Shamsa Mwangunga kuvaana na John Mnyika Ubungo

Kwa hali ilivyo sasa ubungo, hakuna atakayemchagua mbunge toka CCM,Mnyika ana nafasi ya kushinda. Mwangunga asubiri viti maalum.
 
Kuna habari pia kwamba yule vice chair wa UVCCM nae karata yake ataipeleka Ubungo! Kwahiyo kama ni kweli itakuwa J. Mnyika vs B. Malisa
 
Kumbe!!!! nimeanza kupata mwanga juzi juzi Mwangunga alikuwa mgeni rasmi kwenye Kanisa letu Mavurunza, Ubungo kumbe ameamua kuanzia huko!!! nikashangaa hivi huyu Muislam, samahani siyo udini, wamemuwaza wapi mpaka aje huku kumbeee !!!!! lisemwalo lipo na alichangamsha mnada kweli CCM siwawezi.
 
Kumbe!!!! nimeanza kupata mwanga juzi juzi Mwangunga alikuwa mgeni rasmi kwenye Kanisa letu Mavurunza, Ubungo kumbe ameamua kuanzia huko!!! nikashangaa hivi huyu Muislam, samahani siyo udini, wamemuwaza wapi mpaka aje huku kumbeee !!!!! lisemwalo lipo na alichangamsha mnada kweli CCM siwawezi.

Samahani kama nitakuwa nimekosea lakini ni msemo tuuu wanasema "usione nyani mjini ukataka kuanza kumrushia mawe.........."
 
Last edited:
Omutwale,waitu Shumalamu! La Nnape kugombea Ubungo hilo ni wazi siku nyingi linajulikana,Shamsa naona jimbo la Kongwa kaliona maji marefu maana Ndugai balaa na siasa bila shaka kanogewa nazo hivyo anahitaji jimbo,Mnyika ni wazi kwa umri wake atakuwa na ambitions kibao na ninasikia bongo yake inachemka(nasikia o-level alipata A kumi) na kwenye siasa ukiwa na bongo kali ni advantage because you think fast,diwani wa ubungo aitwaye Mringo naye anataka kujitosa kilingeni and indeed watch this guy kwa sababu amekuwa kwenye siasa za wilaya ya kinondoni muda mrefu na anamjua kila mtu,literally.Tusubiri si ajabu na wengine wakaja maana kabla Asha Migiro hajaenda UN ilisemekana naye alikuwa anajiandaa kupandisha bendera Ubungo,kunani Ubungo??????

Osingile Waitu,
Yetu macho tu
 
Kwa hali ilivyo sasa ubungo, hakuna atakayemchagua mbunge toka CCM,Mnyika


Hakuna mtu atakayeweza kucopete na Mnyika ndani ya Ubungo, jamaa anakubalika. Kusema ukweli jamaa ni kichwa cha Chadema ! Watu wanaozungumzia masuala ya elimu awajui lolote kuhusu local politics za hapo Ubungo .
 
Mwanyika anaweza kuwa mzuri compared na Mwangunga kama kweli habari hii ni confirmed, kura yangu itakwenda kwa Mnyika.
 
Sidhani kama ni sahihi kusema kuwa Shamsa anavaana na Mnyika kwasababu hajateuliwa bado na CCM kuwa ndo mgombea wao! Na bado wapo wengi wanaotajwa kuwania nafasi hiyo tena nadhani katika ranking Shamsa yuko mbali mno kupata nafasi hiyo!
Nadhani anataka kutengeneza njia tu akumbukwe uteuzi wa bwana mkubwa.
Nadhani pia kaanza vibaya sana kwa hoja mbili DINI ..kaanza kwa kujivisha utetezi wa waisilami......JINSIA.....analia apewe nafasi kuwakilisha jinsia wakati wamepewa nafaisi kibao za wanawake.
Majina mengine yanayotajwa ambayo nadhani yanaushindani mkubwa ni pamoja na,
1. Hawa Ng'umbi
2. Nape Nnauye
3.Mringo....diwani wa kimara
4. Na kwa mbali Benno Malisa!
 
Beno malissa........zamani nilijua vijana hawawezi kuwa mafisadi...
 
mnnyika ni moto wa petrol, sidhani huyo mama kama atauweza kuuzima, mi nadhani utamlipukia tu, hatapona mkuu.
 
yaani ukeli ni kwamba hata wakisema uchaguzi ni kesho japokuwa huyu mama ni waziri aliyepo madarakani hivi sasa,means bado ana nguvu kubwa ya serikali, lakini hawezi kufurukuta kwa mwanyika,na hilo liko wazi.Juzi nilimuona ktk runinga akipiga magoti kwa waislam, namnukuu, ''waislam wenzangu mungu akipenda ninategemea kugombea ubunge ktk jimbo la ubungo, sasa nikiwa kama muislamu mwenzenu naombeni msaada wenu'' mwisho wa kunukuu. mimi nikamshangaa sana huyu mama nilifikiri ni mtu makini kumbe bogas,kama nyerere angekuwa hai asingejaribu kuomba msaada kwa kutumia udini huyu mama,its true hata mimi ni muislam lakini stail aliyotumia huyu mama ni ya hovyo kabisa
 
Sidhani kama ni sahihi kusema kuwa Shamsa anavaana na Mnyika kwasababu hajateuliwa bado na CCM kuwa ndo mgombea wao! Na bado wapo wengi wanaotajwa kuwania nafasi hiyo tena nadhani katika ranking Shamsa yuko mbali mno kupata nafasi hiyo!
Nadhani anataka kutengeneza njia tu akumbukwe uteuzi wa bwana mkubwa.
Nadhani pia kaanza vibaya sana kwa hoja mbili DINI ..kaanza kwa kujivisha utetezi wa waisilami......JINSIA.....analia apewe nafasi kuwakilisha jinsia wakati wamepewa nafaisi kibao za wanawake.
Majina mengine yanayotajwa ambayo nadhani yanaushindani mkubwa ni pamoja na,
1. Hawa Ng'umbi
2. Nape Nnauye
3.Mringo....diwani wa kimara
4. Na kwa mbali Benno Malisa!

Kama Nape Nnauye atapitishwa kugombea Ubungo basi ni njama za kummaliza kisiasa maana hatafurukuta hata tone kwa bwana Mnyika. Ahesabu hasara!
 
ubungo ina wenyewe......
ubungo sio tena jimbo la majaribio.
huyo mama aende tu akatafute nafasi kijijini kwao.
wakazi wa ubungo tumeipokea kwa kebehi taarifa yake hiyo...
cha msingi namuomba tu akatafute majibu ya uchaguzi ya jimbo la ubungo ya mwaka 2005 kisha atapata jibu ubungo wanamuhitaji nani.
 
Nani hapa ana namba ya simu ya huyu mama ili nimpigie na kumpa onyo mapema asije pata aibu?.
 
Mwacheni sasa apumzike kidogo maana pressure mliyompa imekua ikimpanda tu subirini ishuke kidogo wanaJF.
 
Kwani Mzee Keenja amefulia tayari? Hatagombea?

Ni kweli kuwa Keenja ameamua kuwa hatagombea tena. Miaka kumi ya Ubunge imemtosha. Ila hilo la kufulia sijui unataka kumaanisha nini. Kwani Mkuu ulitaka akae muda gani? Si unajua kila mtu ana haki ya kuomba na kutokuomba kuchaguliwa? Kwani alitakiwa kushika kiti hicho hadi lini?

Ndiyo, Umepatia
Kama unakumbuka vizuri hata 2005 ni miongoni mwa Wabunge ambao JK alikuwa amegoma kuwavusha kitanzi shingoni. Na hata alipokubali kuwanadi walizomewa jukwaani mbele ya JK.

Hivi unataka kuniambia kuwa JK ndie aliyekuwa akivusha wagombea vitanzi? Mbona unanishangaza Mkuu? Maana kama unakumbuka vizuri, JK alishiriki pia kampeni na kumnadi Keenja kuwa Mbunge mwaka 2005.

Sikumbuki alizomewa wapi na nani. Maana nilikuwepo kwenye mikutano yote ya kampeni na sikuliona hilo. Labda kama alizomewa kwenye ndoto zako. Maana wengi waliota.


Keenja ni miongoni mwa wabunge wengi wa CCM walioshindwa vibaya 2005 katika majimbo ya Dar, Msimamizi wa uchaguzi "mkurenzi wa municipal ya Kinondoni" Edgar Berege sijui kama bado anashikilia nafasi hii, ilibidi atumie mbinu zao za kupika matokeo ya kura, kumtangaza mshindi.
Hahahaha, wakati mwingine nadhani utani unazidi busara. Keenja alishinda Ubungo kwa asilimia 54 ya kura zote zilizopigwa. Wagombea waliokuwepo walikuwa 13 (hapo ndipo walipojikaanga - siri yako). Ina maana hata kama wagombea wote wa upinzani wangeunganisha kura zao, bado wangekuwa wameshindwa.

Berege alikuwa ndie msimamizi wa uchaguzi (sahihi kabisa). Alizuiwa na Mnyika kutangaza matokeo kwa kuwa Mnyika alidhani matokeo yalikuwa batili. Alipewa nafasi zote za kuyahakiki akashindwa kuyakubali pia. Ndipo ilipoonekana kuwa nia yake ilikuwa ni ya kutaka kudai matokeo yalicheleweshwa ili aonekane ameibiwa kura, ikabidi kulazimika kutangazwa kwa matokeo bila kujali kama Mnyika anayakubali au lah. Hivyo ndivyo ilivyokuwa.
Sisi hapa tupige kelele tu, lakini bila kuwa na Tume huru ya uchaguzi CCM itaendelea kupanga matokeo ya kura kwa kadiri wanavyoona inafaa. Hutu tuviti wanatowaachia wapinzani ni janja ya kuwaonesha wahisani kuwa Tanzania kuna demokrasia.
Sahihi kabisa. Tume huru ya uchaguzi inahitajika ili kuwa na haki zaidi katika uchaguzi. Tume iliyopo imeundwa ikiwa na upendeleo wa wazi kwa mwajiri wake ambae nae pia ni mgombea.

Kilichomwangusha zaidi John Mnyika ni kutegemea mawakala kutoka UDSM. Kwa bahati mbaya kura zilipingwa baadhi ya Faculty wakiwa kwenye mitihani na hivyo Mawakala toka UDSM wengi hawakwenda vituoni na hivyo kutoa mwanya wa wazi kwa CCM na Keenja kuchezea matokeo watakavyo. Hii haimaanishi kuwa napunguza ukweli katika hoja yako ya Tume Huru bali naonyesha mwanya wa ziada.

Mkuu Omutwale, UDSM ina kura kiasi gani mpaka udhani kuwa Mnyika aliangushwa na makada wa chuo hicho? Ukweli ni kwamba, Mnyika alikubalika sana UDSM na alipata kura nyingi pale kulinganisha na wagombea wote. Ila kura nyingi zaidi ziko mitaani. Huko tunakoishi sote.

Makosa ya Mnyika Ubungo, ni ya kiufundi tu. Nayo ni katika kampeni zake mitaani. Mnyika ni mzuri sana jukwaani. Inahitaji mbinu zaidi za kutafuta kura mitaani ili aweze kushinda. Atashinda siku moja lakini sio 2010. Sorry kama nitakuwa nimewaudhi baadhi ya watu kwa kusema hivyo. Iko wazi sana kuwa ili Mnyika ashinde Ubungo, itabidi aibe wanachama wengi sana wa CCM. CCM iko imara sana Ubungo. Yeyote atakaepitishwa kuwa mgombea wa Ubunge kwa ticket ya CCM pale atashinda tu. Sorry again. Kwanini nasema hivyo, ni suala linalohitaji maelezo marefu.

- Keenja ameamua kutogombea tena baada ya kufulia na kukamulia jimbo, kwa hiyo hapo Ubungo kwa dataz nilizonazo tutegemee wana-JF wawili kujitosa, Mnyika anataka kuendelea na shule lakini kuna wanaomshinikiza kujitosa, atakumbana na another JF,

Kauli hizi si tulizozizoea kutoka kwako Mkuu. Una busara zaidi ya hizo hapo juu.


- Mwagunga, angetafuta pengine, hapa ni moto wa kuotea mbali, maana nimekuwa nikishiriki mwenyewe kwenye kampeni za one on one na prominent wa jimbo hili, katika kujaribu kumsaidia a JF member unajua hili jimbo ni exceptional maana lina wasomi wengi sana, huenda hata kuliko majimbo yote nchini.

Sasa Mwangunga aende kugombea wapi, na nani anaefaa zaidi kugombea Ubungo, Mkuu? Nadhani kila mtu ana haki sawa ya kuomba kuchaguliwa. Yeyote kati ya wanaotajwa ni vyema wakapewa nafasi sawa (walau kwa sasa) wanaopiga kura ni wengi, uamuzi wao ni siri kubwa. Sijui kama tunaweza kutabiri vyema nani atakaeshinda. Tusibiri tuone. Kampeni halali hazijaanza. Lolote linaweza kutokea.


Kuna wengine wanaotajwa kuwania kiti hicho vile vile. Wapo akina Prof. Wangwe, Nape Mnauye (japokuwa anatajwa pia kutaka kugombea Kawe), Mahmoud Mringo Diwani wa Kimara, Hawa Ng'umbi, na wengine watajitokeza tu.
 
yaani ukeli ni kwamba hata wakisema uchaguzi ni kesho japokuwa huyu mama ni waziri aliyepo madarakani hivi sasa,means bado ana nguvu kubwa ya serikali, lakini hawezi kufurukuta kwa mwanyika,na hilo liko wazi.Juzi nilimuona ktk runinga akipiga magoti kwa waislam, namnukuu, ''waislam wenzangu mungu akipenda ninategemea kugombea ubunge ktk jimbo la ubungo, sasa nikiwa kama muislamu mwenzenu naombeni msaada wenu'' mwisho wa kunukuu. mimi nikamshangaa sana huyu mama nilifikiri ni mtu makini kumbe bogas,kama nyerere angekuwa hai asingejaribu kuomba msaada kwa kutumia udini huyu mama,its true hata mimi ni muislam lakini stail aliyotumia huyu mama ni ya hovyo kabisa
Hata mimi nilimuona channel 10 akisema haya mambo. Nilishangaa kwamba kama kampeni zikiamia nyumba za ibada uchaguzi utakuwa mgumu sana sana.
Na naona kama kaanza na wengine watakwenda makanisani kuomba kura kwa watu wao.
Na hapo ndipo kivumbi kitakapotimka.
Ni kama naota vile!?
 
Back
Top Bottom