Serikali yagoma kuongeza posho za wanafunzi Urusi

Mtanzania

JF-Expert Member
May 4, 2006
4,816
678
Serikali yagoma kuongeza posho za wanafunzi Urusi
Na Andrew Msechu

SERIKALI imegoma kulipa posho zinazodaiwa na wanafunzi wa Tanzania waliopo katika Chuo Kikuu cha Lumumba mjini Moscow nchini Urusi, waliovamia ubalozi wa Tanzania nchini humo Jumanne wiki hii, kwa maelezo kwamba madai yao si sahihi.


Wanafunzi hao waliopo mwaka wa maandalizi ya lugha katika chuo hicho wanadai kuwa, walitakiwa kulipwa fedha za miezi ya Agosti, Septemba na Oktoba mara baada ya kuwasili chuoni hapo Septemba mwaka jana, lakini hawakulipwa ila walilipwa kuanzia Novemba mwaka jana.


Taarifa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilikanusha madai ya wanafunzi hao na kusema kuwa, si sahihi na haitambui; na kuwa hawatastahili malipo hayo kwa kuwa walitakiwa kuripoti chuoni hapo Novemba mwaka jana na si Agosti kama wanavyodai.


Taarifa ya wizara hiyo ilieleza jana kuwa, madai hayo si sahihi na kuwa wanafunzi hao walilipwa fedha zao zote za posho tangu Novemba 2007 hadi Septemba 2008 kwa mujibu wa taratibu zilizopangwa na wizara hiyo.


Aidha, taarifa hiyo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, ilieleza kuwa tayari Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (Helsb), imeshaagizwa kuwalipa wanafunzi hao posho zao za mwaka 2008/09 kuanzia Oktoba mwaka huu.


揌atua zote za kuwashauri wanafunzi hao kuondoka ubalozini hapo zimeendelea kwa siku mbili mfululizo bila mafanikio,?ilieleza taarifa hiyo.


Iliongeza kuwa, wizara hiyo kwa kushirikiana na ubalozi wa Tanzania mjini Moscow, inaendelea na juhudi za kuwashauri wanafunzi hao ili warejee kwenye vyuo vyao kwa ajili ya kuendelea na masomo.


Wanafunzi hao wameendelea kukaa katika ubalozi huo wa Tanzania wakidai kuwa hawataondoka hadi hapo watakapopatiwa posho zao au kupata majibu ya kina yanayoweza kuondoa utata uliopo katika malipo ya posho hizo.


Mwaka jana, Serikali iliwakana wanafunzi wa Tanzania waliokuwa wakisoma nchini Ukraine ambao pia walikuwa wakidai malipo ya posho na ada kutoka Helsb, ikidai kuwa walikwenda kwa utaratibu usiokubalika.


Hatua hiyo ilizua mtafaruku mkubwa kupitia iliyokuwa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu wakati huo, chini ya aliyekuwa waziri wake, Prof Peter Msolla na wazazi wa wanafunzi hao, suala lililosababisha vyama vya siasa na vya kiraia kuingilia kati.
 
Ndio maana wameamua kufungua tawi la CCM. Kama alivyosema Mwanakijiji, if you can't fight them, join them.

Wakishinda CHADEMA 2010 sijui hao wanafunzi watabadili tawi na kuwa la CHADEMA?

Ukiwa malaya kwenye maisha, jiandae kutumiwa.
 
Kweli kabisa mkuu.jana nilionya hao jamaa waache kujihusisha na uanzi ambao unafaidisha wengine huku wao na wazazi wao kule nyumbani wakiumia pasipo sababu.
 
shule zimefungwa.......wanafunzi hawana kazi and they have lots of time! wache walale ubalozini
 
shule zimefungwa.......wanafunzi hawana kazi and they have lots of time! wache walale ubalozini


Hapana mkuu
Gharama za maisha zimepanda sana na mkopo unaotolewa kwa wanafunzi ni kiasi kidogo sana kiasi kwamba kinawafanya wanafunzi kujuta kwanini wameenda huko kutafuta elimu.

Ushauri wangu kwa serikali ni ingejikita kuboresha vyuo vyetu na kujenga vingi zaidi na hao ambao wapo masomoni iwahudumie na iachane kabisa na mtindo wa kuwapeleka wanafunzi nje ya nchi.

Maana wengi wana acha masomo na kupoteza malengo na matumaini kutokana na hii posho .
 
Mkuu mkamap,Mawazo yako ni ya maana.Ukweli wa mambo ni kwanza Serikali iache kudhamini wanafunzi wanaoenda kusoma Ng'ambo haswa Eastern Hemisphere nikiwa na maana ya Russia,Ukraine,Poland,Bulgaria,India,China na Korea.Sehemu hizo ukiacha Japan hazina ujanja wa kufanya kazi kama wewe ni Mwanafunzi.Kwa watu wa Russia na Ukraine mwanzoni mwa miaka ya 1990 kulikuwa kuna unafuu kwa sababu walikuwa na uwezo wa kuingia Scandinavia bila visa,huko walienda wakati wa summer kufanya kazi ya kuchuma matunda Strawberries/Blackberries. wengi walikwenda Kristinahamm (Sweden) wenyewe walikuita kwa Mama.Kwa kipindi cha miezi miwili ya likizo kulikuwa na uwezekano wa kurudi Russia na $ kati ya 1000 mpaka 1500 ambazo zilipunguza ugumu wa maisha kwa karibu mwaka mzima wa masomo.

Kama serikali inatoa udhamini ihakikishe allowance za wanafunzi zinakwenda kwa wakati unaotakiwa,vinginevyo ni kuwapa mateso makubwa vijana kwenye eneo hilo lenye baridi kali na ubaguzi.Nijuavyo Mimi serikali kwa kupitia Balozi James Kateka (aliwahi kuwa Ambassodor Russia) iliwahi kuomba Wizara ya Elimu ya Juu kuacha kupeleka wanafunzi Russia kwaudhamini wa Serikali,waliokwenda huko ni wale wa Udhamini binafsi,ambao wazazi wao ndio walikuwa wanawajibika na Posho +Tuition fees.

Bodi ya Mikopo na Wizara husika,ni vyema kuhakikisha kuwa Vijana wote wanalipwa Posho zao na kuondoa kero Ubalozini pamoja na vyuo wanavyotoka wanafunzi hao.Kutokulipa posho kunasababisha mahangaiko na matokeo mabaya ya mitihani kwa wahusika.Jiungeni Pamoja na shinikizeni Wizarani ili posho ije mapema kabla ya mwaka wa masomo.Mliopo Lumumba wasiliane na viongozi waliopita hapo,wawape njia muafaka ya kushughulikia tatizo hilo,kuna magwiji wanaojua ku-deal na masuala hayo,wasilianeni na Dr,Issa Kaniki anaweza kuwa msaada kwenu.
 
Mkuu mkamap,Mawazo yako ni ya maana.Ukweli wa mambo ni kwanza Serikali iache kudhamini wanafunzi wanaoenda kusoma Ng'ambo haswa Eastern Hemisphere nikiwa na maana ya Russia,Ukraine,Poland,Bulgaria,India,China na Korea.Sehemu hizo ukiacha Japan hazina ujanja wa kufanya kazi kama wewe ni Mwanafunzi.Kwa watu wa Russia na Ukraine mwanzoni mwa miaka ya 1990 ilikuwa kuna unafuu kwa sababu walikuwa na uwezo wa kuingia Scandinavia bila visa,huko walienda wakati wa summer kufanya kazi ya kuchuma matunda Strawberries/Blackberries. wengi walikwenda Kristinahamm (Sweden) wenyewe walikuita kwa Mama.Kwa kipindi cha miezi miwili ya likizo kulikuwa na uwezekano wa kurudi Russia na $ kati ya 1000 mpaka 1500 ambazo zilipunguza ugumu wa maisha kwa karibu mwaka mzima wa masomo.

Kama serikali inatoa udhamini ihakikishe allowance za wanafunzi zinakwenda kwa wakati unaotakiwa,vinginevyo ni kuwapa mateso makubwa vijana kwenye eneo hilo lenye baridi kali na ubaguzi.Nijuavyo Mimi serikali kwa kupitia Balozi James Kateka (aliwahi kuwa Ambassodor Russia) iliwahi kuomba Wizara ya Elimu ya Juu kuacha kupeleka wanafunzi Russia kwaudhamini wa Serikali,waliokuja huko ni wale wa Udhamini binafsi,ambao wazazi wao ndio walikuwa wanawajibika na Posho +Tuition fees.

Bodi ya Mikopo na Wizara husika,ni vyema kuhakikisha kuwa Vijana wote wanalipwa Posho zao na kuondoa kero Ubalozini pamoja na vyuo wanavyotoka wanafunzi hao.Kutokulipa posho kunasababisha mahangaiko na matokeo mabaya ya mitihani kwa wahusika.Jiungeni Pamoja na shinikizeni Wizarani ili posho ije mapema kabla ya mwaka wa masomo.Mliopo Lumumbawasiliane na viongozi waliopita hapo,wawape njia muafaka ya kushughulikia tatizo hilo,kuna magwiji wanaojua ku-deal na masuala hayo,wasilianeni na Dr,Issa Kaniki anaweza kuwa msaada kwenu.

Mkuu
saizi nchi nyingi zipo shengeni unakwenda unapotaka lakini sheria za european union zimebana sana kiasi kwamba kimewaelea watu wasio memba,yani kupata kazi sio rahisi kabisa.

Hata hivyo mimi nashauri wasipeleke watu kabisa maana hata tuseme UK ama USA ndugu yangu ni kazi ya ziada kubeba maboksi ama usiku kucha unatengeneza nyama baridi za KEBAB harafu uingie darasani kwenye chuo serious.

Maranyingi watu wanaenda vyuo vya kisanii mara mbili kwa week unaenda shule harafu mda wote ni kufanya kazi ,harafu mtu wa namna hii akimaliza shule anaenda kukabidhiwa ofsi kubwa .Kuna tatizo sana ,serikali kama haitaki kutoa pesa za kutosha isipeleke kabisa .
 
Inagoma kuwasaidia ,hii yote inatokana na mipango ambayo haiandaliwi tokea mwanzo,ni yale mambo ya kusukumizana ,kila kitu kitafuata baadae ,usione feza imeshatafunwa ,inakuwaje Raisi anasafiri kila siku,mafisadi wanachota feza,mikataba ya hela kubwa haimaliziki , lakini feza ya kuwasaidia waliokwenda huko haipo ,lakini sioni ajabu pengine watototo wa walala hoi ambao husomea vibatali hawakupewa fursa hiyo ,walinyimwa walibaguliwa ,au hata intervew yao waliyopasi vizuri ilipindishwa na kuchaguliwa watoto wa vigogo ,sasa yanayowakuta watajua kama wao walipelekwa huko kimipango na feza iliyokusudiwa kupewa wao nayo pia imefanyiwa mipango.
 
serikali ya tanzania haijali wanafunzi wake hasa wale waliopo nje ya nchi.Niliwahi sikia wanafunzi waliopo CHINA waliomba kuongezewa posho yao wanaopewa na heslb toka dola 50 kwa mwezi hadi dola 100 sijuhi waliongewa au vipi,wadau walio karibu na heslb ebu tupashen vipi hao vijana mliwaongezea hizo pesa au vipi?na kama bado tatizo nini?
 
Ndio maana wameamua kufungua tawi la CCM. Kama alivyosema Mwanakijiji, if you can't fight them, join them.

Wakishinda CHADEMA 2010 sijui hao wanafunzi watabadili tawi na kuwa la CHADEMA?

Ukiwa malaya kwenye maisha, jiandae kutumiwa.

I'm ready to sponsor the opening of CCM branch in Moscow!
Let me have your contacts
 
Back
Top Bottom