EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Hatimaye serikali imekubali kuilipa kampuni ya Rail India Technical and Economic Services Ltd (Rites) Sh. bilioni 30 sawa na dola za Kimarekani milioni 20. Serikali imekubali kuilipa Rites kiasi hicho cha fedha pamoja na kuwa Rites inashutumiwa kuiendesha Tanzania Railway Ltd (TRL) katika mazingira ya kutatanisha. Pamoja na kulipa kiasi hicho cha fedha kama gharama za mabehewa matano yenye umri wa miaka kama 50 hivi, serikali pia italipa gharama za usafiri kwa maafisa wote wa ngazi ya juu wa Rites ambao wamekuwa wakifanya kazi hapa nchini kwa miaka minne sasa.
Serikali imefikia uamuzi huu kutokana na majadiliano mazito juu ya kusimamisha mkataba ambapo Rites iliibuka mshindi. Kabla ya kufikia makubaliano hayo Rites iliipa serikali notisi ya siku 60 kwamba kama haitalipa dola za Kimarekani milioni 30.2 kama gharama za kukodisha mabehawa hayo, basi Rites ingevunja mkataba. Waziri kivuli wa Fedha na Mambo ya Uchumi Mh Zitto ameshauri fedha hizo zisilipwe mpaka CAG azifanye kazi na kuzitolea ripoti accounts za TRL.
Serikali imefikia uamuzi huu kutokana na majadiliano mazito juu ya kusimamisha mkataba ambapo Rites iliibuka mshindi. Kabla ya kufikia makubaliano hayo Rites iliipa serikali notisi ya siku 60 kwamba kama haitalipa dola za Kimarekani milioni 30.2 kama gharama za kukodisha mabehawa hayo, basi Rites ingevunja mkataba. Waziri kivuli wa Fedha na Mambo ya Uchumi Mh Zitto ameshauri fedha hizo zisilipwe mpaka CAG azifanye kazi na kuzitolea ripoti accounts za TRL.