Serikali ya Tanzania inatumia ipasavyo Tafiti za Wasomi wake?

RayB

JF-Expert Member
Nov 27, 2009
2,751
196
Ndugu wana JF hebu tuangalie naomba suala lazima la utumiaji wa tafiti zetu tunazozifanya hapa Bongo. Katika upeo wangu na mlolongo wangu wa kutafuta elimu nimekumbana na tafiti nyingi sana na mimi mwenyewe nikiwa mmoja wapo wa watu ambao wamebahatika kufanya tafiti mbalimbali ndani na nje ya nchi. Lakini kiukweli mpaka leo sijaona matokeo ya tafiti nyingi ninazozifahamu hapa kwetu.

Resource nyingi sana huwa zinatumika kufanya tafiti hizo lakini mara zinapopelekwa katika nagzi ya serikali ili kufanya maamuzi huwa hazianyiwi kazi ukizingatia na serikali za wenzetu. Na mimi naamini wenzetu wameendelea sana kutokana na hilo na ndo maana katika bajeti zao tafiti huwa zinapewa kipaumbele sana.

Ukipita katika maofisi ya Wizara mbali mbali utakuta makabrasha ya data mbali mbali lakini watu bado wanafanya kazi kwa kutumia miongozo iliyojengwa chini ya data zilizopitwa na wakati ndo kusema wanafanya kazi kutokana na mazoea tu.

Kitu kingine ambacho huwa kinaniumiza kichwa hivi utasikia sijui timu ya wizara ya kilimo ilikuwa Misri kujifunza kilimo cha umwagiliaji lakini wakirudi huku hawafanyii kazi kabisa bali kuonyeshana picha walizopiga katika mabembea huko nchi za watu.

Nawasilisha
 
ha ha ha

wana muda hata wa kusoma hizo tafiti..ndugu?

Wako busy nakuomba msaada ..tanzania sijaona nchi ya ajabu kama hii ambayo solutions zote za matatizo yake lazima wa outsource, hakuna local solutions kutoka kwa wasomi wa ndani.na wala hawazitumii...

utalii mkulu anasema tu-copy huko jamaica na cuba..badala ya kuuliza chuo cha utalii etc etc ni upuuzi mtupu..
 
Na sisi wananchi pia tunachangia.....

Sasa kila mtu anataka furniture za nje,hata kama ubora ni
wa chini kuliko za kwetu...

Serikali bogus,wananchi pia.
 
Na sisi wananchi pia tunachangia.....

Sasa kila mtu anataka furniture za nje,hata kama ubora ni
wa chini kuliko za kwetu...

Serikali bogus,wananchi pia.
Mkuu pinda alishatoa majibu.Alipoambiwa maendeleo makubwa ya kilimo aliyoshudia indonesia inatokana na wanasayansi aliuliza KWANI HUKU HAKUNA WANASIASA?.Kumbuka ni mkuu wa serikali.Maanayake ni kwamba serikali yake wanasiasa wanasema wataalam wanafuata.Ni aibu lakini ndo Tanzania.May be isemwa na IMF au WB.Vingevyo tafiti za ndani havina nafasi.Hapa ni hakina makamba, Sofia Simba, masha, RA EL na hao wenye degree feki ndo wanaongoza sisi tunafuata hakuna tafiti.
 
Tatizo la waTz ni kwamba wanaoenda kujifunza jambo nje si watendaji/wataalamu bali ni adminstrators! Wakisharudi toka kujifunza makarabrasha wanayaweka kwenye mashelf na hawayatendei kazi! Haya mambo ya kukimbilia posho nje yanatuumiza sana nchi yetu!
 
Hii ni topic nyeti na ya msingi sana. Hua ninasikitika sana ninaposikia wanataaaluma wetu na vyuo vyetu vikipigwa vita humu JF as if hakuna kitu wanachokifanya. Kuna tafiti nyingi mno ambazo tena serikali yenyewe ili commission kwa consultancies wa kwenye hivi vyuo majibu yakatolewa lakini utekelezaji sifuri. Tatizo liko wapi? Kwa uzoefu nilouona ni kwamba nchi yetu na uongozi wake kwanza hakuna mfumo wa kuweka vipaumbele (priority setting mechanisms) na la pili na nafikir ndio kuu ni maamuzi ya kimaendeleo yanaagalia zaidi mwelekeo wa kisiasa unavyoenda. Kama rais katoka sehemu flani au waziri wa eneo fulani, mafungu yanenda kule. Ikifika wakati wa uchaguzi hata kama wasomi watatoa decisions za kunusuru nchi kiafya au kiuchumi priority itaelekezwa kupeleka "maendeleo" kule ambako kura sinaweza kupotea. nk
 
ha ha ha

wana muda hata wa kusoma hizo tafiti..ndugu?

Wako busy nakuomba msaada ..tanzania sijaona nchi ya ajabu kama hii ambayo solutions zote za matatizo yake lazima wa outsource, hakuna local solutions kutoka kwa wasomi wa ndani.na wala hawazitumii...

utalii mkulu anasema tu-copy huko jamaica na cuba..badala ya kuuliza chuo cha utalii etc etc ni upuuzi mtupu..
This is Tanzania. Hatuna lolote tunalotaka kujifunza. Tunapoteza muda mrefu kuzurura nje, kama watoto tusio na baba. I dont understand kama viongozi wetu wanafikiriaje mustakabali wa Taifa.Naona kama wanafikiri usanii ndo utatuletea tunayoyahitaji.
 
H… Healthy, Hopeful, Humble, Humorous, Hummus eater

A … Appreciative, Approachable, Activist for global peace & justice

P … Peaceful, positive, …

P … Passionate, practical, …

Y… Youthful, yummy, …
 
tuwe wakweli kidogo by looking at another angle, wengi thesis na projects ni za kudesa, cooking data, na kudownload kutoka kwenye internet. Sasa hizo research zinazofanywa na graduates waliocook data, zinaweza kutumika kivipi ili hali kila mtu anajua aliyefanya hiyo research hajawaji kufanya yoyote reliable hata ya Masters degree ali cook data? graduates mwenye ku-cook data atawezaje kuresearch kitu chenye faida kwa nchi? uzoefu and skill ya kuresearch kaitoa wapi?
 
This is Tanzania. Hatuna lolote tunalotaka kujifunza. Tunapoteza muda mrefu kuzurura nje, kama watoto tusio na baba. I dont understand kama viongozi wetu wanafikiriaje mustakabali wa Taifa.Naona kama wanafikiri usanii ndo utatuletea tunayoyahitaji.


Ndahani, this country has no leader. Ili kuamsha waTz we need a dikteta hata kwa miaka miwili pale ikulu. kwanza hata Rais wa sasa hajui hata Job Description yake au pengine haipo kabisa ktk katiba na hata mawaziri sidhani kuna mwenye job description.

This is a great country without leadership, but amazingly people get away with life!
 
Nchi yeyote ile haiwezi kuendelea bila kufanya tafiti mbalimbali hasa zinazohusu maendeleo ya jamii yake. Tanzania na nchi nyingi za ki-Afrika haziendelei si kwamba hazifanyi tafiti ila misingi ya maendeleo iliyowekwa na viongozi wetu akiwemo Nyerere, Nkrumah, Kenyata na wengineo katika Afirika ilijengwa katika umimi zaidi kuliko maendeleo ya jamii nzima.
Kwa hiyo kiongozi yeyote yule aliye madarakani atahakikisha tafiti zote iwe kwenye elimu,afya,kilimo nk zinakuwa(cooked) ku-support matakwa ya watawala na wanaomzunguka. Kama hayaendani na matakwa yake atatumia nguvu aliyonayo kama(machinery)Mahakama,Bunge (watu) kama REDET,Tume,wanasiasa,watabiri kina Yahaya kuwa ndio misingi mikuu kwake kwa tafiti zozote zile.
Kwa maana hiyo wewe kama una utafiti wako halisia itabidi uchujwe kwanza na wanasiasa, wataupindisha, wakishindwa kuuzuia mahakama au bunge litauzuia.
 
Mkuu Lumbe kula tano,nakubaliana na wewe juu ya ku cook data hata humu jamvini tumo wengi tu.
Pili hizo research naamini zipo ambazo zinaweza kuanza kufanyiwa implementation katika ngazi walizopo hao wasomi kwa kuanzisha miradi kama demonstration kwa jamii, na jamii au wasomi wengine waka copy na ku paste au wakaendeleza kuanzia pale alipoishia yule aliyeanzisha.
 
Wakuu,
Hii ni mojawapo kati ya threads nilizozipenda hapa JF! Ni kweli kabisa tafiti zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya mataifa mbalimbali. Licha ya kwamba maarifa yanayopatikana kupitia tafiti ndio yamemwendeleza mwanadamu kufikia hapa alipo, nchi moja moja hufaidika kiuchumi kutokana na kazi za watafiti wake.
Naomba tunapoendelea kuchangia tuzingatie pia kuwa, tafiti si zile tu zinazofanya na wanafunzi 'wanaodesadesa', yamkini wanafanya hivyo kwa ajili ya certification. Hata hivyo hili ni tatizo ambalo vyuo husika havina budi kulidhibiti, kwa sheria dhidi ya plagiarism. Katika vyuo vingi duniani ukibainika umedesa hiyo degree sahau. Aidha, tunao watanzania wengi ambao wamesoma katika vyuo visivyoendekeza kudesa, sidhani kama hata hawa wamejiingiza katika utamaduni wa 'kupika' takwimu. Kama wanafanya hivyo, basi aliyeturoga alikufa.
Pili, watafiti wengi tulionao (Doctors and Professors) wamekuwa watumishi wa mataifa na mashirika ya nje (wale wenye uwezo wa kutoa research funds) na hapa ni wale waliohama kabisa nchi na/au wale waliobaki nchini. Serikali inao wajibu wa kuwatumia kwa kuwapa maslahi stahili na ku-commission tafiti zao. Bahati mbaya haifanyi hivyo katika kiwango kinachoridhisha. Hapo ndipo taifa linapopata hasara mara mbili, human resource ya nchi inatumika kwa faida ya nchi zingine (Mwalimu alisema, ili nchi iendelee inahitaji watu wake)
Tatu, nchini Tanzania taasisi za utafiti sio vyuo vikuu tu, zipo nyingi. Tatizo lipo katika matokeo ya tafiti za taasisi hizi kufika katika sekta lengwa. Huu nadhani ni wajibu wa taasisi kwa kiasi kikubwa. Huwa najiuliza, inakuwaje matokeo ya tafiti za REDET yanajulikana nchi nzima, lakini kutoka kwingine husikii kitu; au ni kwa sababu za REDET ni za kisiasa na wanasiasa wako interested?
 
Tafiti hazifanyiwi kazi kwa sababu tumetawaliwa sana na siasa, kama tafiti hazina masilahi kwa wanasiasa zinaishia kwenye makablasha.
 
hii ni mada nzuri sana kwa taifa, lakini mafanikio yake yamekuwa pia hayaonekani kwa kuwa tumetawaliwa sana na siasa. Lakini kama sheria ya plagiaism ipo, kwanini isifanye kazi humu nchini? Nadhani taasisi husika ina jukumu la kufuatilia na kumuajibisha mwenye ku-cook data vilivyo, vinginevyo taasisi hiyo ijulukane kuwa imeshindwa kazi na kufutiwa hata uhalali wake. Ni vema hata kuwa na taasisi moja nchini, lakini yenye sifa dhabiti za kupitisha tafiti kama hizi, kuliko kubaki na nyingi zenye kutumika kama loophole ya kufoji taaluma na ku-cook data.

Huenda hali hii ndio imepelekea hata wataalam (hasa Doctors and Professors) humu nchini kijiingiza kwenye siasa, badala ya kubaki kama kioo na washauri wa jamii. Hii ni kwa sababu maslahi yameelekezwa kwenye siasa zaidi kuliko kazi zao. Pia ukijaribu kufuatilia mahusiano kati ya wanasiasa (hasa wabunge) na wasomi katika majimbo huenda yasiwe yenye kuonesha maelewano na ushirikiano katika kupambana na janga la umaskini, maradhi na ujinga. Ni kwa kuwa tu kila mmoja anajiona kuelewa kuliko mwingine.

Ukifuatilia pia bajeti za kila wizara, hakuna hata kifungu cha "researches"! Hii inaonesha ni jinsi gani hata serikali yetu isivyodhamini tafiti, na kama ipo basi wanatumiwa wataalam kutoka nje (outsourcing).

Sawa, ni vema kufanya traninings mbalimbali kwa watumishi, lakini si kila mtumishi anastahili kwenda kila training. Nadhani kila training inavyotokea inastahili kuwapelekea watu wahusika, mf. mhasibu kwa maswala ya fedha na si kwa maswala ya madini. Hata hivyo kila atakayepelekwa aahidi kuleta matunda mara tu atakaporudi, na asipelekwe tena hadi matunda ya aliyohudhuria nyuma yaonekane kutoka kwake.
 
Mkuu Lumbe kula tano,nakubaliana na wewe juu ya ku cook data hata humu jamvini tumo wengi tu.
Pili hizo research naamini zipo ambazo zinaweza kuanza kufanyiwa implementation katika ngazi walizopo hao wasomi kwa kuanzisha miradi kama demonstration kwa jamii, na jamii au wasomi wengine waka copy na ku paste au wakaendeleza kuanzia pale alipoishia yule aliyeanzisha.
Asante mwanawane, sijasikia thesis, wala dissertation yo yote iliyo kuwa implemented hata na UDSM yenye faida si tu kwa nchi hata kwa chuo chenyewe zaidi ya machine za kufyatua tofali alizokuwa anasimamia Dr. Kawambwa.
 
Wakuu,
Hii ni mojawapo kati ya threads nilizozipenda hapa JF! Ni kweli kabisa tafiti zimekuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya mataifa mbalimbali. Licha ya kwamba maarifa yanayopatikana kupitia tafiti ndio yamemwendeleza mwanadamu kufikia hapa alipo, nchi moja moja hufaidika kiuchumi kutokana na kazi za watafiti wake.
Naomba tunapoendelea kuchangia tuzingatie pia kuwa, tafiti si zile tu zinazofanya na wanafunzi 'wanaodesadesa', yamkini wanafanya hivyo kwa ajili ya certification. Hata hivyo hili ni tatizo ambalo vyuo husika havina budi kulidhibiti, kwa sheria dhidi ya plagiarism. Katika vyuo vingi duniani ukibainika umedesa hiyo degree sahau. Aidha, tunao watanzania wengi ambao wamesoma katika vyuo visivyoendekeza kudesa, sidhani kama hata hawa wamejiingiza katika utamaduni wa 'kupika' takwimu. Kama wanafanya hivyo, basi aliyeturoga alikufa.
Pili, watafiti wengi tulionao (Doctors and Professors) wamekuwa watumishi wa mataifa na mashirika ya nje (wale wenye uwezo wa kutoa research funds) na hapa ni wale waliohama kabisa nchi na/au wale waliobaki nchini. Serikali inao wajibu wa kuwatumia kwa kuwapa maslahi stahili na ku-commission tafiti zao. Bahati mbaya haifanyi hivyo katika kiwango kinachoridhisha. Hapo ndipo taifa linapopata hasara mara mbili, human resource ya nchi inatumika kwa faida ya nchi zingine (Mwalimu alisema, ili nchi iendelee inahitaji watu wake)
Tatu, nchini Tanzania taasisi za utafiti sio vyuo vikuu tu, zipo nyingi. Tatizo lipo katika matokeo ya tafiti za taasisi hizi kufika katika sekta lengwa. Huu nadhani ni wajibu wa taasisi kwa kiasi kikubwa. Huwa najiuliza, inakuwaje matokeo ya tafiti za REDET yanajulikana nchi nzima, lakini kutoka kwingine husikii kitu; au ni kwa sababu za REDET ni za kisiasa na wanasiasa wako interested?

Mkulu usiiesabu REDET kama taasisi yenye faida kwa nchi, ni uzushi mtupu hawa jamaa huwa hata hawadensi huwa wanacook data kwa malengo ya kupewa vyeo na wanasiasa.

Pili fikiria kuwa chuo kama mzumbe ambacho wahitimu wake wengi ndio watumishi wa serikali za mitaa na serikali kuu kutokana na historia yake. Maprofessor wake na wahadhiri baadhi wamenunua vyeti, sorry wamedai wamesoma chuo kikuu kinachoitwa Pacific Western University, chuo alichosomea Mh Lyatonga-chuo ambacho ni feki, makao makuu ya chuo ni kibanda kama cha muuza mitumba pale Los Angeles. Hawa wanaweza kweli kumwandaa researcher?
 
Hii thread ni nzuri sana kwa sababu imegusa mojawapo ya sababu ya maendeleo yetu kusuasua.
Wakati umefika tupunguze tafiti nyingi bali tufanye kazi kwani tafiti nyingi lengo lake kwanza ni kuvuta kasma ya kuitengeneza,makongamano na safari za kitafiti baada ya hapo tunaweka makabrasha makabatini.
Tanzania tuna watafiti wengi wazuri sana sikatai lakini watendaji wako wapi?na kama wapo wameonyesha model ya tafiti hizo?
 
Ndugu wana JF hebu tuangalie naomba suala lazima la utumiaji wa tafiti zetu tunazozifanya hapa Bongo. Katika upeo wangu na mlolongo wangu wa kutafuta elimu nimekumbana na tafiti nyingi sana na mimi mwenyewe nikiwa mmoja wapo wa watu ambao wamebahatika kufanya tafiti mbalimbali ndani na nje ya nchi. Lakini kiukweli mpaka leo sijaona matokeo ya tafiti nyingi ninazozifahamu hapa kwetu.

Resource nyingi sana huwa zinatumika kufanya tafiti hizo lakini mara zinapopelekwa katika nagzi ya serikali ili kufanya maamuzi huwa hazianyiwi kazi ukizingatia na serikali za wenzetu. Na mimi naamini wenzetu wameendelea sana kutokana na hilo na ndo maana katika bajeti zao tafiti huwa zinapewa kipaumbele sana.

Ukipita katika maofisi ya Wizara mbali mbali utakuta makabrasha ya data mbali mbali lakini watu bado wanafanya kazi kwa kutumia miongozo iliyojengwa chini ya data zilizopitwa na wakati ndo kusema wanafanya kazi kutokana na mazoea tu.

Kitu kingine ambacho huwa kinaniumiza kichwa hivi utasikia sijui timu ya wizara ya kilimo ilikuwa Misri kujifunza kilimo cha umwagiliaji lakini wakirudi huku hawafanyii kazi kabisa bali kuonyeshana picha walizopiga katika mabembea huko nchi za watu.

Nawasilisha
hizi ndio siasa zenyewe sasa na si kule kwenye jukwaa la siasa kumejaa ushambenga mtupu. Thanks very much na wachangiaje wote wa hii thread for the eye opening issues.
 
Back
Top Bottom