Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Baada ya wabunge kuingilia kati kashfa ya mama kujifungua akiwa amesimama katika hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam, Serikali imetangaza kuchukua hatua kali kwa watu waliohusika na uzembe huo.
Akizungumza na NIPASHE Jumapili jana akiwa mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema Serikali inalaani tukio hilo, ambapo Wizara yake itawasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kuanza kazi ya uchunguzi mara moja.
Kauli hiyo ya Serikali imekuja siku chache baada ya wabunge wanawake kutoa tamko la kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya bunge, endapo Wizara husika haijachukua hatua kwa kuwafukuza kazi pamoja na kuwashtaki wauguzi waliosababisha mwanamke huyo Kuluthum Abdallah (35) kujifungua akiwa amelazimishwa kusimama.
Kwenye tukio hilo lililotokea Aprili 18, mwaka huu majira ya saa 11.30 jioni, Kuluthum alilazimishwa na mmoja wa wauguzi (Jina lake halijafahamika) kusimama hadi alipojifungua mtoto wakati alipofika kwenye hospitali hiyo kupatiwa huduma ya uzazi.
Hata hivyo, mtoto aliyezaliwa alinusurika kwa kudra za Mungu licha ya kuangukia sakafuni wakati anazaliwa na kuserereka hadi chini ya meza ya mapokezi.
Waziri Mwalimu alisema tukio hilo limemsikitisha na kwamba Serikali haitanyamaza hasa kutokana na ukiukwaji wa Sera ya mama na watoto inayoeleza ni lazima akina mama wajawazito na watoto wapewe huduma bora ili kulinda afya zao.
"Nimesikitishwa sana na jambo hili, kama Wizara yangu yenye wajibu wa kulinda sera ya watoto tunalaani na tutawasiliana na wenzetu kuchunguza kwa kina," alisema Mwalimu.
Alisema anamtuma Mkurugenzi anayehusika na masuala ya watoto kwenda kukutana na wenzake wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kufanya kazi kama timu kwa ajili ya kuangalia namna ya kumfanyia uchunguzi mtoto huyo.
Wakati Waziri huyo akitoa tamko hilo, habari kutoka Wizara ya Afya na kuthibitishwa na mume wa Kuluthum, Ahmadah Yahya zinasema timu ya watu wanne kutoka Wizara hiyo na Hospitali ya Amana imekwenda nyumbani kwao eneo la Majohe kwa ajili ya mahojiano.
Akiongea kwa njia ya simu, Yahya alikiri kupokea ugeni huo na kueleza walikwenda hapo kwa ajili ya kumuhoji mambo mbalimbali kuhusiana na tukio hilo.
Alisema waliofika nyumbani kwake ni pamoja na daktari mmoja na muuguzi kutoka wizarani, Afisa malalamiko wa hospitali ya Amana na mwanasheria.
"Ni kweli wamekuja watu kutoka wizarani hapa nyumbani kwangu, wamenihoji kuhusu tukio lile pamoja na kuchukua picha ya mwanangu," alisema.
Alisema walichoahidi kwake ni kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu pamoja na kumfanyia uchunguzi mtoto huyo japokuwa hawakutoa tarehe maalum ya kumfanyia uchunguzi.
Awali wabunge hao wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Philipa Mturano, walimtaka waziri Dk. Hussen Mwinyi, kuwachukulia hatua wauguzi waliosababisha uzembe huo pamoja na kuchunguza vyeti vya wauguzi wote nchini.
Mturano alisema tukio lililompata mwanamke mwenzao limewasikitisha wabunge wote wanawake na kwa pamoja wameamua kuungana kulifuatilia jambo hilo hadi hapo haki itakapopatikana.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI
Akizungumza na NIPASHE Jumapili jana akiwa mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Wizara ya Wanawake, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu, alisema Serikali inalaani tukio hilo, ambapo Wizara yake itawasiliana na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kuanza kazi ya uchunguzi mara moja.
Kauli hiyo ya Serikali imekuja siku chache baada ya wabunge wanawake kutoa tamko la kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya bunge, endapo Wizara husika haijachukua hatua kwa kuwafukuza kazi pamoja na kuwashtaki wauguzi waliosababisha mwanamke huyo Kuluthum Abdallah (35) kujifungua akiwa amelazimishwa kusimama.
Kwenye tukio hilo lililotokea Aprili 18, mwaka huu majira ya saa 11.30 jioni, Kuluthum alilazimishwa na mmoja wa wauguzi (Jina lake halijafahamika) kusimama hadi alipojifungua mtoto wakati alipofika kwenye hospitali hiyo kupatiwa huduma ya uzazi.
Hata hivyo, mtoto aliyezaliwa alinusurika kwa kudra za Mungu licha ya kuangukia sakafuni wakati anazaliwa na kuserereka hadi chini ya meza ya mapokezi.
Waziri Mwalimu alisema tukio hilo limemsikitisha na kwamba Serikali haitanyamaza hasa kutokana na ukiukwaji wa Sera ya mama na watoto inayoeleza ni lazima akina mama wajawazito na watoto wapewe huduma bora ili kulinda afya zao.
"Nimesikitishwa sana na jambo hili, kama Wizara yangu yenye wajibu wa kulinda sera ya watoto tunalaani na tutawasiliana na wenzetu kuchunguza kwa kina," alisema Mwalimu.
Alisema anamtuma Mkurugenzi anayehusika na masuala ya watoto kwenda kukutana na wenzake wa Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kufanya kazi kama timu kwa ajili ya kuangalia namna ya kumfanyia uchunguzi mtoto huyo.
Wakati Waziri huyo akitoa tamko hilo, habari kutoka Wizara ya Afya na kuthibitishwa na mume wa Kuluthum, Ahmadah Yahya zinasema timu ya watu wanne kutoka Wizara hiyo na Hospitali ya Amana imekwenda nyumbani kwao eneo la Majohe kwa ajili ya mahojiano.
Akiongea kwa njia ya simu, Yahya alikiri kupokea ugeni huo na kueleza walikwenda hapo kwa ajili ya kumuhoji mambo mbalimbali kuhusiana na tukio hilo.
Alisema waliofika nyumbani kwake ni pamoja na daktari mmoja na muuguzi kutoka wizarani, Afisa malalamiko wa hospitali ya Amana na mwanasheria.
"Ni kweli wamekuja watu kutoka wizarani hapa nyumbani kwangu, wamenihoji kuhusu tukio lile pamoja na kuchukua picha ya mwanangu," alisema.
Alisema walichoahidi kwake ni kulifuatilia suala hilo kwa ukaribu pamoja na kumfanyia uchunguzi mtoto huyo japokuwa hawakutoa tarehe maalum ya kumfanyia uchunguzi.
Awali wabunge hao wakiongozwa na Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Philipa Mturano, walimtaka waziri Dk. Hussen Mwinyi, kuwachukulia hatua wauguzi waliosababisha uzembe huo pamoja na kuchunguza vyeti vya wauguzi wote nchini.
Mturano alisema tukio lililompata mwanamke mwenzao limewasikitisha wabunge wote wanawake na kwa pamoja wameamua kuungana kulifuatilia jambo hilo hadi hapo haki itakapopatikana.
CHANZO: NIPASHE JUMAPILI