Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,593
- 29,711
na Sauli Giliard
SERIKALI imewaonya wanaotumia vibaya teknolojia ya mawasiliano ya habari (TEKNOHAMA) kwa kuwakashifu wengine na kuwadhalilisha viongozi.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla mara baada ya kuzindua Wiki ya Teknolojia, Mawasiliano na Habari Duniani, ambayo hapa nchini, imeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kwa kushirikiana na wadau wengine.
Katika maadhimisho hayo yanayoongozwa na kaulimbiu ya Mkinge Mtoto na Teknolojia ya Habari, waziri huyo alisema sheria mbalimbali za kuwalinda watu wasipate madhara yanayotokana na matumizi mabaya ya TEKNOHAMA zinaandaliwa.
Watu wanatumia vibaya teknolojia hiyo. Watu wanawadhalilisha wenzao na hata viongozi, haya si matumizi mazuri. Mtu anafanya hivyo akiwa hapa nchini au hata Marekani, lakini kwa vile hawaonekani, tunasema sasa tutawapata, alisema.
Aliongeza kuwa, matumizi mabaya ya teknolojia hiyo, ikiwamo simu za mikononi, zimewaletea watu madhara makubwa kwa baadhi ya watu na hata kusababisha vifo.
Matumizi mabaya ya simu yanaathiri watu. Hivi karibuni msichana mmoja maeneo ya Muhimbili, alijiua baada ya kutumiwa ujumbe uliomchanganya. Haya si matumizi mazuri ya simu, alisisitiza.
Aliongeza kuwa, pamoja na sheria ya kudhibiti matumizi ya mawasiliano kuandaliwa, serikali imeshaanza mchakato mwingine za kuzuia simu zinazotumia mfumo binafsi (private), na hadi kufikia Julai mwaka huu, itakuwa imekwishaandaa utaratibu wa kusajili watumiaji wa huduma ya simu za mkononi.
Waziri Msolla aliwataka wadau wa huduma za mawasiliano nchini, kupunguza gharama za huduma ya mawasiliano ili Watanzania nao waweze kunufaika na matumizi ya TEKNOHAMA.
Akielelezea hatua ambazo serikali inazichukua kwa lengo la kuiwezesha nchi kuunganishwa, ikiwamo na mikoa na wilaya pamoja na nchi jirani, alisema kwa sasa serikali ipo katika mchakato wa kujenga mkonga wa mawasiliano wenye urefu wa kilomita 10,000, utakaochukua miaka miwili kukamilika, lakini utasaidia teknolojia ya mawasiliano kusambaa na kutumiwa na wengi.
Katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA, Jaji mstaafu Buxton Chipeta alisema ikilinganishwa na kipindi cha muongo mmoja uliopita, kumekuwapo mabadiliko makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano na kufanya wadau kukaa na kutafakari juu ya mabadiliko ya tabia kwa jamii.
Takwimu za TCRA zinaonyesha kuwa, kwa sasa kuna watumiaji wa huduma za simu za mkononi milioni 13 na kumekuwapo na ongezeko kubwa la vituo vya redio na televisheni.
Maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Maua Daftari na wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi kutoka Jiji la Dar es Salaam, yanatarajiwa kuendelea leo kwa kutembelea shule, kuona matumizi hayo katika nyanja ya elimu.
Source: Tanzania Daima
Nilichopata hapo: Wanajiandaa na ule kucheza wimbo wa Fella Anikulapo Kuti uitwao ZOMBI! yaani ngoma ndo imeanza kwenye lele na pamoja na kwamba wapo kweli wanaowachafua watwana wetu hawa kiukwelii lakini kama mjuavyo mtego wa panya hunasa hata mbu hivyo tujiandae kukwea karandinga sooon.
Kama mnabisha subirini baada ya miezi minne mtakubali tu!
Lakini kama jamii tujiulize
TUKATE ISHU
SERIKALI imewaonya wanaotumia vibaya teknolojia ya mawasiliano ya habari (TEKNOHAMA) kwa kuwakashifu wengine na kuwadhalilisha viongozi.
Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla mara baada ya kuzindua Wiki ya Teknolojia, Mawasiliano na Habari Duniani, ambayo hapa nchini, imeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kwa kushirikiana na wadau wengine.
Katika maadhimisho hayo yanayoongozwa na kaulimbiu ya Mkinge Mtoto na Teknolojia ya Habari, waziri huyo alisema sheria mbalimbali za kuwalinda watu wasipate madhara yanayotokana na matumizi mabaya ya TEKNOHAMA zinaandaliwa.
Watu wanatumia vibaya teknolojia hiyo. Watu wanawadhalilisha wenzao na hata viongozi, haya si matumizi mazuri. Mtu anafanya hivyo akiwa hapa nchini au hata Marekani, lakini kwa vile hawaonekani, tunasema sasa tutawapata, alisema.
Aliongeza kuwa, matumizi mabaya ya teknolojia hiyo, ikiwamo simu za mikononi, zimewaletea watu madhara makubwa kwa baadhi ya watu na hata kusababisha vifo.
Matumizi mabaya ya simu yanaathiri watu. Hivi karibuni msichana mmoja maeneo ya Muhimbili, alijiua baada ya kutumiwa ujumbe uliomchanganya. Haya si matumizi mazuri ya simu, alisisitiza.
Aliongeza kuwa, pamoja na sheria ya kudhibiti matumizi ya mawasiliano kuandaliwa, serikali imeshaanza mchakato mwingine za kuzuia simu zinazotumia mfumo binafsi (private), na hadi kufikia Julai mwaka huu, itakuwa imekwishaandaa utaratibu wa kusajili watumiaji wa huduma ya simu za mkononi.
Waziri Msolla aliwataka wadau wa huduma za mawasiliano nchini, kupunguza gharama za huduma ya mawasiliano ili Watanzania nao waweze kunufaika na matumizi ya TEKNOHAMA.
Akielelezea hatua ambazo serikali inazichukua kwa lengo la kuiwezesha nchi kuunganishwa, ikiwamo na mikoa na wilaya pamoja na nchi jirani, alisema kwa sasa serikali ipo katika mchakato wa kujenga mkonga wa mawasiliano wenye urefu wa kilomita 10,000, utakaochukua miaka miwili kukamilika, lakini utasaidia teknolojia ya mawasiliano kusambaa na kutumiwa na wengi.
Katika uzinduzi huo, Mwenyekiti wa Bodi ya TCRA, Jaji mstaafu Buxton Chipeta alisema ikilinganishwa na kipindi cha muongo mmoja uliopita, kumekuwapo mabadiliko makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano na kufanya wadau kukaa na kutafakari juu ya mabadiliko ya tabia kwa jamii.
Takwimu za TCRA zinaonyesha kuwa, kwa sasa kuna watumiaji wa huduma za simu za mkononi milioni 13 na kumekuwapo na ongezeko kubwa la vituo vya redio na televisheni.
Maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Maua Daftari na wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi kutoka Jiji la Dar es Salaam, yanatarajiwa kuendelea leo kwa kutembelea shule, kuona matumizi hayo katika nyanja ya elimu.
Source: Tanzania Daima
Nilichopata hapo: Wanajiandaa na ule kucheza wimbo wa Fella Anikulapo Kuti uitwao ZOMBI! yaani ngoma ndo imeanza kwenye lele na pamoja na kwamba wapo kweli wanaowachafua watwana wetu hawa kiukwelii lakini kama mjuavyo mtego wa panya hunasa hata mbu hivyo tujiandae kukwea karandinga sooon.
Kama mnabisha subirini baada ya miezi minne mtakubali tu!
Lakini kama jamii tujiulize
- Kwa nini viongizi wachafuliwe? je ni wasafi kihivyo?
- Tafsiri ya kuchafuliwa kiongozi ni ipi? hapa wafafanue kiwango au ishu zipi zinazogusa stake ya usafi wa kigogo? Maana isije ikawa neno fisadi kwao ni tusi zito sana. hehe
- Ni mpaka viongozi wakichafuliwa ndipo hatua huchukuliwa? mbona sisi tunachafuliwa kweupeee na hata taarifa zikitolewa kwa vyombo husika hakuna jipya.... Angalizo Magazeti ya Shigongo na wenzake yanavyotuchafua na kuichafua jamii kila kukicha.
- Lini tutapata viongozi wenye busara ambao kauli zao zitaeleweka bila maswali mengi?
TUKATE ISHU