisema wafugaji wana haki ya kuendelea kuishi katika maeneo mengine ya pori la Loliondo, ambayo si tishio kwa usalama wao.
Tuma maoni kwa Mhariri