Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
KATIKA hali isiyo ya kawaida Mtendaji wa Kata ya Nondwa katika Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma,amemtunishia msuli Mkuu wa Wilaya hiyo, Betty Mkwasa. Hali ilitokea baada ya Mkwasa kuhoji ni kwa nini kata hiyo ya Nondwa haijachangia ujenzi wa shule ya sekondari na kusababisha watoto waliofaulu katika kata hiyo kupelekwa kusoma kata nyingine.
Mtendaji huyo, Yoram Ndahani baada ya kuhojiwa aliinuka na kujibu kwamba yuko tayari kuchukuliwa hatua yoyote kwani hakuwa na maelekezo ya michango ya namna hiyo. Hali hiyo ilifanya Mkuu wa Wilaya kuinuka na kumhoji kiongozi kwa nini anajibu jeuri kwani alikuwa na haki ya kuulizwa juu ya utendaji wake.
"Usipende kudharau wanawake, sizungumzi kama mwanamke nazumgumza kama kiongozi tena ni Mkuu wa Wilaya, lakini najua angekuja Mkurugenzi hapa usingemjibu hivi kwa vile anakulipa mshahara, alisema Mkwasa na kuongeza: Utambue kuwa hata huyo Mkurugenzi anaripoti kwangu na angekuwa kiongozi mwingine hapa wewe usingebaki hapa angeenda kukutupa mahabusu ujifunze namna ya kuzungumza na kumjibu kiongozi wako" .
Kutokana na hali hiyo, Ofisa Tarafa wa Kata ya Mpalanga Michael Mkunya aliomba radhi kutokana na kauli hiyo huku viongozi wa kata waliokuwepo hapo wakiomba radhi kutokana na kitendo hicho ambacho walikiita kisichopendeza.
"Kazi ya kiongozi ni kuelekeza, suala la msimamo linatupa shida kidogo kama ni suala la msimamo wa kisiasa ijulikane wakati mwingine anapofika kiongozi mkuu kubali kuelekezwa na
si kubishana," alisema Katibu Tarafa.
Mtendaji huyo, Yoram Ndahani baada ya kuhojiwa aliinuka na kujibu kwamba yuko tayari kuchukuliwa hatua yoyote kwani hakuwa na maelekezo ya michango ya namna hiyo. Hali hiyo ilifanya Mkuu wa Wilaya kuinuka na kumhoji kiongozi kwa nini anajibu jeuri kwani alikuwa na haki ya kuulizwa juu ya utendaji wake.
"Usipende kudharau wanawake, sizungumzi kama mwanamke nazumgumza kama kiongozi tena ni Mkuu wa Wilaya, lakini najua angekuja Mkurugenzi hapa usingemjibu hivi kwa vile anakulipa mshahara, alisema Mkwasa na kuongeza: Utambue kuwa hata huyo Mkurugenzi anaripoti kwangu na angekuwa kiongozi mwingine hapa wewe usingebaki hapa angeenda kukutupa mahabusu ujifunze namna ya kuzungumza na kumjibu kiongozi wako" .
Kutokana na hali hiyo, Ofisa Tarafa wa Kata ya Mpalanga Michael Mkunya aliomba radhi kutokana na kauli hiyo huku viongozi wa kata waliokuwepo hapo wakiomba radhi kutokana na kitendo hicho ambacho walikiita kisichopendeza.
"Kazi ya kiongozi ni kuelekeza, suala la msimamo linatupa shida kidogo kama ni suala la msimamo wa kisiasa ijulikane wakati mwingine anapofika kiongozi mkuu kubali kuelekezwa na
si kubishana," alisema Katibu Tarafa.