Serikali yapata hasara 93bn/- barabara ya Dodoma- Manyoni

August

JF-Expert Member
Jun 18, 2007
8,393
4,056
Serikali yapata hasara 93bn/- barabara ya Dodoma- Manyoni

Na Mwandishi wetu

16th June 2009

Barabara ya Dodoma- Singida.


Serikali imepata hasara ya zaidi ya Sh. bilioni 93.4 kutokana na ujenzi wa barabara ya Dodoma-Manyoni-Singida yenye urefu wa kilometa 244 kuchelewa kukamilika.

Naibu Waziri wa Miundombinu, Ezekiah Chibulunje aliliambia Bunge jana kuwa kutokana na hasara hiyo, gharama za mradi huo sasa, zinatarajiwa kuongezeka kutoka kiasi hicho cha fedha kufikia Sh. bilioni 205.4.

Chibulunje alisema hasara nyingine iliyopatikana kutokana na kuchelewa kwa mradi huo, ni wananchi kuchelewa kupata huduma bora ya barabara mapema kama ilivyokusudiwa.

Kutokana na hali hiyo, alisema serikali iliamua kukatisha mkataba na mkandarasi aliyepewa zabuni hiyo kutokana na kuchelewesha ujenzi wa barabara hiyo.

Naibu Waziri huyo, alisema hayo wakati akijibu swali la Mbunge wa Nzega (CCM), Lucas Selelii aliyetaka kujua sababu zilifanya ujenzi wa barabara hiyo kuchelewa, hasara zilizopatikana na lini mradi huo utakamilika.

Alisema kati ya fedha zilizokadiriwa upya kugharimu ujenzi huo, Sh. bilioni 144.613 zinatarajia kutumika kujenga barabara hiyo sehemu ya Dodoma-Manyoni na Sh. bilioni 60.669 Manyoni-Singida.

Chibulunje alisema mkandarasi anayejenga sehemu ya Mhala-Manyoni yenye urefu wa kilometa 17 ni Estim Construction Company Limited, ambaye anatarajia kukamilisha sehemu hiyo ifikapo Novemba, mwaka huu na yule wa sehemu ya Manyoni-Isunna (kilometa 54); kampuni ya China Geo Corporation (CGC), atakamilisha ujenzi wa sehemu hiyo ifikapo Desemba, mwakani. Hata hivyo, alisema hadi sasa jumla ya kilometa 173 za kiwango cha lami katika barabara hiyo zimejengwa na kukamilika.



CHANZO: NIPASHE
 
je hakuna penalty kutoka kwa mjenzi kufidia hasara kwa serikali? je huyo mjenzi alichaguliwaje? na adhabu kwa wahusika ikoje?
 
Genlemen( and Ladiesof course) , read between the lines.
1 Barabara ya Dodoma-Manyoni-Singida ni miradi miwili tofauti kabisa
2 Barabara ya Manyoni Singida Mkandarasi ni Wachina na walifukuzwa zaidi ya miaka
iliyopita
3 Barabara ya Dodoma Manyoni Mkandarasi Konoike, AMEACHIA NGAZI baada ya ubababishaji mkubwa toka kwa mwenye kazi(zilisalia km 16 tu kukamilisha mradi)
4 Ni vema wananchi kuuliza kiini cha kutotekelezwa/kutokamilika mikataba hiyo ili undani ufahamike
5 Ni rahisi kuwalaumu Makandarasi lakini kuna ufisadi mkubwa uliojificha toka kwa mwenye kazi
 
Genlemen( and Ladiesof course) , read between the lines.
1 Barabara ya Dodoma-Manyoni-Singida ni miradi miwili tofauti kabisa
2 Barabara ya Manyoni Singida Mkandarasi ni Wachina na walifukuzwa zaidi ya miaka
iliyopita
3 Barabara ya Dodoma Manyoni Mkandarasi Konoike, AMEACHIA NGAZI baada ya ubababishaji mkubwa toka kwa mwenye kazi(zilisalia km 16 tu kukamilisha mradi)
4 Ni vema wananchi kuuliza kiini cha kutotekelezwa/kutokamilika mikataba hiyo ili undani ufahamike
5 Ni rahisi kuwalaumu Makandarasi lakini kuna ufisadi mkubwa uliojificha toka kwa mwenye kazi
Nashukuru kwa mchango wako, sasa ni juu wabunge kulikazania hili iweje uzumbe wa watu wetu wenyewe uingizie serikali yetu hasara, ambazo zinaweza kuepukika? Hususana wabunge wenye kuguswa na hii barabara na wale wenye kuguswa na upotevu wa pesa , maana imekuwa kama wimbo wataifa sasa .
 
Bw. Mramba, Bw. Mgonja na Bw. Yona walishitakiwa kwa kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya sh. bilioni 13.7 (ambayo ni 15% tu ya hii hasara). Wakikaa kimya kwa hili tutawashangaa.
 
hivi kitu gani hawa viongozi wetu wanaweza kufanya? wakati ujenzi unacheleweshwa walikuwa wanafatilia? na kama walikuwa wanafatilia kwanini maamuzi hayakufanyika mapema zaidi?
 
The Contractor is supposed to cover the client with insurance (performance Bond) when awarded these projects.
If the contractor failed to deliver what happened to the insurance? Why is the Government footing the loses?

Inaelekea kuna mambo ya ufisadi yamejificha ndani yake na serikali inataka kuyaficha bila kueleza wananchi ukweli.
Ni desturi ya serikali (TANRoads) ku-award construction contracts kwa makandarasi walio-bid kwa bei ya chini na ambao hawana uwezo wa kukamilsha projects as long as wanapata 10% yao. Inapofikia mahali wameshindwa ku-deliver wanakuwa terminated na kutafuta mkandarasi mwingine. this trend have been thehe all the time and construction costs normally doubles.

Kwa nini hawa wanaofanya uzembe huu hawaadhibiwi? (10% goes on the way to the higher level)
 
Back
Top Bottom