Serikali yadaiwa sh bil. 7 na TTCL

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,172
Serikali yadaiwa sh bil. 7 na TTCL


na Bakari Kimwanga


amka2.gif
SERIKALI pamoja na idara zake inadaiwa deni la sh bilioni 7.2 na shirika la simu la TTCL hali inayosababisha shirika hilo nchini kushindwa kujiendesha kiushindani zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Said Amiri Said, aliyasema hayo wakati akizungumza na Waziri wa wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, ambaye alifanya ziara ya kiutendaji katika shirika hilo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi huyo wa TTCL alisema ili kuweza kujiendesha ni lazima serikali ilipe madeni inayodaiwa ikiwa ni pamoja na kulilipa shirika mtaji wa kujiendesha wa dola za Marekani milioni 230!
Said alisema hata kama kutakuwa na ugumu wa kupata fedha za mtaji, serikali itoe walau dola milioni 50, ili kuweza kuingia katika ushindani wa kibiashara na kampuni nyingine za simu za mkono.
Akizungumzia hilo, Profesa Mbarawa, alikiri serikali kufahamu changamoto zinazolikabili shirika hilo.
Lakini alisema kuwa serikali bado inaendelea na juhudi za kulipa madeni hayo ili kuweza kuleta ufanisi TTCL na idara zake.
“Pamoja na changamoto hizo… lakini kuwa na furahi kuona sasa tuna kitengo maalum cha kuendesha mkanga wa taifa wa mawasiliano sasa fanyeni kazi kwa kujituma na maarifa zaidi,” alisema Profesa Mbarawa.
Akizungumzia lengo la ziara hiyo, alisema ni kujua changamoto zinazowakabili na kueleza mikakati mbalimbali ya serikali jinsi ilivyojipanga katika kuboresha huduma katika idara zake na kijamii.
 
HAPO HAPO UTASHANGAA WANAENDA KUWALIPA MAFISADI WA DOWANS YALE MABILIONI LAKINI WANASHINDWA KUWALIPA TTCL DENI LA BILIONI 7.

Because hypocrisy stinks in the nostrils one is likely to rate it as a more powerful agent for destruction than it is.
 


TTCL yahitaji Sh bil. 322 kujikwamua


Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 22nd December 2010 @ 23:15

ILI ijipanue na kupambana na ushindani wa kibiashara uliopo, Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), inahitaji mtaji wa zaidi ya Sh bilioni 322 na kwa kuanzia Sh bilioni 70, zinahitajika kwa haraka.

Pamoja na mtaji huo, pia kampuni hiyo inakabiliwa na changamoto sugu ya taasisi za serikali kutolipa huduma wanazozitoa hasa simu ambapo mpaka sasa inazidai taasisi za serikali pekee Sh bilioni 7.2.

Hayo yalibainishwa jana na Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Said Said alipojibu maswali ya waandishi wa habari wakati wa mkutano baina ya Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa na watumishi wa kampuni hiyo.

"Si kwamba hatuwezi kujiendesha, tunajenga minara, tunalipa mishahara, lakini ili kuweza kujipanua kibiashara tunahitaji Dola za Marekani milioni 230, lakini fedha hizo kwa kampuni yoyote ni nyingi, kwa uchache wake tukipata Dola milioni 50, tutapanuka katika soko," alisema Said.

Mkutano huo ni sehemu ya ziara ya Waziri huyo kutembelea idara na taasisi zilizopo katika wizara yake baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni.

Said alitoa ufafanuzi huo baada ya waziri awali kueleza kuwa mkutano wake na watumishi wa TTCL (waandishi hawakuwepo), umebaini kuwa kampuni hiyo pamoja na kufanya vizuri katika mawasiliano mpaka sasa, inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo madeni na mtaji.

"Nimefika hapa kufahamiana na wafanyakazi, lakini pia kupitia changamoto zilizopo na kuona namna ya kukabiliana nazo, matumaini ya shirika hili kwa serikali ni makubwa, shirika lina matatizo ya mtaji, lakini tayari suala hilo liko serikalini na utaratibu kupata fedha," alisema Profesa Mbarawa bila kufafanua zaidi.

Aidha, katika kufafanua hilo, Waziri huyo alisema pamoja na hitaji la mtaji pia taasisi za serikali zinadaiwa na kwamba utaratibu unafanywa ili katika kipindi kifupi kijacho madeni hayo yawe yamelipwa.

Hata hivyo, hakuweka wazi kipindi hicho pale alipoulizwa kwa madai kuwa fedha za serikali zina utaratibu wake.

Waziri huyo pamoja na kufafanua namna serikali ilivyoanzisha kitengo cha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) kinachojiendesha tofauti na TTCL, alizitaka kampuni za ndani na nje ya nchi kutumia mkongo huo ili kurahisisha mawasiliano na kuingiza taifa mapato.
 
Well that's the hell of the money for ttcl kupata at once but na madeni wanayodai wakilipwa hata wakipata for a start bilioni 100
 
na wao pia wapandishe bei ili wananchi walipie deni la serikali!tuilize serikali pesa za bajeti ya office communications wamemlipa nani? maana huwepo ktk bajeti.utashangaa zote kakomba BMTL
 
HAPO HAPO UTASHANGAA WANAENDA KUWALIPA MAFISADI WA DOWANS YALE MABILIONI LAKINI WANASHINDWA KUWALIPA TTCL DENI LA BILIONI 7.

Because hypocrisy stinks in the nostrils one is likely to rate it as a more powerful agent for destruction than it is.
TTCL nao wapeleke madai yao Paris
 
Serikali yadaiwa sh bil. 7 na TTCL


na Bakari Kimwanga


amka2.gif
SERIKALI pamoja na idara zake inadaiwa deni la sh bilioni 7.2 na shirika la simu la TTCL hali inayosababisha shirika hilo nchini kushindwa kujiendesha kiushindani zaidi.
Mkurugenzi Mkuu wa TTCL, Said Amiri Said, aliyasema hayo wakati akizungumza na Waziri wa wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, ambaye alifanya ziara ya kiutendaji katika shirika hilo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi huyo wa TTCL alisema ili kuweza kujiendesha ni lazima serikali ilipe madeni inayodaiwa ikiwa ni pamoja na kulilipa shirika mtaji wa kujiendesha wa dola za Marekani milioni 230!
Said alisema hata kama kutakuwa na ugumu wa kupata fedha za mtaji, serikali itoe walau dola milioni 50, ili kuweza kuingia katika ushindani wa kibiashara na kampuni nyingine za simu za mkono.
Akizungumzia hilo, Profesa Mbarawa, alikiri serikali kufahamu changamoto zinazolikabili shirika hilo.
Lakini alisema kuwa serikali bado inaendelea na juhudi za kulipa madeni hayo ili kuweza kuleta ufanisi TTCL na idara zake.
"Pamoja na changamoto hizo… lakini kuwa na furahi kuona sasa tuna kitengo maalum cha kuendesha mkanga wa taifa wa mawasiliano sasa fanyeni kazi kwa kujituma na maarifa zaidi," alisema Profesa Mbarawa.
Akizungumzia lengo la ziara hiyo, alisema ni kujua changamoto zinazowakabili na kueleza mikakati mbalimbali ya serikali jinsi ilivyojipanga katika kuboresha huduma katika idara zake na kijamii.


HIYO NI TTCL, hakyanani sijui TANESCO watakuwa wanadai mabilioni mangapi. Bila shak ni RICHMOND + DOWANS + KAGODA + MAJENGO PACHA+ VIJISENTI.

Hivi kwani huwa zile bajeti kubwa za ofisi zinazozidi hadi za maendeleo huwa haziweki gharama za simu na umeme??? Au wanaweka matumboni mwao. mb..wa kabisa hawa majitu
 
Back
Top Bottom