Songambele
JF-Expert Member
- Nov 20, 2007
- 4,695
- 2,553
Serikali imeomba mkopo wa $ 83 karibia Tsh 98billioni kutoka serikali ya India ili kuinusuru kampuni ya TRL iliyopewa dhamana ya kundesha usafiri wa reli ya kati Tanzania bara , kampuni ambayo imekumbwa na matatizo ya kifedha baada ya kubinafsisha lililokuwa shirika la reli(TRC). (Tafsiri isiyokuwa rasmi kutoka THISDAY la Leo).
Hiki ni kielelezo tosha kwa kushindwa kwa PSRC na Serikali kuwasaidia watanzania kuondokana na matatizo waliyonayo kwa muda mrefu. Itakuwa vipi shirika liuzwe kwa kampuni ya briefcase ambayo siku chache baada ya kuuziwa shirika inakosa uwezo wa kuendesha shirika. Sitaki kuamini kwamba PSRC na Serikali walishindwa kutathmini uwezo wa kifedha wa kampuni kabla kukabidhi, kuna kila dalili ya kuonyesha kuwa watu wenye mikono michafu wamefanya vitu vyao hapa (Ufisadi).
Na inapokopa seriakali nani atalipa? kama sio sisi walipa kodi wakati Wahindi watakuwa wameshaamisha faida kwao, Pinda alikinga kifua mwanzoni mwa mwaka huu jamaa walikopeshwa na serikali zaidi ya Tsh 5bn kulipa mishahara sijui kama zimesharudishwa? leo serikali hiyo hiyo inataka kuingilia tena kukopa tena kunatofauti gani na ilipokuwa TRC. Hata kama serikali ina hisa bado haishiriki katika management ila katika kukopa wahindi wanaitaungiliza serikali huu ni ujinga lazima tuupinge kwa nguvu zote.
Wanapokuwa wawekezaji wazalendo je wanapata suport sawa na hii wanaopewa wahindi wa TRL? Haiwezekani jamaa wakute kila kitu halafu bado na pesa uwapatie wao kazi yao kuongoza siamini kama kuna watanzania wameshindwa kuongoza kama watapewa support kama ya hawa jamaa.
Ni wakati muafaka kwa serikali kukubali mashirika au kampuni zinazotaka kufa zife haraka kuliko kuziacha zichukue muda mrefu kufa wakati watanzania wataumia zaidi kama kampuni za namna hii zitakawia kufa, tazameni kesi ya Enron ilielekea kufa na ikafa haraka, jana kuna benki kubwa ya marekani imetangazwa mufilisi na hiatachukua muda utasikia mambo yamekwisha. Sasa bongo kampuni inaelekea kufa mnataka kuizuia isife kwa gharama za watanzania.
Vyovyote vile ni mtazamo wangu kutokana na habari iliyoandikwa na Thisday, wajumbe mjadala huko kwenu karibuni tunahitaji nondo za kiuchumi na biashara hapa, umbumbu wetu katika mambo haya unatugharimu.
Hiki ni kielelezo tosha kwa kushindwa kwa PSRC na Serikali kuwasaidia watanzania kuondokana na matatizo waliyonayo kwa muda mrefu. Itakuwa vipi shirika liuzwe kwa kampuni ya briefcase ambayo siku chache baada ya kuuziwa shirika inakosa uwezo wa kuendesha shirika. Sitaki kuamini kwamba PSRC na Serikali walishindwa kutathmini uwezo wa kifedha wa kampuni kabla kukabidhi, kuna kila dalili ya kuonyesha kuwa watu wenye mikono michafu wamefanya vitu vyao hapa (Ufisadi).
Na inapokopa seriakali nani atalipa? kama sio sisi walipa kodi wakati Wahindi watakuwa wameshaamisha faida kwao, Pinda alikinga kifua mwanzoni mwa mwaka huu jamaa walikopeshwa na serikali zaidi ya Tsh 5bn kulipa mishahara sijui kama zimesharudishwa? leo serikali hiyo hiyo inataka kuingilia tena kukopa tena kunatofauti gani na ilipokuwa TRC. Hata kama serikali ina hisa bado haishiriki katika management ila katika kukopa wahindi wanaitaungiliza serikali huu ni ujinga lazima tuupinge kwa nguvu zote.
Wanapokuwa wawekezaji wazalendo je wanapata suport sawa na hii wanaopewa wahindi wa TRL? Haiwezekani jamaa wakute kila kitu halafu bado na pesa uwapatie wao kazi yao kuongoza siamini kama kuna watanzania wameshindwa kuongoza kama watapewa support kama ya hawa jamaa.
Ni wakati muafaka kwa serikali kukubali mashirika au kampuni zinazotaka kufa zife haraka kuliko kuziacha zichukue muda mrefu kufa wakati watanzania wataumia zaidi kama kampuni za namna hii zitakawia kufa, tazameni kesi ya Enron ilielekea kufa na ikafa haraka, jana kuna benki kubwa ya marekani imetangazwa mufilisi na hiatachukua muda utasikia mambo yamekwisha. Sasa bongo kampuni inaelekea kufa mnataka kuizuia isife kwa gharama za watanzania.
Vyovyote vile ni mtazamo wangu kutokana na habari iliyoandikwa na Thisday, wajumbe mjadala huko kwenu karibuni tunahitaji nondo za kiuchumi na biashara hapa, umbumbu wetu katika mambo haya unatugharimu.