Serikali yapigana kujisafisha tuhuma za ufisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Haiwezekani kupambana na mafisadi kwa maneno tu wakati huo huo bado mmewakumbatia mafisadi waliojivika ngozi ya uongozi

Posted Date::10/30/2007
Serikali yapigana kujisafisha tuhuma za ufisadi
* Zaendelea kutawala kikao chao na wafadhili
* Maamuzi ya mdajala huo kutolewa Ijumaa

Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

HUKU sakata la tuhuma za ufisadi likizidi kutawala mazungumzo yanayoendelea kati ya serikali na nchi 14 wahisani, serikali imejikuta kuwa katika wakati mgumu ya kufafanua kuhusu uchunguzi wa tuhuma hizo, kufuatia wahisani hao kuendelea kuhoji.

Taarifa zilizofikia gazeti hili jana kutoka ndani ya mkutano huo ulioanza juzi zinaeleza pamoja na mambo mengine, tuhuma hizo za ufisadi ambazo zimetolewa na wapinzani bado zimetawala mazungumzo hayo huku serikali ikijipanga vema kuzifafanua.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, kazi kubwa ya serikali pamoja na kueleza mafanikio ya bajeti, imekuwa ikifanya kazi ya kufafanua tuhuma hizo.

Sakata hilo la tuhuma za ufisadi ambalo liliibuliwa katika siku ya kwanza ya mkutano huo ulioanza juzi, ziliendelea kuwa ajenda nzito hadi jana.

Balozi wa Uingereza nchini Philip Perham, ambaye ni Mwenyekiti wa nch14 wahisani, aliibua upya sakata hilo siku ya kwanza ya mkutano huo, wakati wa kujadili taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Serikali ya mwaka 2006/07.

Hata hivyo, akizungumza na gazeti hili jana, Waziri wa Fedha, Zakia Meghji alisema serikali haijapuuza tuhuma hizo na kwamba siku zote imekuwa ikizichunguza.

"Tuhuma zinazotolewa siyo kwamba hazifanyiwi kazi, tunazifanyia kazi na ndiyo maana tumeanza uchunguzi hata kuhusu EPA -(Akaunti ya Madeni ya Nje),"alisema Meghji.

Meghji alisema serikali pia imewaeleza wahisani hao kwamba hatua nyingine ambazo serikali imechukua ni pamoja na kuangalia kwa karibu mzunguuko wa fedha chafu nchini.

Alisema katika kufanikisha hilo, serikali kupitia kitengo chake maalumu cha Kuangalia Mzunguuko wa Fedha nchini (Financial Inteliigency Unit), imekuwa ikichunguza fedha zilizopatikana kwa njia chafu.

"Tumewaeleza kuwa tuna kitengo chetu cha Financial Intelligency Unit, amabcho kazi yake kubwa ni kuangalia mzunguuko wa fedha chafu, ikiwemo zilizopatikana kinyume cha sheria," alifafanua Meghji.

Waziri Meghji alisema tuhuma hizo mpya kuhusu Sh 10 bilioni zinazoelezwa kuchotwa kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kwenda Chama cha Mapinduzi (CCM) wakati wa Uchaguzi mkuu wa 2005, zote zinahusu uchunguzi katika EPA.

"Utakuta mambo mengine yapo yote, yanahusu EPA na serikali inafanya uchunguzi, hakuna kiti kipya zaidi," alisisitiza Meghji.

Alisema serikali iko makini na imekuwa ikifuatilia na kuzifanyia kazi tuhuma zote hatua kwa hatua.

Meghji aliongeza kwamba majumuisho ya mkutano huo wa ndani unaondelea yatatolewa Ijumaa wiki hii.

Kuhusu uhusiano kati ya serikali na nchi hizo alisema:, " Mbona hakuna tatizo, mazungumzo yanaendelea vizuri, Ijumaa majumuisho yatatolewa, hakuna tatizo kabisa".

Hii si kauli ya kwanza kutolewa na nchi wahisani kuishinikiza serikali, kwani tayari kauli kama hiyo walikwisha itoa siku za nyuma. Baada ya kutoa msimamo huo, Waziri wa Mambo ya Nje, Benard Membe aliwataka kutulia ili vyombo vya dola viweze kuchunguza tuhuma za ufisadi BoT.
 
He he he kizungumkuti,CCM mwisho,inapiga tarehe tu mtachoka wenyewe kufuatilia lazima mbwage manyanga.
 
He he he kizungumkuti,CCM mwisho,inapiga tarehe tu mtachoka wenyewe kufuatilia lazima mbwage manyanga.

Tubwage manyanga ili tuwaachie mafisadi waendelee kuivuruga Tanzania kwa kujilimbikizia mali, kusaini mikataba mibovu, kula rushwa n.k. Inaonyesha jinsi usivyo na mapenzi ya kweli kwa nchi yako, vinginevyo usingetoa kauli hiyo ya kihayawani.
 
Mwiba,
Are you serious? kipi kimekuchekesha zaidi? majibu ya jumla jumla ya Zakia?

Kuna mahali kwenye bible kunaeleza aina ya watu wa aina yako na hao mafisadi. kwamba People will love nothing but money and themselves, kwamba watakuwa arrogant, boastful na abusive with no respect and no pity to others.

CCM must cleanse from all dirty games then will fit for any honourable purpose otherwise the death is beeping her.
 
Tusubiri kusikia hayo yaliyoitwa "majumuisho" hiyo Ijumaa.

Kama kweli uchunguzi unafanyika, sijui unafanyikaje wakati watuhumiwa wanaendelea na nyadhifa zao, si wangejiuzulu au wangeondolewa kwanza, otherwise huo uchunguzi hautakuwa huru kabisa ndio longolongo zilezile...
 
Mwiba,
Acha umbumbumbu wewe, nchi yako inamalizwa wewe unafanya mzaha, yaani watu wengine bwana, unaona ufahari kuwa fisadi-wannabe eh?!
 
Huyo mwiba labda mtoto wa fisadi, kasomeshwa kifisadi na hata sasa anaishi kifisadi. What else do you expect to hear from him?
 
Imetolewa mara ya mwisho: 01.11.2007 0111 EAT
•
Makamba aonya wapinzani

Habari Zinazoshabihiana
• Mbowe: Makamba hawezi kuua Upinzani 04.01.2007 [Soma]
• Makamba aonya vigogo 'wasitafune' milioni 400/- 29.03.2006 [Soma]
• Makamba awa shubiri CCM 08.07.2006 [Soma]

*Awaambia ukiwa na nyumba ya vioo usitupe mawe
*Ajibu tuhuma za ufisadi za CCM kuhusishwa na Kampuni
*Asema CCM ikiamua kujibu upinzani utakwisha

Na John Daniel, Dodoma

KATIBU Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Bw. Yussuf Makamba, amejibu tuhuma zilizotolewa na vyama vya upinzani dhidi ya chama chake kwamba kina uhusiano na kampuni ya Deep Green Finance, na kueleza kuwa tuhuma hizo hazina hata chembe ya ukweli.

Alisema jana alipozungumza na waandishi wa habari mjini hapa kuwa tuhuma hizo zilizoitwa bomu zitawalipukia wao na kuwaonya kuwa wakiendelea kuzusha maneno ya uongo na CCM ikaamua kujibu, vitakufa siku hiyo hiyo kwa maelezo kuwa wana historia ndefu ya viongozi hao na madhambi yao waliyofanya walipokuwa CCM.

"Nawaomba niwaambie viongozi wa Upinzani kupitia kwenu, kwamba kama nyumba yako ina vioo usitupe mawe, sisi (CCM) tukiamua kurudishia tutamaliza kabisa vioo vya nyumba zao, CCM haina uhusiano wowote na Kampuni ya Deep Green Finance kama wanavyodai, walidai ni bomu, lakini litawarudia na kuwalipukia wenyewe.

"Viongozi hao wa vyama vya upinzani walikuwa waandamizi serikalini, wengine tumekaa nao hapa wamekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Naibu Waziri Mkuu, wengine walikuwa makanisani, tunajua walifanya nini huko, tunajua madhambi yao makubwa ila sisi ni wastaarabu, wakiendelea tutajibu mapigo," alisema Bw. Makamba.

Alisema kukaa kwao kimya haimaanishi kwamba yeye na chama chake ni mabubu, bali ni kwa sababu tu ya kutopenda malumbano ya kisiasa na kwamba ameamua kujibu hilo kwa kuwa lilihusisha chama moja kwa moja kuwa kina uhusiano wa kibiashara na kampuni hiyo.

Alisema kutoa tuhuma alizoita za uongo, ni dalili ya wapinzani kutafuta vigezo vya kushindwa mwaka 2010 baada ya kuona kuwa CCM inasonga mbele na kwamba ina viongozi makini, wanaofaa na imejaa kila aina ya watu wenye uwezo mkubwa.
 
duh kwa kuwa ishasemwa hapo ^^ Mwiba watch out !

We wacha tu hawa ni wagagagigikoko,hawajui sababu ya mtu mzima kucheka,hivi mtu anapocheka huwa ni muwasho,kama ukurutu au upele basi sijawahi kumwona mwenye matatizo hayo kucheka na maradhi ya upele na ukurutu ,lakini tuombe uhai miezi si mingi hii hoja yao ya kuona wametushika pabaya itakufa na hakuna kitakacho kuwa,ipo wapi ya mahita ipo wapi ya zombe ipo wapi ya unga,sasa hili nalo litatoweka kama mvua za alnino.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom