BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Serikali yaridhia utoaji mimba
* PRO-LIFE yapinga, yamwandikia Kikwete
na Joseph Sabinus
Tanzania Daima~Sauti ya watu
SERIKALI imetia saini kuridhia itifaki za haki za wanawake, ikiwemo ya kuruhusu utoaji mimba nchini.
Tanzania imeridhia mkataba huo, huku madhehebu mbalimbali ya dini yakipiga marufuku utoaji mimba, kwani ni kinyume cha mafundisho ya dini.
Itifaki hiyo ambayo inasubiri kutungiwa sheria bungeni ili ianze kutekelezwa, imo katika Mkataba wa Haki za Binadamu na Haki za Wanawake barani Afrika na Itifaki ya Maputo.
Itifaki ya Maputo inazipa wajibu nchi wanachama kuhakikisha kuwa, zinalinda na kuboresha afya za wanawake, hususan afya ya uzazi.
Itifaki hiyo kwa mujibu wa uchunguzi, inaainisha haki mbalimbali za mwanamke, ikiwa pamoja na haki ya kuamua kuzaa au kutozaa, haki ya kuamua kupata watoto na nafasi ya mtoto mmoja hadi mwingine, pamoja na haki ya kuchagua njia ya uzazi wa mpango, ikiwemo kutoa mimba.
Waziri wa Nchi, Sera, Uratibu na Bunge, Philip Marmo, alithibitisha kuridhia kwa itifaki hiyo katika barua yake yenye Kumb. Na. I/CFC.188/444/01 ya Januari 30 mwaka huu, kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kutetea Uhai (PRO-LIFE), Tanzania, Emil Hagamu, aliyeiandikia barua serikali kuhoji uhalali wa Tanzania kuridhia itifaki hiyo.
Katika barua hiyo, Hagamu alimwomba Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuingilia kati na kuzuia haraka mauaji ya watoto yanayoweza kutokea endapo Bunge litapitisha sheria ya utoaji mimba.
Akifafanua kuhusu kuridhia kwa itifaki hiyo, Waziri Marmo katika barua yake ya majibu kwa PRO-LIFE ambayo Tanzania Daima ina nakala yake, alisema Itifaki ya Haki za watu na Haki za Wanawake Barani Afrika, Ibara ya 14, kipengele cha (2) C, kinasema:
"Kwa kuangalia maudhui ya vipengele hivi kwa ujumla ni kweli inatoa tafsiri sahihi ya kuridhia utoaji mimba ili kukidhi vigezo kama inavyojieleza, ambavyo ni kwa mimba iliyosababishwa na shambulio la aibu kama vile kubakwa au kwa mimba inayohatarisha afya ya mwili na akili ya mama au uhai wa mtoto."
Akirejea barua ya PRO-LIFE, Tanzania yenye kumbukumbu namba PLT/C-A/2009 ya Januari 5, mwaka huu, Waziri Marmo alikiri kuwa kweli Tanzania imeridhia itifaki hizo, lakini bado hazijatungiwa sheria.
"Ni kweli Tanzania iliziwekea sahihi na kuridhia itifaki za Haki za Wanawake katika Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Haki za Wanawake barani Afrika na Itifaki ya Maputo," alisema.
Waziri Marmo katika barua hiyo kwa Mkurugenzi wa PRO-LIFE, ambaye pia ni Mratibu wa Human Life International (HLI) Kanda ya Tanzania, alisema japo Tanzania imeridhia itifaki hizo mbili, bado hakuna sheria iliyotungwa kusimamia au kuruhusu utoaji mimba.
"Taratibu nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingine ni kwamba, itifaki na mikataba ya kimataifa, haiwezi kuwa sheria ya nchi hadi zitakapotungiwa sheria za Bunge.
"Isitoshe, lugha zinazotumika katika itifaki mbalimbali zinakuwa za jumla sana na tafsiri yake inaweza kupotoshwa kwa urahisi ikifanywa bila kufuata tafsiri ya vyombo husika vilivyopewa mamlaka ya kutoa tafsiri ya maana ya miandiko katika sheria ambayo hapa kwetu ni Mahakama," inasema sehemu ya barua hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Waziri Marmo alifafanua kuwa Tanzania imeridhia itifaki hiyo kama ilivyo kwa nchi nyingine.
Hata hivyo alisema mchakato wa kutungia sheria bado unafanyiwa kazi ili kujua kama sheria hiyo ni muhimu kwa sasa nchini.
"Kuridhia ni suala jingine, lakini tujiulize tuna mahitaji hayo kwa sasa? Ni sawa na kuwa na msitu wa miti mingi, halafu unajiuliza, je, nahitaji kupanda miti mipya kwa sasa?
"Kwa hiyo niseme tu kwamba ni kweli serikali imeridhia kuingia na imesaini mkataba huo, lakini mchakato wa kupitisha sheria bado unafanyiwa kazi," alisema Waziri Marmo.
Akizungumza na Tanzania Daima baada ya kupata barua ya ufafanuzi kutoka kwa Waziri Marmo, Hagamu alisema PRO-LIFE, Tanzania iliwaomba Waziri Mkuu na Spika wa Bunge, kumshauri Rais na wabunge kuwa makini ili wasiruhusu kupitishwa kwa sheria hiyo inayolenga kutekeleza maamuzi ya Itifaki ya Maputo (Maputo Protocol) yaliyopitishwa miaka miwili iliyopita.
Akifurahia tamko hilo la serikali kuhusu kutoruhusu au kutunga sheria ya kuhalalisha utoaji mimba, Hagamu alisema utekelezaji wa Makubaliano ya Maputo yanayozilazimisha nchi zilizosaini kuridhia kuwapo kwa sheria hiyo, kunamaanisha kuruhusu umwagaji damu kwa kuwafanyia mauaji watoto ambao hawajazaliwa.
Alisema endapo sheria hiyo itapitishwa, Watanzania wajiandae kushuhudia watoto ambao ni taifa la kesho, wakiangamizwa bila sababu za msingi huku wanawake wakiteseka kutokana na madhara ya utoaji mimba.
"Utoaji mimba haujawahi kuleta manufaa yoyote katika nchi zilizowahi kupitisha sheria hiyo... Inabidi serikali na viongozi wote watambue wajibu mkubwa walio nao katika kulinda maisha ya watu wao tangu wakiwa tumboni, wakizaliwa, wakiwa vijana na hata wanapozeeka," alisema Hagamu.
"Kwa kuwa haki ya mwanamke haipatikani kwa kumuua mtoto wake aliye tumboni, bali kwa kulinda hadhi yake ya umama, tunaitaka serikali kuachana kabisa na wazo la kutaka kuleta sheria hii ya mauaji kwa watu wasio na hatia wala uwezo wa kujitetea," alisema Hagamu.
Tanzania ilisaini itifaki hiyo Novemba 5, 2003; Bunge likaridhia Machi 3, 2007 na rais kutia saini Mei 7, mwaka huohuo.
Kati ya nchi 53 za Umoja wa Afrika, nchi 45 zimesaini itifaki hiyo na 25 tayari zimeridhia kupitia mabunge na Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo 25.
* PRO-LIFE yapinga, yamwandikia Kikwete
na Joseph Sabinus
Tanzania Daima~Sauti ya watu
SERIKALI imetia saini kuridhia itifaki za haki za wanawake, ikiwemo ya kuruhusu utoaji mimba nchini.
Tanzania imeridhia mkataba huo, huku madhehebu mbalimbali ya dini yakipiga marufuku utoaji mimba, kwani ni kinyume cha mafundisho ya dini.
Itifaki hiyo ambayo inasubiri kutungiwa sheria bungeni ili ianze kutekelezwa, imo katika Mkataba wa Haki za Binadamu na Haki za Wanawake barani Afrika na Itifaki ya Maputo.
Itifaki ya Maputo inazipa wajibu nchi wanachama kuhakikisha kuwa, zinalinda na kuboresha afya za wanawake, hususan afya ya uzazi.
Itifaki hiyo kwa mujibu wa uchunguzi, inaainisha haki mbalimbali za mwanamke, ikiwa pamoja na haki ya kuamua kuzaa au kutozaa, haki ya kuamua kupata watoto na nafasi ya mtoto mmoja hadi mwingine, pamoja na haki ya kuchagua njia ya uzazi wa mpango, ikiwemo kutoa mimba.
Waziri wa Nchi, Sera, Uratibu na Bunge, Philip Marmo, alithibitisha kuridhia kwa itifaki hiyo katika barua yake yenye Kumb. Na. I/CFC.188/444/01 ya Januari 30 mwaka huu, kwenda kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Kutetea Uhai (PRO-LIFE), Tanzania, Emil Hagamu, aliyeiandikia barua serikali kuhoji uhalali wa Tanzania kuridhia itifaki hiyo.
Katika barua hiyo, Hagamu alimwomba Rais Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuingilia kati na kuzuia haraka mauaji ya watoto yanayoweza kutokea endapo Bunge litapitisha sheria ya utoaji mimba.
Akifafanua kuhusu kuridhia kwa itifaki hiyo, Waziri Marmo katika barua yake ya majibu kwa PRO-LIFE ambayo Tanzania Daima ina nakala yake, alisema Itifaki ya Haki za watu na Haki za Wanawake Barani Afrika, Ibara ya 14, kipengele cha (2) C, kinasema:
"Kwa kuangalia maudhui ya vipengele hivi kwa ujumla ni kweli inatoa tafsiri sahihi ya kuridhia utoaji mimba ili kukidhi vigezo kama inavyojieleza, ambavyo ni kwa mimba iliyosababishwa na shambulio la aibu kama vile kubakwa au kwa mimba inayohatarisha afya ya mwili na akili ya mama au uhai wa mtoto."
Akirejea barua ya PRO-LIFE, Tanzania yenye kumbukumbu namba PLT/C-A/2009 ya Januari 5, mwaka huu, Waziri Marmo alikiri kuwa kweli Tanzania imeridhia itifaki hizo, lakini bado hazijatungiwa sheria.
"Ni kweli Tanzania iliziwekea sahihi na kuridhia itifaki za Haki za Wanawake katika Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Haki za Wanawake barani Afrika na Itifaki ya Maputo," alisema.
Waziri Marmo katika barua hiyo kwa Mkurugenzi wa PRO-LIFE, ambaye pia ni Mratibu wa Human Life International (HLI) Kanda ya Tanzania, alisema japo Tanzania imeridhia itifaki hizo mbili, bado hakuna sheria iliyotungwa kusimamia au kuruhusu utoaji mimba.
"Taratibu nchini Tanzania kama ilivyo kwa nchi nyingine ni kwamba, itifaki na mikataba ya kimataifa, haiwezi kuwa sheria ya nchi hadi zitakapotungiwa sheria za Bunge.
"Isitoshe, lugha zinazotumika katika itifaki mbalimbali zinakuwa za jumla sana na tafsiri yake inaweza kupotoshwa kwa urahisi ikifanywa bila kufuata tafsiri ya vyombo husika vilivyopewa mamlaka ya kutoa tafsiri ya maana ya miandiko katika sheria ambayo hapa kwetu ni Mahakama," inasema sehemu ya barua hiyo.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Waziri Marmo alifafanua kuwa Tanzania imeridhia itifaki hiyo kama ilivyo kwa nchi nyingine.
Hata hivyo alisema mchakato wa kutungia sheria bado unafanyiwa kazi ili kujua kama sheria hiyo ni muhimu kwa sasa nchini.
"Kuridhia ni suala jingine, lakini tujiulize tuna mahitaji hayo kwa sasa? Ni sawa na kuwa na msitu wa miti mingi, halafu unajiuliza, je, nahitaji kupanda miti mipya kwa sasa?
"Kwa hiyo niseme tu kwamba ni kweli serikali imeridhia kuingia na imesaini mkataba huo, lakini mchakato wa kupitisha sheria bado unafanyiwa kazi," alisema Waziri Marmo.
Akizungumza na Tanzania Daima baada ya kupata barua ya ufafanuzi kutoka kwa Waziri Marmo, Hagamu alisema PRO-LIFE, Tanzania iliwaomba Waziri Mkuu na Spika wa Bunge, kumshauri Rais na wabunge kuwa makini ili wasiruhusu kupitishwa kwa sheria hiyo inayolenga kutekeleza maamuzi ya Itifaki ya Maputo (Maputo Protocol) yaliyopitishwa miaka miwili iliyopita.
Akifurahia tamko hilo la serikali kuhusu kutoruhusu au kutunga sheria ya kuhalalisha utoaji mimba, Hagamu alisema utekelezaji wa Makubaliano ya Maputo yanayozilazimisha nchi zilizosaini kuridhia kuwapo kwa sheria hiyo, kunamaanisha kuruhusu umwagaji damu kwa kuwafanyia mauaji watoto ambao hawajazaliwa.
Alisema endapo sheria hiyo itapitishwa, Watanzania wajiandae kushuhudia watoto ambao ni taifa la kesho, wakiangamizwa bila sababu za msingi huku wanawake wakiteseka kutokana na madhara ya utoaji mimba.
"Utoaji mimba haujawahi kuleta manufaa yoyote katika nchi zilizowahi kupitisha sheria hiyo... Inabidi serikali na viongozi wote watambue wajibu mkubwa walio nao katika kulinda maisha ya watu wao tangu wakiwa tumboni, wakizaliwa, wakiwa vijana na hata wanapozeeka," alisema Hagamu.
"Kwa kuwa haki ya mwanamke haipatikani kwa kumuua mtoto wake aliye tumboni, bali kwa kulinda hadhi yake ya umama, tunaitaka serikali kuachana kabisa na wazo la kutaka kuleta sheria hii ya mauaji kwa watu wasio na hatia wala uwezo wa kujitetea," alisema Hagamu.
Tanzania ilisaini itifaki hiyo Novemba 5, 2003; Bunge likaridhia Machi 3, 2007 na rais kutia saini Mei 7, mwaka huohuo.
Kati ya nchi 53 za Umoja wa Afrika, nchi 45 zimesaini itifaki hiyo na 25 tayari zimeridhia kupitia mabunge na Tanzania ni miongoni mwa nchi hizo 25.
Last edited: