Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,167
- 79,331
Wajameni mie nashindwa kuelewa maana ya kufunga! ina maana watuhumiwa hawana kesi ya kujibu au? na kama ni hivyo zile billioni 11 zilienda wapi? Naomba kueleweshwa!
Wajameni mie nashindwa kuelewa maana ya kufunga! ina maana watuhumiwa hawana kesi ya kujibu au? na kama ni hivyo zile billioni 11 zilienda wapi? Huu usanii ni Mungu anajua
Kwa hiyo mawaziri hawa wataidai fidia serikali.
asante mkuu huruma ilikuwa ishaniporonyoka nilikuwa najua Dowans style mambo ya serikali kususia kesi duh hiki kiswahili nacho! BTW naona Daily News limekuwa linalisifia jimbo la Rombo hata kurudia habari sijui kunani huko? au ndo mambo ya kusafishana taratibu....ina maana upande wa serikali umemaliza kuwasilisha ushahidi wke dhidi ya watuhumiwa, kinachofuatia nikwa mahakama kupitia ushahidi huo na kuona kama watuhumiwa wana kesi ya kujibu, ikiwa ipo basi mahakama inatoa nafasi kwa watuhumiwa kujitetea na kisha hukumu kutolewa, so mambo bado magumu kwa akina Mramba.... punguza jazba comrade!
CCM oyeeeeeeee.
MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA.
Serikali imekua ikiendeshwa kikomedian sana mkuu.Zombe anaidai serikali fidia ya bilioni tano, dowans, bado iptl tunailipa kila builioni 5, hawa wakina yona nao watataka tuwalipe mabilioni, liyumba naye akitoka.....
Jamani hii nchi inakwenda wapi?
SOURCE:
MICHUZI
Mi nilijua hii ni danganya toto tu maana wahisani waliposikia kashfa za EPA waligoma kuchangia badget ya mwaka 2009/10 ndo maana ikawakamata yona na mramba ili kuwadanganya kuna uwajibikaji.
Pia ukifuatilia huyo jaji aliyekua amekabidhiwa hiyo kesi bwana Utamwa mi namjua vizuri alikua mkoani kwenye mahakama za rufaa ila kwa muda wa mwaka mmoja amepandishwa vyeo mara tatu...kapandishwa kua msajili wa mahakama kuu kabla hata mwaka haujaisha kapandishwa kua jaji wa mahakama kuu na hapo ndipo alipokabidhiwa kesi ya yona na mramba.
KWELI HII NCHI INA WENYEWE!!
Mpaka mkwere amalize muda wake tutakula nyasi.
Kama ndo hivi nashukuru mkuu ila tusubirie tuone hukumu maana bado siamini kama hukumu itakua ya halali au yenye ukweli ndani yake.Mkuu punguza jazba, kufunga kesi na kuachiwa huru ni vitu viwili tofauti, kufunga kesi maana yake ni kuwa upande wa mashtaka umekamilisha ushaidi wake sasa kinachosubiliwa ni mahakama kuja na kauli kama watuhumiwa wana kesi ya kujibu au hawana kesi ya kujibu. huyo michuzi uliyemkoti kichwani bure kabisa inaonekana hata yeye hiyo habari kaipata kwa text msg. kama yeye ni mwandishi makini angalau angeandika kesi ya Mramba ushaidi wakamilika, hao ndio waandishi wetu hata akiwa chooni anataka yeye ndio aonekane ndio mtoa habari wa kwanza. pumba.
Ndio nchi ilivo, maamuzi tulikuwa nayo nov. hatukuamini tulipoambiwa.... hawa na wenyewe kama Zombe, watashinda na kudai kiinua mgongo chao.... Chama cha kijani juu!!!!!!:welcome:we mkuu unalosema ni la kweli ama uzushi?
kama ni kweli,basi walipanga iwe hivyo ndio maana ccm waliwasimamisha kugombea ubunge wakitambuwa kuwa watatoka tuu
jamani hii nchi mbona ipo hivi?
haya jamani maamuzi sahihi tunayo wananchi wakati ndio huuuuuuu
mapinduziiii daimaaaaaaaaalane: