nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Na Joseph Ishengoma
Wuhan, China
Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imekubali kuanza utekelezaji
wa miradi miwili mikubwa nchini (Tazania) katika mwaka wa fedha
2012/2013 ukiwemo ujenzi wa reli ya TAZARA kati ya Kapilimposhi Zambia
na Dar es saalam.
Mradi mwingine ni wa Makaa ya Mawe Ludewa na Chuma Liganga ambayo kwa pamoja itagharimu zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 4.
Akizungumza katika maHafari ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma
katika vyuo vikuu mjini Wuhan, China, Balozi wa Tanzania katika Jamhuri
ya Watu wa China Phillipo Marmo amesema, ujenzi wa miradi hiyo utaongeza
ufanisi katika usafiri na usafirishaji pamoja na kukuza ajira kwa
watanzania.
"Mwaka huu wa fedha, zaidi ya waandisi 400 kutoka China watakwenda Tanzania kuifumua na kuijenga upya reli ya TAZARA," amesema.
"Ujenzi huo utaboresha uimara wa reli na kupunguza muda wa kusafiri
kwa kutumia reli hiyo katika maeneo inapotoa huduma tofauti na ilivyo
sasa."
Reli ya TAZARA iliyojengwa kwa msaada wa serikali ya Watu wa China
kati ya mwaka 195 hadi 1975 imekuwa ikilalamikiwa sana na watumiaji
wake kutokana na ubovu wa miundombinu yake, yakiwemo mabehewa, mataaluma
na hata uongozi.
Kuhsu miradi ya Makaa ya mawe na chuma, Balozi Mmo ameeleza kuwa
miradi hiyo inayotarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili
ujenzi wake takapoanza, itasidia kukuza uchumi wa Taifa na kuongeza
ajira kwa Watanzania.
"Nchi yenye chuma inakuwa na mwelekeo mzuri wa kuwa na viwanda vitakavyotoa ajira kwa wananchi wake," amesema. Kuhusu utalii, Balozi huyo amewataka wanafunzi Watanzania walioko China kuitangaza vema nchi yao ili kuongeza pato la taifa kutokana na China kuwa na idadi kubwa ya watalii kila mwaka.
"China inatoa watalii milioni 100 kila mwaka, kati ya hao ni 10,000
tu wanaoenda Tanzania. Lengo la serikali ni kuendelea kutangaza vivutio
vya utalii tulivyonavyo ili angalau asilimia moja ya watalii wa hapa
waende kwetu," amesema na kuongeza kuwa, "tukifanya hivyo tutaongeza
ajira na kukuza uchumi kupitia nyanja ya utalii". Kati ya watalii
milioni 100 kutoka china, watalii zaidi ya 300,000 wanatembelea Angola.
Maelezo hayo ya Mhe Marmo yametokana na hotuba ya Mwenyekiti wa WUTASA Bi Fatma Waziri kwa mgeni rasmi kuwa uwepo wa wanafunzi wa Tanzania mjini Wuhan ni zaidi ya uanafunzi kwani wamekuwa wakiitangaza vivutio mbalimbali vya utalii kupitia maonesho ya utamaduni.
Awali wahitimu katika riasala yao iliyosomwa na DR. Ally Ahmed Saburi wameiomba serikali kushughulikia kwa haraka maombi ya mikopo ya wanafunzi walioko nje ya nchi kwani wanafunzi wa Kitanzanai wanaotegemea mikopo kutoka bodi ya mikopo na
serikali ya mapinduzi Zanzibar wanapata wakati ngumu na kuishi kwa shida
kutokanana ucheleweshwaji wa fedha.
"Wanafunzi wanaotegemea mikopo ya serikali wanakuwa na maisha magumu kutokana na ucheleweshwaji wa mikopo au wakati mwingine kuikosa kabisa. Tunaomba serikali iliangalie jambo hili kwa ukaribu ili kuepusha aibu wanayopata wanafunzi wanaotegemea mikopo nje ya nchi," alisema Dr. Ally.