mwankuga
JF-Expert Member
- Aug 30, 2010
- 334
- 120
Nchi yetu imefikia pabaya sana,ambapo wananchi tusipoamua kuchukua hatua,watu wachache wataendelea kutunyonya.Mfano suala la DOWANS,wananchi tunatwika mzigo wa kulipa deni la DOWANS,huku umeme ukiwa wakubabaisha sana.
Viongozi wetu wamekuwa wakiingia mikataba ya kinyonyaji ambayo inawafaidisha wao na mabwana zao,huku wananchi wa kawaida tukiwa na maisha magumu sana.Mfumo wa bei imefanya bidhaa nyingi sokoni kuwa juu sana,lakini huku kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uchungu wakiendelea kula maisha.
Viongozi weti ni wala nyama za watu.Wameingia madarakani kwa mbinu chafu ikiwemo kupata pesa kwa watu wachafu ambapo baada ya kuingia madarakani hulazimika kulipa fadhila kwa matapeli kama akina Rostam Aziz.Kama kweli Kikwete amechaguliwa kihalali na wananchi mbona hasikilizi matakwa ya wananchi,badala yake anawasikiliza watu wachache ambao hatuna imano nao.
Wananchi,tusemi sasa inatosha.Wametunyonya vya kutosha,wametudharau vya kutosha,sasa ni muda wa kufanya mapinduzi,si muda wa kukaa na kunywa kahawa.Ni muda wa kuwapinga wazi wezi hawa ambao wanajifanya ni viongozi.
Viongozi wetu wamekuwa wakiingia mikataba ya kinyonyaji ambayo inawafaidisha wao na mabwana zao,huku wananchi wa kawaida tukiwa na maisha magumu sana.Mfumo wa bei imefanya bidhaa nyingi sokoni kuwa juu sana,lakini huku kikundi cha watu wachache wasiokuwa na uchungu wakiendelea kula maisha.
Viongozi weti ni wala nyama za watu.Wameingia madarakani kwa mbinu chafu ikiwemo kupata pesa kwa watu wachafu ambapo baada ya kuingia madarakani hulazimika kulipa fadhila kwa matapeli kama akina Rostam Aziz.Kama kweli Kikwete amechaguliwa kihalali na wananchi mbona hasikilizi matakwa ya wananchi,badala yake anawasikiliza watu wachache ambao hatuna imano nao.
Wananchi,tusemi sasa inatosha.Wametunyonya vya kutosha,wametudharau vya kutosha,sasa ni muda wa kufanya mapinduzi,si muda wa kukaa na kunywa kahawa.Ni muda wa kuwapinga wazi wezi hawa ambao wanajifanya ni viongozi.