Shairi - kisima nimekiacha

UTATA

Nakupa heri ya mwaka, Mola atujalie
Atujazie fanaka, mabaya tuyakimbie
Atupe zake baraka, wachawi watukimbie
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Choveki nakutuma, Sindano nitafutie
Kwa Macheni amezama, asubuhi mdamkie
Mpe zangu karama, akili imfungukie
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama hana utata, mtoto wa kiungwana
Jando amelipata, masomo walimshona
Akili ameipata, busara zipo bayana
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama hana madhila, kajaa furaha tele
Ni mtu mwenye fadhila, hajipendei kelele
Usije ntia hila, kwa wivu uliotele
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama mtu makini, hula kwa kuchagua
Hana umasikini, wa kushindwa kutambua
Mola kanipa dini, vya halali navijua
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama namalizia, Kibaranga najiendea
Chelangwa nitamwambia, mjini kutembelea
Maneno kukupatia, utuondelee fedhea
Hakika nakuapia, Chama sina uduvi

Chama
Gongo la Mboto DSM


UUNGWANA NI VITENDO

Misifa wajisifia, wazidi kunishangaza
kwa mema wajipambia, tena wazi watangaza
watu walishasikia, sumu uliisambaza
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na mema umepuuza, kwa jando ulopitia
Hili nimechunguza, mafunzo hukushikia
wabaki sasa kucheza, mjini wakusifia
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Siwezi kuwa na wivu, kwa yako hiyo tabia
vipi mola nimuovu, mabaya kujisifia
Niombayo kwake hofu, ya shari kuyakimbia
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Uturi sasa wa nini, na hewa ulichafua
kuvisifu vya mjini, raha wajua tumbua
kila siku kwa macheni, vinyeo wavipangua
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na mara umegeuka, eti wala kwa makini
wajua kweli zunguka, acha wako ufitini
Ni haya imekushika, umeacha vya gizani?
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Fadhila unafadhili, wadai huna kelele
vipi upande wa pili, umeiacha misele?
Mtani mwendo badili, achana na misukule
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na iwapo nakukwaza, naomba unisamehe
Ila wacha kujikweza, punguza na starehe
Ya dunia hutoweza, uliza wako mashehe
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Ni mengi nimeyasema, kwa hapa ninasimama
Na mola mwenye rehema, akupe yenye karama
Azidishe ya neema, mola wetu yu karima
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako


SMG
 
UUNGWANA NI VITENDO

Misifa wajisifia, wazidi kunishangaza
kwa mema wajipambia, tena wazi watangaza
watu walishasikia, sumu uliisambaza
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na mema umepuuza, kwa jando ulopitia
Hili nimechunguza, mafunzo hukushikia
wabaki sasa kucheza, mjini wakusifia
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Siwezi kuwa na wivu, kwa yako hiyo tabia
vipi mola nimuovu, mabaya kujisifia
Niombayo kwake hofu, ya shari kuyakimbia
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Uturi sasa wa nini, na hewa ulichafua
kuvisifu vya mjini, raha wajua tumbua
kila siku kwa macheni, vinyeo wavipangua
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na mara umegeuka, eti wala kwa makini
wajua kweli zunguka, acha wako ufitini
Ni haya imekushika, umeacha vya gizani?
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Fadhila unafadhili, wadai huna kelele
vipi upande wa pili, umeiacha misele?
Mtani mwendo badili, achana na misukule
Uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Na iwapo nakukwaza, naomba unisamehe
Ila wacha kujikweza, punguza na starehe
Ya dunia hutoweza, uliza wako mashehe
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako

Ni mengi nimeyasema, kwa hapa ninasimama
Na mola mwenye rehema, akupe yenye karama
Azidishe ya neema, mola wetu yu karima
uungwana ni vitendo, twapima maneno yako


SMG

KARIBU TANGA

Mola wangu karima, hakika kanijalia
Kanipa nyingi hekima, macho kanifungulia
Sina ujanja wa kima, hilo nakubalia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Ukweli nakwambia, sina nikifichacho
Maneno yangu sikia, nasema bila mipasho
Fadhila nasadikia, pasina roho ya korosho
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Sindano nakualika, nyumbani karibia
Ule mseto hakika, na nguru wa kunukia
Utoe zako hamaka, upate jifurahia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Usiogope fadhila, watanga ni jadi yetu
Fadhila kwetu jalala, jione mtu wa kwetu
Na kitanda utalala, upate raha za kwetu
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Mchumba nikupatie, mwenye adili sawia
Ndoa iangukie, halali upate jilia
Furaha zikurudie, Mola atakujalia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Na dini tukufundishe, akili ipate tulia
Maadili turudishe, tusije pata kulia
Tamaa zako ziishe, nuru ipate jazia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Mjadala naufunga, Chama najiendea
Karibu nyumbani Tanga, ubaki kujisemea
Usije tia nanga, Tanga ukafemea
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
KARIBU TANGA

Mola wangu karima, hakika kanijalia
Kanipa nyingi hekima, macho kanifungulia
Sina ujanja wa kima, hilo nakubalia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Ukweli nakwambia, sina nikifichacho
Maneno yangu sikia, nasema bila mipasho
Fadhila nasadikia, pasina roho ya korosho
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Sindano nakualika, nyumbani karibia
Ule mseto hakika, na nguru wa kunukia
Utoe zako hamaka, upate jifurahia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Usiogope fadhila, watanga ni jadi yetu
Fadhila kwetu jalala, jione mtu wa kwetu
Na kitanda utalala, upate raha za kwetu
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Mchumba nikupatie, mwenye adili sawia
Ndoa iangukie, halali upate jilia
Furaha zikurudie, Mola atakujalia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Na dini tukufundishe, akili ipate tulia
Maadili turudishe, tusije pata kulia
Tamaa zako ziishe, nuru ipate jazia
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Mjadala naufunga, Chama najiendea
Karibu nyumbani Tanga, ubaki kujisemea
Usije tia nanga, Tanga ukafemea
Karibu mtani nyumbani, uingie mahabani

Chama
Gongo la Mboto DSM


NA TANGA NDIO NYUMBANI

Binadamu si kamili, tuombe istifara
Mola wetu muhimili, tujaze yenye busara
Tuepushe na batili, na nyoyo ziwe imara
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Yarabi tupe shufaa, tuondoshe matatani
Tukinge na mabalaa, akhera na duniani
Maisha haya hadaa, tuepushie shetani
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Namshukuru jalia, muongozo nilipata
Chuoni kuhudhuria, suna hadithi nafata
Si kama najisifia, ya dini sina utata
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Mtani ninashukuru, Tanga kunikaribisha
Mji uso na kufuru, ni mengi yenye bashasha
Kibwando Bada na Nguru, hamu haiwezi kwisha
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Ni chuda ninatokea, ndio kwenye maskani
Bakwata nilisomea, miaka ya themanini
wewe wapi mebobea, nijuze basi mtani
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Vitongoji navijua, vyote vya Tanga mjini
Na kote wanitambua, Tanga mimi si mgeni
Uliza hata washua, mabawa na chumbageni
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Nadhani tukaribishe, ndugu zetu wa kusini
waje wajipumzishe, kwa raha za jasmini
wasahau mishemishe, wakandwe mdalasini
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Mapenzi yale ya Tanga, hayahitaji vileo
Mambo udi kungu manga, kitandani kipepeo
Na kuna mambo ya kanga, waoshwa na pembejeo
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani

Swahiba basi nambie, ni wapi unatokea
Nataka nijipangie, niweze kuja tembea
Na mengi tujadilie, tujenge na mazoea
Tanga nishakaribia, na Tanga ndio nyumbani


Sindano Mwana wa Ganzi (SMG)
 
CHUMBAGENI

Mwalimu Hemedi makini, elimu yake si haba
Maadili yenye fani, yenye ubora kabakaba
Sindano rudi nyumbani, uje upate mahaba
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Chuda mji wangu, vidudu nimesoma
Ngamiani ni kwangu, malaria nimepima
Maumau timu yangu, Yuda niliwatema
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Chumbageni karibu, nipitie Sembuyagi
Usije kuyaharibu, kwa kunywa konyagi
Yatakuwa maajabu, ukionja lagilagi
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Ukifika kwa Kipevu, muulize Mwanaidi
Usilete uerevu, na kujitia mkaidi
Kuwa mvumilivu, komamanga ufaidi
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia

Chama
Gongo la Mboto DSM
 
CHUMBAGENI

Mwalimu Hemedi makini, elimu yake si haba
Maadili yenye fani, yenye ubora kabakaba
Sindano rudi nyumbani, uje upate mahaba
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Chuda mji wangu, vidudu nimesoma
Ngamiani ni kwangu, malaria nimepima
Maumau timu yangu, Yuda niliwatema
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Chumbageni karibu, nipitie Sembuyagi
Usije kuyaharibu, kwa kunywa konyagi
Yatakuwa maajabu, ukionja lagilagi
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia


Ukifika kwa Kipevu, muulize Mwanaidi
Usilete uerevu, na kujitia mkaidi
Kuwa mvumilivu, komamanga ufaidi
Chumbageni karibia, ule raha za kuridhia

Chama
Gongo la Mboto DSM


CHUMBAGENI NITAFIKA


kwa dua nina anzia, natamkia shahada
Yarabi twatarajia, kwako mwingi msaada
Tukinge na yadunia, tujaalie ziada
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

Mwalimu Ali Hemedi, ni wengi katufundisha
Alikuwa maridadi, hajui kutatanisha
Kwa lugha nae stadi, kiingereza alitisha
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

kikumbuka ya zamani, Jumuiya tulitisha
Popa na usagarani, uliza hawatabisha
Mpaka boza pangani, kote tulisababisha
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

Kutajia mau mau, wanikumbusha bomboka
Nani wa leo wadau, wazama tulisha ondoka
Na mengi nimesahau, ni mbali tulipotoka
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

Nasema sio uongo, nitakuja chumbageni
Nafanya sasa mipango, iwe wa sita mwanzoni
Na mpe salamu Longo, swahiba huyu mtani
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

Na chuda nakualika, nyumbani nikirudia
Ni ngali na heka heka, riziki natafutia
siwezi tena bweteka, uzee meshaingia
Chumbageni nitafika, nyumbani nikirudia

Sindano Mwana wa Ganzi (SMG)
 
Kumbe jukwaa la lugha lina matusi hivi!
Mambo ya kuchimbana mitaro kumbe hayakuanza juzi!! 👇

**Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena**
 
Kumbe jukwaa la lugha lina matusi hivi!
Mambo ya kuchimbana mitaro kumbe hayakuanza juzi!! 👇

**Kisima liharibiwa, waovu watu wabaya
Tope walivyochimbuwa, kweli walikosa haya
Umbole kahujumiwa, 'saizi' sasa yapwaya
Kisima nimekiacha, maji hayanyweki tena**


Waungwana hatutusi:

Waungwana hatutisi, sikia Jitu Bandia
Twaongea kwa wepesi, na pia twaitikia
Na maneno ni vipisi, kichwani humalizia
Sikia Jitu Bandia, waungwana hatutussi!

Haja yake ni kisima, kwa kina kaelezea
Matusi hajayasema, wakati aelezea
Usongo wake kisima, malenga kaongelea
Wengine nakumbushia, waungwana hatutusi!

Ya tatu hapa tamati, kikomo nakomelea
Naijulisha kamati, matusi sijazowea
Ujuwe hawanipati, kutusi wakianzia
Sikia Jitu Bandia, waungwana hatutusi!

Choveki
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom