Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
Fidelis Butahe na Aidan Mhando
SAKATA la mgogoro wa Ziwa Nyasa limezidi kuchukua sura mpya baada ya Serikali ya Tanzania kupingana na kauli ya Rais wa Malawi, Joyce Banda aliyetangaza nchi hiyo kujitoa katika mazungumzo ya kutafuta suluhu ya mgogoro huo baada ya kubaini kuwa Tanzania imezindua ramani mpya inayogusa mipaka ya ziwa hilo.
Kauli hiyo ya Banda aliyoitoa juzi ilionekana wazi kufifisha matumaini yaliyokuwa yameanza kupatikana kupitia mazungumzo hayo.
Jana Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ilisema mabadiliko ya ramani ya taifa hayahusiani na mgogoro wa Malawi na Tanzania katika Ziwa Nyasa.
Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa wizara hiyo, Dk Selassie Mayunga aliliambia Mwananchi kuwa mabadiliko ya ramani yanatokana na kuongezwa kwa mikoa mipya pamoja na wilaya, lakini hayahusiani na mgogoro uliopo.
Ni kweli kuna mabadiliko ya ramani ya taifa lakini mabadiliko haya yanatokana na kuongezeka kwa mikoa na wilaya mpya, alisema Dk Mayunga na kuongeza:
Mipaka ya nchi katika mabadiliko ya ramani hii imebaki kama ilivyokuwa enzi za ukoloni na hatuwezi kufanya mabadiliko ya mipaka hiyo.
Dk Mayunga alibainisha kwamba siyo vyema mabadiliko hayo yakahusishwa na mgogoro wa Tanzania na Malawi kwa kuwa hakuna uhusiano wowote kati ya ramani ya Taifa na ramani ya mipaka hiyo.
Tumeamua kufanya mabadiliko hayo hasa kwa kutambua kwamba kuna mikoa mipya minne na wilaya 19 jambo ambalo lilikuwa na ulazima wa kutoa ramani mpya ya kuonyesha wilaya hizo na mikoa hiyo ili wananchi wafahamu mipaka ya maeneo yao, alisema.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule alipoulizwa kuhusu suala hilo alitaka apewe muda ili azungumze na mabalozi wanaoziwakilisha nchi hizo kila upande, ili kutoa jibu sahihi.
Uamuzi wa Malawi kujitoa katika mazungumzo hayo, umekwenda sambamba na kufutwa kwa ziara ya Rais Banda nchini, hatua ambayo inazidisha mgogoro baina ya nchi hizi mbili.
Rais Banda alisema tayari ameiagiza Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi yake, kujitoa katika mazungumzo hayo kutokana na kile alichodai kuwa ni vitendo vya Tanzania kutoashiria utafutaji wa suluhu kwa njia ya amani.
Rais Banda alitoa agizo hilo alipokuwa akilihutubia taifa hilo baada ya kurejea nchini kwake akitokea Umoja wa Mataifa (UN) alikokuwa kwa ziara ya kikazi.
"Wakati naondoka kwenda UN nilidhani suala la mpaka wa Malawi na Tanzania lilikuwa likihitaji mazungumzo, lakini nikiwa huko nikasikia kwamba Tanzania imezindua ramani mpya inayogusa ziwa hilo," alisema Banda na kuendelea:
"Baada ya hatua hiyo wavuvi wa Malawi wameanza kufukuzwa ufukweni na boti zetu zinaondolewa Tanzania. Ni suala zito sasa ambalo tunatakiwa kuchukua hatua nyingine," alisema.
Alisema mbali na kuzinduliwa kwa ramani, pia alishangazwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete alipolihutubia taifa na kuilaumu nchi yake kwamba inawazuia Watanzania wasitumie maji ya Ziwa Nyasa.
Banda alisema akiwa UN alijadiliana na Katibu Mkuu Ban Ki-moon kuhusu suala hilo kwa lengo la kupata mawazo kabla ya kulifikisha suala hilo Mahakama ya Haki ya Kimataifa (ICJ).
Kuvunjika kwa mazungumzo hayo kumekuja baada ya kuwapo kwa vikao kadhaa vilivyofanyika nchini Malawi na Tanzania, ambavyo hata hivyo, havikuweza kupata mwafaka.
Alipotakiwa kuzungumzia hatua hiyo ya Malawi alisema," Ndiyo kwanza nasikia kwenu. Sijapata mawasiliano na waziri ila ninachojua, ndani ya mwezi huu (Oktoba) mazungumzo hayo yataendelea."
Serikali yaikana Malawi ramani ya Ziwa Nyasa
SAKATA la mgogoro wa Ziwa Nyasa limezidi kuchukua sura mpya baada ya Serikali ya Tanzania kupingana na kauli ya Rais wa Malawi, Joyce Banda aliyetangaza nchi hiyo kujitoa katika mazungumzo ya kutafuta suluhu ya mgogoro huo baada ya kubaini kuwa Tanzania imezindua ramani mpya inayogusa mipaka ya ziwa hilo.
Kauli hiyo ya Banda aliyoitoa juzi ilionekana wazi kufifisha matumaini yaliyokuwa yameanza kupatikana kupitia mazungumzo hayo.
Jana Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ilisema mabadiliko ya ramani ya taifa hayahusiani na mgogoro wa Malawi na Tanzania katika Ziwa Nyasa.
Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani wa wizara hiyo, Dk Selassie Mayunga aliliambia Mwananchi kuwa mabadiliko ya ramani yanatokana na kuongezwa kwa mikoa mipya pamoja na wilaya, lakini hayahusiani na mgogoro uliopo.
Ni kweli kuna mabadiliko ya ramani ya taifa lakini mabadiliko haya yanatokana na kuongezeka kwa mikoa na wilaya mpya, alisema Dk Mayunga na kuongeza:
Mipaka ya nchi katika mabadiliko ya ramani hii imebaki kama ilivyokuwa enzi za ukoloni na hatuwezi kufanya mabadiliko ya mipaka hiyo.
Dk Mayunga alibainisha kwamba siyo vyema mabadiliko hayo yakahusishwa na mgogoro wa Tanzania na Malawi kwa kuwa hakuna uhusiano wowote kati ya ramani ya Taifa na ramani ya mipaka hiyo.
Tumeamua kufanya mabadiliko hayo hasa kwa kutambua kwamba kuna mikoa mipya minne na wilaya 19 jambo ambalo lilikuwa na ulazima wa kutoa ramani mpya ya kuonyesha wilaya hizo na mikoa hiyo ili wananchi wafahamu mipaka ya maeneo yao, alisema.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, John Haule alipoulizwa kuhusu suala hilo alitaka apewe muda ili azungumze na mabalozi wanaoziwakilisha nchi hizo kila upande, ili kutoa jibu sahihi.
Uamuzi wa Malawi kujitoa katika mazungumzo hayo, umekwenda sambamba na kufutwa kwa ziara ya Rais Banda nchini, hatua ambayo inazidisha mgogoro baina ya nchi hizi mbili.
Rais Banda alisema tayari ameiagiza Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi yake, kujitoa katika mazungumzo hayo kutokana na kile alichodai kuwa ni vitendo vya Tanzania kutoashiria utafutaji wa suluhu kwa njia ya amani.
Rais Banda alitoa agizo hilo alipokuwa akilihutubia taifa hilo baada ya kurejea nchini kwake akitokea Umoja wa Mataifa (UN) alikokuwa kwa ziara ya kikazi.
"Wakati naondoka kwenda UN nilidhani suala la mpaka wa Malawi na Tanzania lilikuwa likihitaji mazungumzo, lakini nikiwa huko nikasikia kwamba Tanzania imezindua ramani mpya inayogusa ziwa hilo," alisema Banda na kuendelea:
"Baada ya hatua hiyo wavuvi wa Malawi wameanza kufukuzwa ufukweni na boti zetu zinaondolewa Tanzania. Ni suala zito sasa ambalo tunatakiwa kuchukua hatua nyingine," alisema.
Alisema mbali na kuzinduliwa kwa ramani, pia alishangazwa na kauli ya Rais Jakaya Kikwete alipolihutubia taifa na kuilaumu nchi yake kwamba inawazuia Watanzania wasitumie maji ya Ziwa Nyasa.
Banda alisema akiwa UN alijadiliana na Katibu Mkuu Ban Ki-moon kuhusu suala hilo kwa lengo la kupata mawazo kabla ya kulifikisha suala hilo Mahakama ya Haki ya Kimataifa (ICJ).
Kuvunjika kwa mazungumzo hayo kumekuja baada ya kuwapo kwa vikao kadhaa vilivyofanyika nchini Malawi na Tanzania, ambavyo hata hivyo, havikuweza kupata mwafaka.
Alipotakiwa kuzungumzia hatua hiyo ya Malawi alisema," Ndiyo kwanza nasikia kwenu. Sijapata mawasiliano na waziri ila ninachojua, ndani ya mwezi huu (Oktoba) mazungumzo hayo yataendelea."
Serikali yaikana Malawi ramani ya Ziwa Nyasa