Serikali ya CCM yazidi kuchafuka UDOM

Vunjavunja

Member
May 18, 2012
92
11
CCM yazidi kupoteza imani kupitia kwa wasomi wa vyuo, itambulike kuwa chuo kikuu cha UDOM kina wanafunzi wa kila pande ya nchi wapo wa Mtwara(kusini), Kigoma (magharibi), Kagera (kasikazini magharibi), Arusha (kasikazini), Dar-es-salaam (mashariki) na mikoa mingine yote ya Tanzania bara na Zanzibar, ni kilio ambacho watakikumbuka miaka ijayo. Kitu ambacho wanatufanyia wanafunzi wa UDOM kutucheleweshea mkopo wetu ni njia mwafaka ya kwenda tunatangaza sera mbaya kwa serikali ya Tanzania (CCM), Kiukweli ccm ndo mwisho wa utawala wao maana tumejipanga kwenda kueneza cdm katika kata zote hapa nchini wasidhana kuwa wanatunyanyasa sisi ila wajue wanatengeneza bom ambalo litawalipua mda wowote yangu ni hayo wa jf ni kweli tumechoka hali ya wanafunzi ni mbaya pale wazazi wa wanafunzi wa Udom litambueni ndo serikali yetu inayotufanyia haya ikiwa wachache wanajilimbikizia mali ya umma wengi wanakufa na njaa. Mungu ibariki udom.
 
Poleni sana, nasikia chuo kitafungwa kwa sababu hali ya wanachuo ni mbaya
 
ninyi ndio kipenzi cha ccm na kikwete iweje awatende hivyo ? poleni sana naimani kwa mtini mmejifunza next time mtawasikiliza wanaharakati na hamta mchangia tena kikwete mamilioni
 
Ingizeni nguvu na ari ya mabadiliko mioyoni mwenu si kwa sababu serikali ya CCM imewanyima boom bali kumbukeni kuwa wadogo zenu bado wanakalia mawe na madarasa yao yameezekwa nyasi

Kumbukeni kuwa wazazi wenu na wadogo zenu wanatembea zaidi ya kilomita kumi kufuata mahitaji ya maji hospitali ,mabasi,sehemu za kuabudia na starehe

Kumbukeni kuwa jamii nzima wanakunywa maji si salama ,hospitali hazina wafanyakazi wala sawa,wekeni hasira kali ndani yamioyo yenu kuichukia serikali ya CCM na CCM kwa kunyang.anya ardhi ya wazazi wenu yenye mali chini na kuwapa wazungu,waarabu,wahindi,na wasomali

Musipopata hasira ya ujasiri ni kazizi chenu na cha wanenu kitakachopata taabu kwelikweli,tabu zaidi ya hii amkeni sasa nendeni vijijini mukaongee na wazazi wenu,wadogo zenu,jirani zenu kapitisheni ujumbe wa ukombozi ni sasa ni nyie tu munaoweza kusaidia kuchochea mabadiliko ya kifikra toka kwa wazazi wenu na ndugu zenu kiujumla na muna nguvu kwani muko wengi sana
 
Poleni sana jamani. Hii inatia uchungu hasa ukizingatia hali halisi za wazazi wengi wa Tanzania. Maombi yangu kwenu wadada na wakaka vumilieni jamani, jua litachomoza hivi karibuni. Asijiingize mtu kwenye vitendo viovu kwa ajili ya mafisadi hawa. Poleni sana waungwana!
 
Kwa mtu ajuaye maana ya jamii ni nini? Hawezi kusema wanafunzi wa UDOM walimchagia jk fedha kama nilivyo sema kuwa udom ni sehemu ya wanafunzi kutoka pande mbalimbali za nchi hatuwezi wote kuwa cdm au ccm katika jamii ya watu elfu ishirini kama **** kuna vyuo vya watu elfu moja na kuna wachama wa cdm na ccm je udom penyewe watakosa? Kama wewe ni greater thinkers toa maoni yako.
 
wanafunzi wa UDOM tulizeni akili msome, nyie ndo mnapesa sana nakumbuka mwaka 2010 miliichangia ccm , sasa endeleeni kuvuna mlichopanda
 
ukweli wa hayo tutauona hivi karibuni kwenye uchaguzi wenuwa raisi.mtawachagua hao ccm
 
Kwahiyo wakiwapa boom hamtaenda vijijini kueneza harakati za mabadiriko ya kweli hapa Tanzania?
Mbona hasira na maneno yenu makali kuhusu CCM mnayatamka pale mnapokosa boom?HYPOCRICY!
 
CCM yazidi kupoteza imani kupitia kwa wasomi wa vyuo, itambulike kuwa chuo kikuu cha UDOM kina wanafunzi wa kila pande ya nchi wapo wa Mtwara(kusini), Kigoma (magharibi), Kagera (kasikazini magharibi), Arusha (kasikazini), Dar-es-salaam (mashariki) na mikoa mingine yote ya Tanzania bara na Zanzibar, ni kilio ambacho watakikumbuka miaka ijayo. Kitu ambacho wanatufanyia wanafunzi wa UDOM kutucheleweshea mkopo wetu ni njia mwafaka ya kwenda tunatangaza sera mbaya kwa serikali ya Tanzania (CCM), Kiukweli ccm ndo mwisho wa utawala wao maana tumejipanga kwenda kueneza cdm katika kata zote hapa nchini wasidhana kuwa wanatunyanyasa sisi ila wajue wanatengeneza bom ambalo litawalipua mda wowote yangu ni hayo wa jf ni kweli tumechoka hali ya wanafunzi ni mbaya pale wazazi wa wanafunzi wa Udom litambueni ndo serikali yetu inayotufanyia haya ikiwa wachache wanajilimbikizia mali ya umma wengi wanakufa na njaa. Mungu ibariki udom.

mnajirudi? mwaka 2015 nendeni tena mkamchukulie mgombea urais fomu ya kugombea sio ndio zenuu?
 
Hata wakiulizwa viongozi wa cdm ambao wamepa nafasi ya kuitembelea udom wanaikubali kuwa udom kuna kisima cha maji safi ambacho kikielekea urahiani kinaenda kusafisha magambo yote. Ni kweli udom kuna wanachama wengi wa cdm kuliko vyuo vingine hapa nchini kwa ukweli ninaoujua ila tutambue kuna mshika mpini na mshika jembe sijui na nani bora kati ya watu hao wawili.
 
Kasinge waitu! ila jadili kwa lugha ambayo ni known kwa watu wote kutuletea kihaya una maana gani? Au unajua wana jamiiforum wote ni wahaya. Be care!
 
Mh!!! Kazi kweli kweli!! Kama haya Yanawakuta UDOM, sisi ambao tarehe ishirini na nane tunaanza mitihani na kumaliza tarehe sata tumeambiwa kuwa kuna uwezekano mkubwa wa kuja chuoni kusaini fedha za ada kutoka bodi...!!!!

Nakumbuka tulikuwa wakwanza kufungua chuo katika vyuo vyote Tz (Tulifungua 19/9/2011) na kwa mujibu wa maelezo ya mkurugenzi wa bodi, alisema kuwa fedha ziliisha baada ya kutuma kwa vyuo ambavyo viliwahi kufungua...!!! Sasa kama ni hivyo, mbona Mwenge hadi leo watu tunapiga miayo tu???

Maskini mimi, yaani nikimaliza college nitoke Mpanda all the way to Moshi kuja kusaini tuition fee? Hiyo nauli ya kuja na kurudi ni nusu ya fedha ya awamu ya nne ya bodi!!! Kweli ccm na serikali yake MUST GO!!! KWELI TUMECHOKA!!!

POLENI WAHANGA WOTE WA BODI YA MIKOPO YA VYUO VIKUU, LAKINI MKURUGENZI ALIKIRI KUWA HAKUNA FEDHA!!!
 
Hivi hawa si ndiyo walimchangia Kikwete hela ya kuchukulia form? Mbuzi kabisa nyie, I wish msipewe hilo bumu mwaka mzima.
 
Hawa vilaza si ndio waliandamana juzi kumpongeza Jakaya Kikwete kwa kuunda baraza la mawaziri 55 duuh sasa iweje leo walalamike ati Gamba lao linawafanyia vibaya.Poleni sana nafikiri mlisahau ule usemi usemao wajinga ndio waliwao na bado
 
Back
Top Bottom