Shairi la Leo...........

CAMARADERIE

JF-Expert Member
Mar 3, 2011
4,419
1,920
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,

Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.
 
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,

Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.
Kofia nakuvulia, Camaraderie hima,
Ushairi metulia, Nakupatia heshima,
Vina umevipatia, Pia nayo mizania
Hakika nimefikiri, kabla sijakupongeza.

Narudi kitandani, kufikiri kwa kina.
 
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,

Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.
Shahiri limeeleweka hasa kwa wenye akili timamu,
Endelea kutujuza hasa kwa yale mema.
 
fesi buku umkweli, mapenzi yanaraha duniani.shairi sio kubeli, rahayake ipo kichwani.tusi lete ufedhuli, tuyasomapo gazetini.
ok na mm nna shairi languushikwapo shkamana kilichoko mfukoni mwako ndio chako, usipigie hesabu cha mwenzako!!!!
 
Fikiri zako fikira, ufikiri kila tendo,
Fikiri lilo na dhara, ufikiri na Ia pendo,
Fikiri lilo tohara, ufikiri na uvundo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri sana dunia, ina mzuri mdundo,
Fikiri sana yalia, ina mzuri mshindo,
Fikiri mwisho sikia, unapasuka msondo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Fikiri ndugu dahari, dunia ina mikondo,
Fikiri hizi habari, ni kushuka na mipando,
Fikiri dunia pori, chaka Ia uwi na kondo,
Fikiri fikiri tendo, la amani na busara.

Fikiri dau muundi, muunda dau muundo,
Fikiri lende kilindi, daule likaze mwendo,
Fikiri dau halendi, nguvu za dau upondo,

Fikiri ninakariri, usiwe mwenye mfundo,
Fikiri tena fikiri, kila ovu liwe kando,
Fikiri mno hatari, ukiwa na mbovu nyendo,
Fikiri fikiri tendo, Ia amani na busara.

Camarade wa Luthuli,siyo yule wa kimango ,
Usia ka warasuli,umefikia viwango,
Sije leta ufedhuli,wakaharibu mpango,
Ulonena ninakili,yamesheheni mafunzo
 
Fikiri lililo mbele , la nyuma liweke kando
Fikiri usiwe msukule, utakosa kaa na gando
Fikiri acha kelele , kimya kimya uwe mwendo
Fikiri hili na lile , uziepuke skendo

Fikiri utafakari , dunia tambara bovu
Fikiri utahadhari, usije acha makovu
Fikiri kwa Indhari, uache wako utovu
Fikiri usitahayari , epukana na uchovu

Fikiria familia , yako ilokuzunguka
Fikiria daharia, zinavyokupukutika
Fikiria usijelia , usije ukaumbuka
Fikiria zingatia, maisha yalivyochafuka

Fikiria wenye njaa, kama wewe ushatoka
Fikiria wanaotambaa, kama waweza kuruka
Fikiria walivyozagaa , mayatima walochoka
Fikiria kila saa, ni wapi uliposhika?
 
Fikiri lililo mbele , la nyuma liweke kando
Fikiri usiwe msukule, utakosa kaa na gando
Fikiri acha kelele , kimya kimya uwe mwendo
Fikiri hili na lile , uziepuke skendo

Fikiri utafakari , dunia tambara bovu
Fikiri utahadhari, usije acha makovu
Fikiri kwa Indhari, uache wako utovu
Fikiri usitahayari , epukana na uchovu

Fikiria familia , yako ilokuzunguka
Fikiria daharia, zinavyokupukutika
Fikiria usijelia , usije ukaumbuka
Fikiria zingatia, maisha yalivyochafuka

Fikiria wenye njaa, kama wewe ushatoka
Fikiria wanaotambaa, kama waweza kuruka
Fikiria walivyozagaa , mayatima walochoka
Fikiria kila saa, ni wapi uliposhika?
Hahahaha.......Fellow tablet katika kufikiri na kutafakari.......ngoja niendelee kumla mbuzi wa iddi kwanza.
 
Titi la mama litamu,hata likiwa la mbwa,
Kiswahili naazimu,sifayo iliyofumbwa,
Kwa wasiokufahamu,niimbe ilivyo kubwa,
Toka kama mlizamu, funika palipozibwa,
Titile mama litamu ,Jingine halishi hamu.

Lugha yangu ya utoto,hata sasa nimekua,
Tangu ulimi mzito,sasa kusema najua,
Ni sawa na manukato,moyoni mwangu na pua,
Pori bahari na mto,napita nikitumia,
Titile mama litamu,jingine halishi hamu.
 
Namba nawe mlimwengu, pulikiza matamko
Nikweleze neno langu, uzinduwe bongo lako
Nayo nda M'ngu si yangu, na ayani haya yako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

Simama uitete, usivikhofu vituko
Aliyo nayo mwendee, akupe kilicho chako
Akipinga mlemee, mwandame kulla endako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

Amkani mulolala,na wenye sikio koko
Isiwe mato kulola,natutizame twendako
Tuwate na kuduwala,usingizi si mashiko
Uwatapo haki yako,utaingiya motoni

Teteya kwa kula hali, usiche misukosuko
Siche wingi wala mali,sabilisha roho yako
Unyonge usikubali, ukaonewa kwa chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

Siche kifaru na ndovu, wangazidi nguvu zako
Wapempe kwa uwekevu, unusuru haki yako
Siandame wapumbavu,kilicho chako ni chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni

Cha mtu hakifitiki,kikafungiwa kiliko
Huzuka kikawa hiki,kazana utwae chako
Uwatapo yako haki,fahamu ni dhara kwako
Leo na kwa Mola wako,utaingiya motoni

Fumbuwa unyang'arize, uone duniya yako
Bure sijiangamize,kuangalia wendako
Utatupa upoteze,wende ambapo si pako
Uwatapo haki yako,utaingiya motoni

Kadhalika nako pia,huko ambako sikwako
Huwezi kujitetea,wala huwi na mashiko
Basi iwaze duniya,kwani ya kale hayako
Uwatapo haki yako ,utaingiya motoni

Kadi tamati shairi,sitii la ongezeko
Mwanati iwa tayari, utete haki yako
Unyonge usiukiri,Jifunge ufe kwa chako
Uwatapo haki yako, utaingiya motoni
 
Fikiri hii dunia, ni wapi ilipotoka
Fikiri na jinsia, kisa cha kutenganika
Fikiri viumbe pia, vile walivyoumbika
Fikiri jee ngamia, nundule lahitajika?

Fikiri na macho yake, yenye vizibo viwili
Fikiri na mwili wake, kiu kustahamili
Fikiri na kwato zake, moto wa jangwa himili
Fikiri muumba wake, muweza wa kila hili

Fikiri nae farasi, aendae akipuma
Fikiri na yake kasi, nguvuze zenye kuvuma
Fikiri na ufanisi, pale unapo mtuma
Fikiri jitanafasi, jisogeze kwenye mema
 
Tulikuwa tunapewa dozi hizi mashuleni........na Malenga wetu RTD!.......yule jamaa sijui kaishia wapi aliyekuwa akitusomea mashairi redioni
 
Back
Top Bottom