Entrepreneur
JF-Expert Member
- Jun 26, 2011
- 1,087
- 620
Wakuu kunajambo ambalo watu wengi hawajaliona,watu hapa naona wanazungumzia mambo ya kuchukua elfu tano na kupata na kuendelea mpaka unakua tajiri ambayo ni ndoto.Sasa basi nyie mnaotupigia mahesabu jinsi elfu tano ilivyoongezeka mpaka ikafikia mamilioni suala la hasara kwenye hiyo biashara halipo?wewe hiyo joice yako umeichukua ukaipeleka standi kuuza bwana afya akajanmgambo wa jiji akaichukua katika zoezi la kuzibiti kipindupindu.Manake naona kila mtu anazungumzia kupata tuuu biashara haiko hivyo wakuu ukiona faida kuna hasara pia.
Kitu kingine nilichoona watu wengi hapa kwenye vichwa vyao biashara wanayofikiria ni umachinga tuu,hamuwezi kuwa na mawazo mapana zaidi mkaachana na biashara ya umachinga mkafikiria biashara nyingine kama kilimo n.k.
Panueni mawazo wakuu msifikirie umachinga tuu ndio utawatoa.
Lakini hata kilimo kinategemea usindikaji pia. Hao wasindika matunda (kama NDYOKO) ni important stakeholder in the value chain