Shambulio la marekani tumejifunza nini

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
MASHAMBULIZI YA MAREKANI SOMALIA TUMEJIFUNZA NINI

Ndugu

Tumeona siku za karibuni Jeshi la marekani kwa kutumia ndege zake zilifanikiwa kumuuwa gaidi mmoja raia wa Kenya waliyekuwa wanamtafuta sana toka balozi zao zilipolipuliwa jijini dar es salaam na nairobi .

Nimeshangaa kwanini serikali ya Kenya haikuingia yenyewe ndani ya Somalia kwenda kumtafuta gaidi huyo kama walikuwa wanajua alipo na taarifa za uwepo wake katika eneo hilo , badala yake wameruhusu jeshi la marekani kushambulia eneo hilo na kufanikiwa kumuuwa gaidi huyo

Nachouliza nchi yetu ya tanzania tumejiandaa vipi na vitendo hivi vya jeshi la marekani kuingilia mipaka ya nchi zingine kwa matakwa yao wenyewe , serikali ya Kenya haijatoa tamko lolote la maana kwa nchi ya marekani wala umoja wan chi za afrika nao umekaa kimya tu kuhusu shambulio hilo pamoja na kwamba wamezoea kufanya mashambulizi siku za nyuma .

Binafsi sipendi harakati za kigaidi mahala popote lakini pia sipendi kuona nchi zinavyovamia nchi zingine kwenye kuuwa watuhumiwa haswa kwa njia hizo zilizotumika kesho kutwa tunaweza kusikia wameenda kupiga mwanza kutafuta magaidi

Na ndio kwanza wanatafuta nafasi ya kuanzisha kituo chao cha kijeshi kwa nchi za afrika , naamini huko mbeleni kutakuwa na matishio makubwa zaidi ya hili kwa nchi hiyo kuamua kuvamia nchi zingine
 
Binafsi sipendi harakati za kigaidi mahala popote lakini pia sipendi kuona nchi zinavyovamia nchi zingine kwenye kuuwa watuhumiwa haswa kwa njia hizo zilizotumika kesho kutwa tunaweza kusikia wameenda kupiga mwanza kutafuta magaidi

Na ndio kwanza wanatafuta nafasi ya kuanzisha kituo chao cha kijeshi kwa nchi za afrika , naamini huko mbeleni kutakuwa na matishio makubwa zaidi ya hili kwa nchi hiyo kuamua kuvamia nchi zingine


Nenda mbali zaidi ya kutokupenda.

Do something about it to show your seriousness!

Innocent pals are killed.
 
sasa unajua mimi hapo ndipo ninapokushangaa maana kwana umesema kwamba unashangaa serikali ya kenya haikuingia yenyewe kumsaka gaidi huyo sasa unataka marekani nao wakae kimya kama kenya ili apange mbinu zingine shida ya sisi africa hatujishughulishi sasa mtu yuko kenya lakini gaidi mpaka auliwe na mtu kutoka marekani jamani hii nini hasa
 
kweli dada Kelly Tulivamia Uganda mbona hatukusema nini? Tulikwenda kumpiga nduli pale Kagera au ilikuwa gear ya kuingilia tu, mpaka leo Tanzania haikukaa sawa, acha we ufisadi ulianzia mbali kweli
 
mimi napongeza wamarekani kwa kazi nzuri ya kupambana na ugaidi, kwanza hata wangeweka kambi yao TZ ni poa tu kwa sababu sisi tumeshindwa hata kutafuta mabomu ya mbagala je al qaeda tutawaweza? ambao wanawasumbua hata marekani wenyewe?

Kuhusu issue ya somalia, kwanza kenya hawakujua kwamba nabhan yupo somalia kutokana na weakness ktk intel yao sasa wangeingia vipi huko while hawajui kama adui yupo.
 
Ni kinyume cha haki za utawala wa nchi. Lakini kwa kuwa marekani ndio polisi wa Duniya basi ndio anapeta
 
Yule gaidi kauwawa Somalia na ndio alikimbilia...ujue kuwa anahusika pia kushambulia interest za marekani...apart from ndege ya israel an hotel za mombasa ku target wamarekani na israel...Somalia wahalifu wote wanakimbilia huko..kabla hawajasumbua wengine they have to be neutralized
 
:(
MASHAMBULIZI YA MAREKANI SOMALIA TUMEJIFUNZA NINI

Ndugu

Tumeona siku za karibuni Jeshi la marekani kwa kutumia ndege zake zilifanikiwa kumuuwa gaidi mmoja raia wa Kenya waliyekuwa wanamtafuta sana toka balozi zao zilipolipuliwa jijini dar es salaam na nairobi .

Nimeshangaa kwanini serikali ya Kenya haikuingia yenyewe ndani ya Somalia kwenda kumtafuta gaidi huyo kama walikuwa wanajua alipo na taarifa za uwepo wake katika eneo hilo , badala yake wameruhusu jeshi la marekani kushambulia eneo hilo na kufanikiwa kumuuwa gaidi huyo

Nachouliza nchi yetu ya tanzania tumejiandaa vipi na vitendo hivi vya jeshi la marekani kuingilia mipaka ya nchi zingine kwa matakwa yao wenyewe , serikali ya Kenya haijatoa tamko lolote la maana kwa nchi ya marekani wala umoja wan chi za afrika nao umekaa kimya tu kuhusu shambulio hilo pamoja na kwamba wamezoea kufanya mashambulizi siku za nyuma .

Binafsi sipendi harakati za kigaidi mahala popote lakini pia sipendi kuona nchi zinavyovamia nchi zingine kwenye kuuwa watuhumiwa haswa kwa njia hizo zilizotumika kesho kutwa tunaweza kusikia wameenda kupiga mwanza kutafuta magaidi

Na ndio kwanza wanatafuta nafasi ya kuanzisha kituo chao cha kijeshi kwa nchi za afrika , naamini huko mbeleni kutakuwa na matishio makubwa zaidi ya hili kwa nchi hiyo kuamua kuvamia nchi zingine

Mkuu inaelekea uelewa wako wa haya masual ya kufuatilia magaidi yana walakin.
Kwanza huwezi kulinganisha Kenya au Tanzania kwa uwezo wa kuwafuatilia hao magaidi na Marekani.
Kama si Marekani tusingewajua waliotehga mabomu ubalozi wa Marekani Kenya na Tanzania.Hii ni kwa sababu ugaidi huu asili yake ni mtandao ambao wala hatungeweza kuufuatilia.Uwezo wa vitengo vyetu vya ulinzi unaeleweka vyema.
Leo ni miaka 11 toka kulipuliwa mabomu balozi za Marekani Dar es salaam na Nairobi.Leo umma wa kitanzania bado uko gizani juu ya mlolongo mzima wa jambo hili.
Hatuwezi kujifananisha na Marekani katika bajeti kufanya investigation,surveillance na hatimaye kufanya surgical execution ya kuua hawa magaidi.
Kwa upande wangu mimi nawapongeza Marekani kwa hilo.Tukumbuke kuwa katika milipuko ya DSM na Nairobi karubu wote waloi uwawa ni ndugu zetu.
Hivyo basi kama magaidi hao watakuwepo hapa kwetu na wanajificha tukipata msaada wa aina yoyote kuna ubaya gani
Vile vile kumbuka hivi karibuni kulikuwepo na mazoezi ya kijeshi kati ya nchi zetu za Afrika Mashariki katika kujiweka sawa na tishio la magaidi.
 
Back
Top Bottom