Serikali yakimbilia mahakamani tena

Baba Mkubwa

JF-Expert Member
Oct 18, 2008
793
58
Na Reuben Kagaruki, Jijini

WAKATI walimu wanatarajia kuanza mgomo wao nchi nzima Jumatatu kushinikiza kulipwa fedha za malimbikizo yao, Serikali imetoa tamko zito ikisema mgomo huo ni batili huku ikikimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kuomba iuzuie.

Hatua hiyo ya serikali imetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, alipozungumza na waandishi wa habari leo asubuhi na kutoa msimamo wa Serikali kuhusiana na mgomo uliotangazwa na Chama Cha Walimu Tanzania (CWT).

Akiwa ameongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Edna Mangesho na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Hamis Dihenga, Luhanjo amesema mgomo huo ni batili kwa sababu baadhi ya vipengele havikutekelezwa.

"Katika kusudio la mgomo wa walimu baadhi ya masharti hayakutimizwa ndio maana Serikali inapinga mgomo batili usio na kikomo,"amesisitiza Luhanjo.

Ameongeza kuwa tayari Serikali imekwishawasilisha Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi maombi ya Anuai Na:21 ya mwaka 2008 kuiomba izuie mgomo usio na kikomo unaokusudiwa kuanza Jumatatu.

"CWT imepelekewa samansi ya kuitwa mahakamani kwa ajili ya shauri hilo la maombi ya Anuai ambalo limepangwa kusikilizwa Jumatatu," amesisitiza Luhanjo.

Amesema kutokana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa, Serikali imekitaka chama cha walimu kusitisha mgomo usio na kikomo. Luhanjo amesema mwalimu atakayeshiriki mgomo huo hatalipwa mshahara na serikali kwa sababu ya kushiriki mgomo batili.

Ametishia kuwa walimu watakaogoma, watalipwa mishahara yao na aliyeitisha mgomo huo. Amesema watakaogoma watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria za kazi.

"Mgomo huo hauna maslahi kwa umma na hata kwa walimu wenyewe kwa sababu unakusudiwa kufanyika katika kipindi ambacho wanafunzi wanapaswa kufanya mitihani yao ya kuvuka madarasa na vidato,"amesema.

Ameikumbusha CWT kutambua kuwa suala hilo tayari lipo mahakamani hivyo kitendo cha walimu kugoma kitakuwa sawa na kuishinikiza mahakama kwenye kesi iliyofunguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alitangaza kuwa mgomo huo usiokuwa na kikomo utaanza rasmi Jumatatu ambapo utahusisha walimu wa shule za msingi, sekondari, vyuo vya ualimu na vile vya maendeleo ya jamii ambao ndio wanachama wa CWT.

Mukoba amewataka walimu wasiogope vitisho vya Serikali kwa sababu mgomo huo ni halali. Baraza la Taifa la CWT linatarajia kukutana Januari mwakani ili kupitia utekelezaji wa madai yao.

Source: Dar leo
 
Na Reuben Kagaruki, Jijini

WAKATI walimu wanatarajia kuanza mgomo wao nchi nzima Jumatatu kushinikiza kulipwa fedha za malimbikizo yao, Serikali imetoa tamko zito ikisema mgomo huo ni batili huku ikikimbilia Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi kuomba iuzuie.

Hatua hiyo ya serikali imetangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, alipozungumza na waandishi wa habari leo asubuhi na kutoa msimamo wa Serikali kuhusiana na mgomo uliotangazwa na Chama Cha Walimu Tanzania (CWT).

Akiwa ameongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Edna Mangesho na Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Hamis Dihenga, Luhanjo amesema mgomo huo ni batili kwa sababu baadhi ya vipengele havikutekelezwa.

"Katika kusudio la mgomo wa walimu baadhi ya masharti hayakutimizwa ndio maana Serikali inapinga mgomo batili usio na kikomo,"amesisitiza Luhanjo.

Ameongeza kuwa tayari Serikali imekwishawasilisha Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi maombi ya Anuai Na:21 ya mwaka 2008 kuiomba izuie mgomo usio na kikomo unaokusudiwa kuanza Jumatatu.

"CWT imepelekewa samansi ya kuitwa mahakamani kwa ajili ya shauri hilo la maombi ya Anuai ambalo limepangwa kusikilizwa Jumatatu," amesisitiza Luhanjo.

Amesema kutokana na hatua zinazoendelea kuchukuliwa, Serikali imekitaka chama cha walimu kusitisha mgomo usio na kikomo. Luhanjo amesema mwalimu atakayeshiriki mgomo huo hatalipwa mshahara na serikali kwa sababu ya kushiriki mgomo batili.

Ametishia kuwa walimu watakaogoma, watalipwa mishahara yao na aliyeitisha mgomo huo. Amesema watakaogoma watachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria za kazi.

"Mgomo huo hauna maslahi kwa umma na hata kwa walimu wenyewe kwa sababu unakusudiwa kufanyika katika kipindi ambacho wanafunzi wanapaswa kufanya mitihani yao ya kuvuka madarasa na vidato,"amesema.

Ameikumbusha CWT kutambua kuwa suala hilo tayari lipo mahakamani hivyo kitendo cha walimu kugoma kitakuwa sawa na kuishinikiza mahakama kwenye kesi iliyofunguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa CWT, Gratian Mukoba, alitangaza kuwa mgomo huo usiokuwa na kikomo utaanza rasmi Jumatatu ambapo utahusisha walimu wa shule za msingi, sekondari, vyuo vya ualimu na vile vya maendeleo ya jamii ambao ndio wanachama wa CWT.

Mukoba amewataka walimu wasiogope vitisho vya Serikali kwa sababu mgomo huo ni halali. Baraza la Taifa la CWT linatarajia kukutana Januari mwakani ili kupitia utekelezaji wa madai yao.

Source: Dar leo

Ahsante mkuu.

Hapa nadhani kuna kitu. Kwa nini serikali inakimbilia mahakamani badala ya kuwalipa haki zao?? Nadhani walimu waendelee na mgomo. Kila kitu mbele kwa mbele. Maana najua 2010 watarudi kwao kuwaomba wasimamie uchaguzi! Kazi ipo...!
 
Hivi hii serikali ina kichaa?sasa mahakamani ndo kunaifanya ilipe haya malimbikizo ya waalimu?
 
Hii ndio kawaida ya serikali yetu,badala ya kutatua matatizo inaongeza matatizo. ' WIZI MTUPU'
 
Hii ndio kawaida ya serikali yetu,badala ya kutatua matatizo inaongeza matatizo. ' WIZI MTUPU'

Walimu wanagoma, wanafunzi nao wanagoma, madaktari wanagoma, wazee wanaandamana, wanachi wanampiga mawe raisi wao, Wafanyabiashara walio na tenda za kulisha chakula mashuleni nao wanagoma! haaaaaaa nchi hii tutafika kweli?
Kikwete tukwambie ukweli tu ingawa unauma, pamoja na kwamba ulichaguliwa na wengi hao mnaosema ni asilimia 80! naona nchi imekushinda. Jiondoe mwenyewe kutunza heshima yako, maana hata uking'an'gania watu hawakupendi tena.
 
Jamani mnaofahamu sheria tusaidiane, iliyotengua Hukumu ya Serikali Kuzuia Walimu Kugoma ni Mahakama ya Rufaa (niko tayari kusahihishwa kama nimekosea), sasa inawezekana kuna Mahakama inayoweza kutengua Uamuzi wa Mahakama ya Rufaa? Au ni Ubabe wa Serikali aka WIZI MTUPU

Ndege
 
kufuatana na taarifa iliyo tolewa leo na mrajis wa mahama ya rufaa, mahakama hiyo haikuruhusu walimu kugoma. ilichosema ni kwamba ''vifungu vya sheria mahakam kuu ilivyotumia kuzuia mgomo wa walimu havikuwa halali".

sasa kama havikuwa halali si maana yake mgomo wa wakati ule ulikuwa halali kuendelea na sasa ni kitu gani kitazuia walimu kuendelea na mgomo wao!

inavyo elekea, mahakama inatafutiwa njia ya kutafsiri hukumu yake ili mgomo wa jumatatu uwe batili. nadhani suluhisho ni kupata hukumu yenyewe 'verbatim' ili kila mtu aweze kuifsiri hukumu hiyo ya juzi.

macinkus
 
Jamani mnaofahamu sheria tusaidiane, iliyotengua Hukumu ya Serikali Kuzuia Walimu Kugoma ni Mahakama ya Rufaa (niko tayari kusahihishwa kama nimekosea), sasa inawezekana kuna Mahakama inayoweza kutengua Uamuzi wa Mahakama ya Rufaa? Au ni Ubabe wa Serikali aka WIZI MTUPU

Ndege

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tannzania, Mahakamani ndipo mahali pekee pa kupatia haki. Na Mahakama ya Rufaaa ndio chombo cha Juu kabisa katika utoaji wa haki.

Ila kama bado unahisi uamuzi wa Mahakama ya Rufaa
Haujakutendea haki, unajenga hoja tena lazima iwe na nguvu kisheria kuiomba Mahakama hiyo kupitia tena maamuzi yake. Inaitwa Court Review. Mahakama ikijiridhisha una hoja ya msingi, wanaamua kuitisha Court Review. Kama hukumu ilitolewa na Jaji mmoja, Court Review wanakaa Majaji 3. Wakiamua kama hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 5. Kama bado hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 7 wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania. Hii inaitwa Full Bench. Uamuzi wake ni Wa Mwisho yaani Final. Hapo ndiyo mwisho wa haki kwa Tanzania.

Zaidi ya hapo hakuna hata Rais hawezi kusaidia. Mwisho wa uwezo wa rais ni kuamua kusaini hati ya kutekelezwa kwa adhabu ya kifo au kutoisaini. Na kutoa misamaha kwa wafungwa.

Nikirudi kwa walimu, wao wana haki ya kugoma kwa mujibu wa sheria. Serikali pia ina haki ya kuzuia mgomo ambao ni batili.

Naungana na walimu kuwa madai yao ni ya msingi na wana haki ya kugoma. Siungi mkono mgomo kwenye kipindi hiki cha kusahihisha mitihani ya taifa.

Naiunga mkono serikali kuuzuia mgomo huu wa walimu kwa sababu kwa mujibu wa sheria, hakuna mgomo usiokuwa na ukomo.

Mwisho ombi kwa Mkoba na walimu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi Wa Umma, Mhe. Hawa
Ghasia yuko hapa New Dheli India kwa ziara muhimu kitaifa. Tafadhalini sana msije mkamtibulia ziara yake akalazimika kuikatisha wakati sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu.

Ushauri wangu ni kwenu walimu msigome. Hamuwezi kushindana na serikali. Mkoba atawaponza ila kumbukeni anayewalipa mishahara ni serikali na hata huyo Mkoba anategemea makato toka mshahara huo huo. Gomeni lakini cha moto mtakipata!.
 
Serikali yoyote duniani inayoshindwa kukaa meza moja na waajiriwa wake ili kutafuta ufumbuzi wa matatizo yoyote yaliyopo kati yake na waajiriwa wake na kukimbilia mahakamani ni serikali ambayo imeshindwa kazi yake na haistahili kuendelea kuwepo madarakani.
 
Nikirudi kwa walimu, wao wana haki ya kugoma kwa mujibu wa sheria. Serikali pia ina haki ya kuzuia mgomo ambao ni batili.

Naungana na walimu kuwa madai yao ni ya msingi na wana haki ya kugoma. Siungi mkono mgomo kwenye kipindi hiki cha kusahihisha mitihani ya taifa.

Naiunga mkono serikali kuuzuia mgomo huu wa walimu kwa sababu kwa mujibu wa sheria, hakuna mgomo usiokuwa na ukomo.

Mwisho ombi kwa Mkoba na walimu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi Wa Umma, Mhe. Hawa
Ghasia yuko hapa New Dheli India kwa ziara muhimu kitaifa. Tafadhalini sana msije mkamtibulia ziara yake akalazimika kuikatisha wakati sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu.


Ushauri wangu ni kwenu walimu msigome. Hamuwezi kushindana na serikali. Mkoba atawaponza ila kumbukeni anayewalipa mishahara ni serikali na hata huyo Mkoba anategemea makato toka mshahara huo huo. Gomeni lakini cha moto mtakipata!.

Pasco,

Umejichanganya unaunga mkono serikali,na unaunga mkono waalimu!!! Confused!! Naona umeamua kuwa msemaji wa serikali, 'sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu. Unashauri waalimu waweke silaha chini ilinyie mlio Delhi mumuulize Mh Hawa Ghasia, Pasco wa JF naulizia masuala ya waalimu? This is very low....

Wacha waalimu wagome, serikali imeshindwa walipa...wacha wagome kipindi hiki muhimu kwao, haiwezi wafukuza ni kuwatishia nyau tu.

Ushi
 
Pasco,

Umejichanganya unaunga mkono serikali,na unaunga mkono waalimu!!! Confused!! Naona umeamua kuwa msemaji wa serikali, 'sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu. Unashauri waalimu waweke silaha chini ilinyie mlio Delhi mumuulize Mh Hawa Ghasia, Pasco wa JF naulizia masuala ya waalimu? This is very low....

Wacha waalimu wagome, serikali imeshindwa walipa...wacha wagome kipindi hiki muhimu kwao, haiwezi wafukuza ni kuwatishia nyau tu.

Ushi[/QUOTE

Nimesema naunga mkono madai ya walimu ni genuine na nawaunga mkono waalimu kuitumia haki yao ya kugoma kwa kutumia mgomo halali.

Nikasema siungi mkono waalimu kugoma kipindi hiki cha
Mitihani ya taifa. Na nikasema naunga mkono serikali kuupinga mgonmo ambao hauna ukomo.

Kisheria kila mgomo lazima uwe na ukomo. Mgomo usio na ukomo, sio halali kisheria

Walimu, walimu, walimu msidanganyike mkagoma mgomo wenu sio wa halali na ile hukumu iliyouzuia bado inasimama
Japo sababu za Mahakama kuu kufikia uaamuzi wa kuuzuia ndizo zilizoelezwa kuwa na kasoro, sio hukumu!
 
Ushi[/QUOTE
Japo sababu za Mahakama kuu kufikia uaamuzi wa kuuzuia ndizo zilizoelezwa kuwa na kasoro, sio hukumu![/QUOTE]

sasa hii ndio unasema nini. kama sababu za kufikia uamuzi zina kasoro, kivipi hukumu isiwe na kasoro. nadhani ni vema mwenye hukumu yenyewe aiweke hapa.

macinkus
 
Katika nchi huru yeyote mgomo ni halali, kuna uhalali zaidi pale mgomo uwekwapo wazi katika vyombo vya habari na wahusika wakuu yaani serikali miezi mitatu kabla ya mgomo.
Walimu wana haki ya kugoma. Ninawaunga mkono.

Endapo serikali ya CCM haitatekeleza madai yao, walimu waijibu serikali ya CCM kwa vitendo November 2010.

Nijuavyo mimi wabunge wa CCM huwatumia walimu kama nguo safi ya ndani wakati wa uchaguzi, wakisha chaguliwa na kuanza kuitwa waheshiwa huwageuzia kibao walimu waliowasaidia kuingia bungeni na kuwaweka katika kundi la nguo chafu za ndani.

Walimu gomeni mna haki.

Wale wanaodhani walimu ni kondoo wasio na moyo wala hisia za maumivu nao wana haki kufanya hivyo,mtazamo wao dhidi ya walimu siyo katiba wala sheria ni maoni tu.
 
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tannzania, Mahakamani ndipo mahali pekee pa kupatia haki. Na Mahakama ya Rufaaa ndio chombo cha Juu kabisa katika utoaji wa haki.

Ila kama bado unahisi uamuzi wa Mahakama ya Rufaa
Haujakutendea haki, unajenga hoja tena lazima iwe na nguvu kisheria kuiomba Mahakama hiyo kupitia tena maamuzi yake. Inaitwa Court Review. Mahakama ikijiridhisha una hoja ya msingi, wanaamua kuitisha Court Review. Kama hukumu ilitolewa na Jaji mmoja, Court Review wanakaa Majaji 3. Wakiamua kama hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 5. Kama bado hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 7 wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania. Hii inaitwa Full Bench. Uamuzi wake ni Wa Mwisho yaani Final. Hapo ndiyo mwisho wa haki kwa Tanzania.

Zaidi ya hapo hakuna hata Rais hawezi kusaidia. Mwisho wa uwezo wa rais ni kuamua kusaini hati ya kutekelezwa kwa adhabu ya kifo au kutoisaini. Na kutoa misamaha kwa wafungwa.

Nikirudi kwa walimu, wao wana haki ya kugoma kwa mujibu wa sheria. Serikali pia ina haki ya kuzuia mgomo ambao ni batili.

Naungana na walimu kuwa madai yao ni ya msingi na wana haki ya kugoma. Siungi mkono mgomo kwenye kipindi hiki cha kusahihisha mitihani ya taifa.

Naiunga mkono serikali kuuzuia mgomo huu wa walimu kwa sababu kwa mujibu wa sheria, hakuna mgomo usiokuwa na ukomo.

Mwisho ombi kwa Mkoba na walimu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi Wa Umma, Mhe. Hawa
Ghasia yuko hapa New Dheli India kwa ziara muhimu kitaifa. Tafadhalini sana msije mkamtibulia ziara yake akalazimika kuikatisha wakati sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu.

Ushauri wangu ni kwenu walimu msigome. Hamuwezi kushindana na serikali. Mkoba atawaponza ila kumbukeni anayewalipa mishahara ni serikali na hata huyo Mkoba anategemea makato toka mshahara huo huo. Gomeni lakini cha moto mtakipata!.

Pasco are you serious?
Unadhani walimu wakigoma wao pekee ndio watapata cha moto?!
Hapa umejidanganya. Na nadhani umejidanganya kwa kuwa uko nje ya nchi.
Hapa walimu wakigoma serikali imekipata cha moto haswa.
Leo nilikuwa na mzazi mmoja anayejua matokeo ya mgomo kwa walimu kwani ana mwanae ambaye anaingia kidato cha nne. Na anao wawili ambao ni kati ya hao waliofukuzwa juzi Chuo kikuu. Huyu alikuwa mpenzi wa JK hujapata kuona. Lakini lugha niliyosikia akizungumza leo, sikuamini. Nakuaminia kuwa serikali itakipata cha moto na hakuna hata mwalimu mmoja anayeweza kufukuzwa. Nasema hili nikijua huu ndio ukweli.
Na kama inavyosema serikali kwamba haitawalipa kama wakigoma, nakuhakikishia huu mgogoro hautakwisha milele kama hawatalipwa. Na itabidi JK na kabineti yake waingie darasani kufundisha. Je, wataweza?
Basi tusubiri tuone kama mshindi hakuwa mwalimu!
 
Kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tannzania, Mahakamani ndipo mahali pekee pa kupatia haki. Na Mahakama ya Rufaaa ndio chombo cha Juu kabisa katika utoaji wa haki.

Ila kama bado unahisi uamuzi wa Mahakama ya Rufaa
Haujakutendea haki, unajenga hoja tena lazima iwe na nguvu kisheria kuiomba Mahakama hiyo kupitia tena maamuzi yake. Inaitwa Court Review. Mahakama ikijiridhisha una hoja ya msingi, wanaamua kuitisha Court Review. Kama hukumu ilitolewa na Jaji mmoja, Court Review wanakaa Majaji 3. Wakiamua kama hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 5. Kama bado hujaridhika unajenga hoja wanakaa Majaji 7 wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania. Hii inaitwa Full Bench. Uamuzi wake ni Wa Mwisho yaani Final. Hapo ndiyo mwisho wa haki kwa Tanzania.

Zaidi ya hapo hakuna hata Rais hawezi kusaidia. Mwisho wa uwezo wa rais ni kuamua kusaini hati ya kutekelezwa kwa adhabu ya kifo au kutoisaini. Na kutoa misamaha kwa wafungwa.

Nikirudi kwa walimu, wao wana haki ya kugoma kwa mujibu wa sheria. Serikali pia ina haki ya kuzuia mgomo ambao ni batili.

Naungana na walimu kuwa madai yao ni ya msingi na wana haki ya kugoma. Siungi mkono mgomo kwenye kipindi hiki cha kusahihisha mitihani ya taifa.

Naiunga mkono serikali kuuzuia mgomo huu wa walimu kwa sababu kwa mujibu wa sheria, hakuna mgomo usiokuwa na ukomo.

Mwisho ombi kwa Mkoba na walimu, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Menejimenti ya Utumishi Wa Umma, Mhe. Hawa
Ghasia yuko hapa New Dheli India kwa ziara muhimu kitaifa. Tafadhalini sana msije mkamtibulia ziara yake akalazimika kuikatisha wakati sie wengine tulioko huku ndio tunategemea kupata mwanya wa kumuona na kumpiga maswali yetu likiwemo hilo la kilio chenu.

Ushauri wangu ni kwenu walimu msigome. Hamuwezi kushindana na serikali. Mkoba atawaponza ila kumbukeni anayewalipa mishahara ni serikali na hata huyo Mkoba anategemea makato toka mshahara huo huo. Gomeni lakini cha moto mtakipata!.

Umeeleza vizuri sana. Ila hii paragraph ya mwisho...eh! Walimu wanadai haki yao, hawashindani na serikali. Ila serikali ndiyo inayoshindana na walimu ili iwashinde na haki zao zipotee. Ni aibu kubwa sana kwa serikali yetu kuona kuwa ina maneno tu bila utendaji.

Hebu fikiria hata wanaohamishwa kupisha ujenzi wa miradi ya maendeleo - ama hawalipwi na kama wakilipwa siyo kiasi ambacho kingetakiwa. Hivi ingetokea malimbikizo kama hayo kwa wabunge bado wangekuwa wanahudhuria vikao vya bunge Dodoma?

Kinachotakiwa ni serikali kurekebisha makosa yake na kujipanga upya ili mambo yaende vizuri. La sivyo nchi yetu itakuwa ya ajabu sana - rasilimali tele lakini watu masikini wa kupindukia.
 
mie naona sasa ni vizuri waziri magembe akasema ukweli maana anaonekana ni mtu mbabaishaji yeye pamoja na serikali yake maaana
huu ni totaly ujinga na naweza sema upuuuuzi kwani hatuwezi kuona migomo katika kila kada

wazeee east africa
walimu
wanafunzi wa msingi
wanafunzi wa vyuo vikuuu
wafanyakazi reli
wafanyakazi nmb

haya sasa yetu macho
hili ni bomu linalosukwa na nawahakikishieni liko karibuni kulipuka
hizi hasira zimechangiwa na mafisadi kutochokuliwa sheria huku wale wezi wa kuku na vibaka wakifia magerezani na wengine kuonja mauti kwa kupigwa na wananchi wenye hasira kali

mie nashauri kuwa kwa kuwa wezi hawa wakubwa tunawajua
tutumie nguvu kuwaondoa katika jamiiiiiii yetu kama serikali inawaogopa

nashangaa serikali inasema inaogopa kwa kuwa wanahela,hela nini juuu ya sheria na mamlaka tuliyompa raisi
 
Pasco are you serious?
Unadhani walimu wakigoma wao pekee ndio watapata cha moto?!
Hapa umejidanganya. Na nadhani umejidanganya kwa kuwa uko nje ya nchi.
Hapa walimu wakigoma serikali imekipata cha moto haswa.
Leo nilikuwa na mzazi mmoja anayejua matokeo ya mgomo kwa walimu kwani ana mwanae ambaye anaingia kidato cha nne. Na anao wawili ambao ni kati ya hao waliofukuzwa juzi Chuo kikuu. Huyu alikuwa mpenzi wa JK hujapata kuona. Lakini lugha niliyosikia akizungumza leo, sikuamini. Nakuaminia kuwa serikali itakipata cha moto na hakuna hata mwalimu mmoja anayeweza kufukuzwa. Nasema hili nikijua huu ndio ukweli.
Na kama inavyosema serikali kwamba haitawalipa kama wakigoma, nakuhakikishia huu mgogoro hautakwisha milele kama hawatalipwa. Na itabidi JK na kabineti yake waingie darasani kufundisha. Je, wataweza?
Basi tusubiri tuone kama mshindi hakuwa mwalimu!

Nakubaliana na madai ya waalimu ni genuine. Nakubaliana na haki ya kugoma ila mgomo halali. Pia nakubali walimi wakigoma uwe ni mgomo halali ama sio halali ni janga lisilopimika.

Hayo yote tisa, kumi serikali imelipa bilioni za walimu leo. Walimu wakachukue pesa zao Jumatatu.
Kesho Jumapili najua Mkoba aatatangaza tena waendelee na mgomo mpaka madai yao ylipwe yote.
Ttatizo la sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma. Kwa vile kisheria hakuna mgomo usio na ukomo. Walimu wakigoma serikali italia na serikali ikkitumia sheria walimu watalia. Who laugh last, Laugh most.
 
Nakubaliana na madai ya waalimu ni genuine. Nakubaliana na haki ya kugoma ila mgomo halali. Pia nakubali walimi wakigoma uwe ni mgomo halali ama sio halali ni janga lisilopimika.

Hayo yote tisa, kumi serikali imelipa bilioni za walimu leo. Walimu wakachukue pesa zao Jumatatu.
Kesho Jumapili najua Mkoba aatatangaza tena waendelee na mgomo mpaka madai yao ylipwe yote.
Ttatizo la sheria ni msumeno hukata mbele na nyuma. Kwa vile kisheria hakuna mgomo usio na ukomo. Walimu wakigoma serikali italia na serikali ikkitumia sheria walimu watalia. Who laugh last, Laugh most.

Walimu pekee yao wana uwezo wa kuipiga mweleka CCM na serikali yake.
Mwalinu yeyote mwenye adabu zake na maadili pale kijijini ni sawa na taa itoayo nuru usiku na mchana.
Mwalimu akitoa ushauri au akiweka neno sawa watu wengi huko kijijini huchulia neno hilo ndiyo kauri ya mwisho ya kumaliza utata.
Nadhani Serikali ya CCM ina Understimate potential power ya walimu.
Mwlimu akigoma sijui utamfuata wapi na rungu lako la FFU ukampasue kichwa.

Kuna migogoro inayosuruhishwa kwa Rungu la FFU lakini huu wa Walimu sidhani kama serikali itakuwa ya mwisho kucheka.
Serikali inaweza kuwa ya mwisho kuchekea msalani.
 
Pasco are you serious?
Unadhani walimu wakigoma wao pekee ndio watapata cha moto?!
Hapa umejidanganya. Na nadhani umejidanganya kwa kuwa uko nje ya nchi.
Hapa walimu wakigoma serikali imekipata cha moto haswa.
Leo nilikuwa na mzazi mmoja anayejua matokeo ya mgomo kwa walimu kwani ana mwanae ambaye anaingia kidato cha nne. Na anao wawili ambao ni kati ya hao waliofukuzwa juzi Chuo kikuu. Huyu alikuwa mpenzi wa JK hujapata kuona. Lakini lugha niliyosikia akizungumza leo, sikuamini. Nakuaminia kuwa serikali itakipata cha moto na hakuna hata mwalimu mmoja anayeweza kufukuzwa. Nasema hili nikijua huu ndio ukweli.
Na kama inavyosema serikali kwamba haitawalipa kama wakigoma, nakuhakikishia huu mgogoro hautakwisha milele kama hawatalipwa. Na itabidi JK na kabineti yake waingie darasani kufundisha. Je, wataweza?
Basi tusubiri tuone kama mshindi hakuwa mwalimu!

Mkuu tupo ukurasa mmoja dogo Pasco nilikuwa naheshimu sana michango yake, kwa hili amenikwaza namchukulia hapa kama ni mlevi wa fikra na amepotoka kwa hili. Huwezi kusupport serikali imenyanyasa sana walimu and the like na kwa sasa waishika pabaya tuone kama inaweza kufukuza kazi walimu wa nchi nzima.solidality kwa waaalimu ni muhimu sana kuliko kipindi chochote.

Ushi wa Rombo
 
Back
Top Bottom