Shairi: "Kafata Nini Nchini?"

Choveki

JF-Expert Member
Apr 16, 2006
458
170


"Kafata Nini Nchini?"




Nawauliza wajuzi, myajuayo ya ndani
Alipofika majuzi, akenda hadi chumbani
Kama vile paka jizi, akivizia machoni
Kafata nini nchini, kichaka huyo mwajua?

Nawauliza magamba, kichaka kafata nini?
Kafika huku atamba, akipepesa machoni
Kakenua kama mamba, udenda u mdomoni
Kafata nini nchini, semeni niwe sambamba

Ama magwanda mwajua?, kilomleta nchini
Kafika mwachekelea, na ninyi mpo sirini?
Magwanda mwachemshia, ama mwajua kunani?
Kafata nini nchini, magwanda naulizia

Si bure miye nahisi, kufika kwake nchini
Avizia kama fisi, mzoga u kigamboni?
Nasaka mwenye nyepesi, atoe hayo ya ndani
Kafata nini nchini, tujulisheni na sisi

Kaditama wa tamati, kalamu naweka chini
Wengine wasema ati, dili la kweli madini!
Alishawapa visheti, ati sasa taabani
Kafata nini nchini, tetesi nyingi baruti!

Choveki


 
sio 'KAFATA'
Kafuata. Ok makali?

"Inakubalika"

Kitunzi yakubaliki, nakujulisha ujuwe

Kutunga siyo mikiki, kupanga ndiyo kwenyewe

Tungo ni kama mkuki, misingi uilewe

Kwa lunga ya kishiri, nasema yakubalika


Ulizia kwa malenga, magwiji hao wenyewe

Kinaga tena ubaga, tajua bila kiwewe

Tunatunga kwa kulenga, fasihi uilewe

Kwa lugha za kishairi, nasema yakubalika


Narudi kwake kichaka, namuhisi kama mwewe

Karuka hadi kafika, nchini yeye mwenyewe

Ni chepi hicho hakika, anacho taka apewe?

Kwa lugha za kishairi, nasema yakubalika


Choveki
 
sio 'KAFATA'
Kafuata. Ok makali?

lugha ya ushairi haina ubaya na uharibifu wa mofolojia za maneno.
Pengine hata muundo wa sentensi unaweza kuvurugwa ili kufikia kusudi la msanii.
Sawasawa?
 
Back
Top Bottom