Shairi: Mavi ya Mbuzi

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
1,985
1,282
MAVI YA MBUZI.
1.
Nilidhani ni karanga, kumbe ni mavi ya mbuzi,
Sikudhani ni pakanga, katika wangu mchuzi,
Kuamini mtu janga, jiandae na mauzi.
Kuna mambo ya kuchunga, wakati wa maamuzi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
2.
Nilidhani ni maziwa, kumbe ni tui la nazi,
Ati nimependelewa, na mola wangu Azizi,
Kumbe janga nimepewa, wallahi si kumaizi,
Yale niliyotendewa, mlipaji ni mwenyezi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
3.
Nilidhani ni malaika, kumbe adui shetani,
Mimi nilimchunuka, tena nilimuamini,
Kumbe vile anicheka, aniingize mjini,
Akapanga kuchomoka, na sanduku la thamani.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
4.
Nilidhani muumini, alo na sifa stahiki,
Kumbe najenga imani, kwa kiumbe mnafiki,
Akafanya ushetani, kanirushia mkuki,
Namshukuru Manani, yu mtupu mnafiki,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
5.
Nilidhani ni kitanda, kumbe tusi la maiti,
Kule kote kunikanda, ni mbinu zake afriti,
Ili apate niponda, aibe japo katiti,
Mja alivyonitenda, nilitamani mauti,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
6.
Aheri shetani jini, kuliko shetani mtu,
Mbago hata subiani, mtumaji hawi chatu,
Hata ndugu wa ndani, kumwamini sithubutu,
Aweza kuwa shetwani, anipige na mtutu.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
7.
Unapoweka imani, uweke na tahadhari,
Silaha iwe bindoni, si msaahu Qahari
Ujue wafanya nini, inapotokea shari,
Kilio chafaa nini, mtenda hana habari,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
8.
Yupo fanani bubusa, katika sanaa zake?
Yaani aso yagusa, mambo ya jamii yake?
Au ashindwe papasa, sakafu ya moyo wake?
Kama yupo ni tutusa, kina shida kichwa chake,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
9.
Niliuchonga ujiti, nichore yalo nisibu,
Nikafuata shuruti, pamoja na taratibu,
Wino wa chani kiwiti, ukakinakshi kitabu,
Mwisho ikawa kunuti, nipate chuma thawabu,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
10.
Sijui niweke koma, ama niweke mkato,
Wenye kutendwa hukoma, ama hukwepa kong'oto,
Sitarudia pogoma, kama mbogo aso mato,
Kuwa boya nimekoma, sikiza msaka sato.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

Dotto Rangimoto Chamchua.(Njano5)
mzalendo.njano5@gmail.com
0762845394/0784845394 Morogoro

Limechapishwa ktk gazet la mwanancji la tarehe 1/01/2016

kwa mashairi mengine kama hayo waweza kujisomea katika blogu yangu, kwenye icon ya mashairi utabofya hapo kisha utayaona mashairi mengi nilitotunga

SASA HAMSINI RASI, HAMSINI MAJINUNI. | Kisima Cha Jangwani.
 

Attachments

  • mavi 2.jpg
    mavi 2.jpg
    53.5 KB · Views: 86
  • mavi.jpg
    mavi.jpg
    47.9 KB · Views: 87
haya ndo yalomkuta lowassa!
alimwamini akabwaga moyo wake kumbe la haullah, kweli amini kivuli chako pekee!
 
Penda sana kazi hizi za mashairi big up kaka kwa shair zuri lenye ujumbe lukuki
 
A
MAVI YA MBUZI.
1.
Nilidhani ni karanga, kumbe ni mavi ya mbuzi,
Sikudhani ni pakanga, katika wangu mchuzi,
Kuamini mtu janga, jiandae na mauzi.
Kuna mambo ya kuchunga, wakati wa maamuzi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
2.
Nilidhani ni maziwa, kumbe ni tui la nazi,
Ati nimependelewa, na mola wangu Azizi,
Kumbe janga nimepewa, wallahi si kumaizi,
Yale niliyotendewa, mlipaji ni mwenyezi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
3.
Nilidhani ni malaika, kumbe adui shetani,
Mimi nilimchunuka, tena nilimuamini,
Kumbe vile anicheka, aniingize mjini,
Akapanga kuchomoka, na sanduku la thamani.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
4.
Nilidhani muumini, alo na sifa stahiki,
Kumbe najenga imani, kwa kiumbe mnafiki,
Akafanya ushetani, kanirushia mkuki,
Namshukuru Manani, yu mtupu mnafiki,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
5.
Nilidhani ni kitanda, kumbe tusi la maiti,
Kule kote kunikanda, ni mbinu zake afriti,
Ili apate niponda, aibe japo katiti,
Mja alivyonitenda, nilitamani mauti,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
6.
Aheri shetani jini, kuliko shetani mtu,
Mbago hata subiani, mtumaji hawi chatu,
Hata ndugu wa ndani, kumwamini sithubutu,
Aweza kuwa shetwani, anipige na mtutu.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
7.
Unapoweka imani, uweke na tahadhari,
Silaha iwe bindoni, si msaahu Qahari
Ujue wafanya nini, inapotokea shari,
Kilio chafaa nini, mtenda hana habari,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
8.
Yupo fanani bubusa, katika sanaa zake?
Yaani aso yagusa, mambo ya jamii yake?
Au ashindwe papasa, sakafu ya moyo wake?
Kama yupo ni tutusa, kina shida kichwa chake,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
9.
Niliuchonga ujiti, nichore yalo nisibu,
Nikafuata shuruti, pamoja na taratibu,
Wino wa chani kiwiti, ukakinakshi kitabu,
Mwisho ikawa kunuti, nipate chuma thawabu,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.
10.
Sijui niweke koma, ama niweke mkato,
Wenye kutendwa hukoma, ama hukwepa kong'oto,
Sitarudia pogoma, kama mbogo aso mato,
Kuwa boya nimekoma, sikiza msaka sato.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

Dotto Rangimoto Chamchua.(Njano5)
mzalendo.njano5@gmail.com
0762845394/0784845394 Morogoro

Limechapishwa ktk gazet la mwanancji la tarehe 1/01/2016

kwa mashairi mengine kama hayo waweza kujisomea katika blogu yangu, kwenye icon ya mashairi utabofya hapo kisha utayaona mashairi mengi nilitotunga

SASA HAMSINI RASI, HAMSINI MAJINUNI. | Kisima Cha Jangwani.
ACT wamesha kugeuka nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom