Kachanchabuseta
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 7,269
- 675
[h=1]Dr Shein amuapisha shekhe Kabhi kuwa Muft mkuu Zanzibar.[/h]Written by 27/09/2011
Na Talib Ussi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi mbali mbali akiwemo Sheikh Saleh Omar Kabhi kuwa Mufti Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Othman Masoud,Mawaziri, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdala Mwinyi, Wakuu wa vikosi vya Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na viongozi wengine.
Source:www.mzalendo.net
Na Talib Ussi
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaapisha viongozi mbali mbali akiwemo Sheikh Saleh Omar Kabhi kuwa Mufti Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika Ikulu mjini Zanzibar.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Spika wa Baraza la Wawakilishi Mhe. Pandu Ameir Kificho, Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Makungu, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Othman Masoud,Mawaziri, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdala Mwinyi, Wakuu wa vikosi vya Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na viongozi wengine.
Source:www.mzalendo.net