WAKATI Bw. Kagame huko Rwanda kafunga soko la serikali kuhodhi magari yanayokula mabilioni ya fedha za umma bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa raia wa kawaida ila tu kwa wale wanaoyatumia na jamaa zao, hapa Tanzania magari ya kifahari zaidi ya 700 ndio kwanza yanapakuliwa bandarini.
Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.
Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.
Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?
Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?
Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?
Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?
Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.
Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.
Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?
Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?
Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?
Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?