Serikali tatu, Rai ya mzee Aboud Jumbe!

Nadhani Aboud Jumbe amefurahi sana hii Rasimu kuiona ikiwa na mawazo yake miaka 30 nyuma na akiwa bado hai!.........!
 
Nadhani Aboud Jumbe amefurahi sana hii Rasimu kuiona ikiwa na mawazo yake miaka 30 nyuma na akiwa bado hai!.........!
Mzee jumbe alidai serikali 3 wakati wazanzibari walisha mchoka na kumchukia ndio maana akataka kurudisha mapenzi yake kwa wananchi wa znz kupitia hoja ya serikali 3 kitu ambacho hakiendani na katiba ya ccm na hasa Nyerere.Na alilifanya hilo hilo kama kutaka kuwalaghai wznz ili aendelee kuishi maisha urais. Fuatilia jumbe aliupata urais mwaka gani na alidai serikali 3 mwaka gani utagundua kama sio muumin wa serikali 3 bali ni mtu mfa maji tuu.m/zimunguu amsameh
 
jumbeee.jpg
RAI YA MZEE ABOUD JUMBE


Ukiachilia mbali kitabu chake cha THE PARTNERSHIP, Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu Wa Kwanza wa Rais wa Tanzania kabla ya kushinikizwa kujiuzuluna chama mwaka 1984 kutokana na msimamo wake wa serikali tatu, ameandika pia kitabu kingine kinachoitwa TUISHI BILA KUBAGUANA.

Kwenye kitabu hicho kilichochapishwa mwaka 2003 Mzee Jumbe anaeleza mengi kuhusu kuvuliwa kwake nyazifa za uongozi kwenye chama na serikali. Fuatana nami nikupe machache;

KIKAONI DODOMA

"…Siku tatu za kwanza za mkutano, Jumanne hadi Alhamis, ni wajumbe wachache tu, wote wakiwa kutoka Tanzania visiwani, ndio waliosimama mmoja baada ya mmoja kulalamika na kushambulia kule walikokuita 'kupenda kwangu na kunyima madaraka, kutosikiliza shauri wala maoni, kujifanyia nitakavyo, kutoipenda CCM na Azimio la Arusha na madai mengine kama hayo'…" ( uk 15)

KUJIUZULU

"….Siku ya Jumamosi, baada ya kumuachia Ramadhani Haji (aliyekuwa Waziri Kiongozi) kutoa maelezo yake, ndipo mimi nilipochambua tuhuma zilizotolewa. Nilipomaliza nikashauri niruhusiwe kuacha shughuli zote za chama na serikali"

BAADA YA KIKAO

"….Nilipowasili nilikofikia, si muda walifika Mabwana Kawawa na Sokoine wakifuatiwa muda mfupi na Mwalimu Nyerere. Niliambiwa kwa vile niliacha madaraka kwa mdomo hakuna ushahidi, bora kufanya uthibitisho kwa maandishi.
Kwa kutotaka 'kuchafua hali ya hewa' niliandika kuacha madaraka ya Makamu Mwenyekiti wa chama na Makamu wa wa Rais wa Muungano, nikampa aliyekuwa mpiga taipu wangu achape. Mwalimu aliponiuliza kuhusu Zanzibar nilimwahidi kufanya hivyo nikifika Zanzibar"

HAIFAI KWENDA ZANZIBAR!

"...Hapo ndipo aliponiambia ingekuwa bora kwa 'sasa' kutokwenda Pemba (Nilikotaka kumpeleka kwao mke wangu niliyekuwa nimefuatana naye ) wala kwenda Unguja na kwa hiyo niandike na kuacha kwangu shughuli za Zanzibar. Kwa kuona wazi wasiwasi uliojidhihirisha, nilikubali yote."

ULINZI MKALI

"...Tulipofika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na kukuta ulinzi mkali wa Jeshi na Polisi, wakiwepo mkuu wa jeshi na mkuu wa jeshi la polisi, nilishindwa kabisa kuelewa sababu na maana ya yote hayo yalikuwa ni ya nini au kwa nini? Mpaka leo hakuna aliyenielimisha na bado niko ujingani" (uk 17)

SIMU IMEKATWA!

"....Nilipwerewa nilipofika nyumbani Mjimwema na kutaka kupiga simu Unguja. Niliona, kabla ya kutangazwa yaliyotokea, niwatulize wake zangu na wanangu Unguja angalau wajue tu nilikuwa salama Mjimwema. Niligundua simu hazifanyi kazi! Hapo nilimshukuru Mwenyezi Mungu nikamwachia yeye na kukaa kusubiri maajabu mengine huku nikiwaza 'Tunakwenda wapi'?"

SERIKALI TATU

"....Mfumo wa serikali tatu ndio umekuwa msimamo wangu na ndio mtizamo wangu uliopingwa vikali na chama..."

MAHUBIRI YA KUUVUNJA MUUNGANO!

"....Wenye kuhubiri kuuvunja muungano, watambue kuwa hawawezi kufanya hivyo kienyeji… Huu ni muungano wa Watanzania, si wa chama hiki au kile. Wote wenye umri wa miaka ishirini na tisa na chini ya hapo ambao naamini ndio wengi, hawajawahi kuwa chochote isipokuwa Watanzania.
Kabla ya kuwanyang'anya au kuwafutia utanzania wao, wana haki ya kushirikishwa kuamua nasaba yao. Hii inamaana itapaswa kufanyika kura ya maoni ili Watanzania wenyewe ndio waamue kuvunja au kubadili mfumo wa Muungano.
Kisheria na kwa mujibu wa katiba, si jambo dogo au jepesi kuvunja Muungano, kama inavyoonekana baadhi ya viongozi kudhani. Lazima Watanzania kuangalia, kutafakari kwa makini na kujuana kwa yakini tunatoka wapi, kwa nini tuliungana, tumefika wapi na sasa tunataka au hatutaki nini, au tunataka kwenda wapi."

RAI YAKE

"....Katika zoezi hili (kuhusu Muungano), wanasiasa na Watanzania kwa ujumla wanapaswa wawe wakweli, wenye busara na zaidi kuliko yote ni uaminifu. Miaka 100 ijayo hapatakuwa, sio tu katika hili bali kote duniani, hata mmoja miongoni mwa walio duniani leo na hata akiwepo hatakuwa na lake. Bali, vizazi vyetu vitakuwepo. Mazao ya mbegu tunazoatika au kupanda leo itabidi kuvunwa na vizazi vyetu kesho"

Kwa uchambuzi/simulizi kuhusu vitabu na waandishi endelea kutembelea ukurasa wetu wa "Kitabu Nilichosoma" (
https://www.facebook.com/KitabuNilichosoma?hc_location=timeline )
Au piga 0653619906 ( Ado) kwa taarifa kuhusu vinakopatikana vitabu vya historia, siasa nk
Kauli mbiu yetu ni KITABU NI SILAHA
 
Mzee jumbe alidai serikali 3 wakati wazanzibari walisha mchoka na kumchukia ndio maana akataka kurudisha mapenzi yake kwa wananchi wa znz kupitia hoja ya serikali 3 kitu ambacho hakiendani na katiba ya ccm na hasa Nyerere.Na alilifanya hilo hilo kama kutaka kuwalaghai wznz ili aendelee kuishi maisha urais. Fuatilia jumbe aliupata urais mwaka gani na alidai serikali 3 mwaka gani utagundua kama sio muumin wa serikali 3 bali ni mtu mfa maji tuu.m/zimunguu amsameh

Mkuu, ni kama tunawaza sawa na wewe hivi? Huyu mzee aliingia madarakani mwaka 1972 soon after Karume's sn death, yeye ndiye kwa ridhaa yake aliunganisha ASP na TANU na kufanya hi ccm tulionayo leo, kitu pekee ambacho watu wengi hua hawataki kukijua ni hiki, kwanini Wazanzibari wengi (viongozi na sio wananchi) huuchukia muungano wakati mambo yao yanapokua hayaendi kama wanavyo taka? Huyu mzee alianza kufanya hivi mara baada ya maandamano ya wazanzibari wengi, nakumbuka UWT tawi la Zanzibar pia lilishikinza mambo fulani enzi za utawala wake, kuzima fujo hizo mwenyekiti wa UWT taifa enzi hizo bibi Sophia Kawawa akatia timu huko, nakumbuka alipendekeza kitu hi, "ndoa za wake wengi sio nzuri" Ukweli ndio aliharibu zaidi cause yeye kama mwislam na ameenda kuyasema hayo kwenye ardhi ya kiislam, palikua hapaotoshi.

And here the SAGAgoes on, maalimu Seif akiwa kama waziri kiongozi zanzibar ndiye aliyemchongea Jumbe kwa Nyerere, alipoona deal la kuja kua rais haliwezekani, akachafua nae hali ya hewa, mzee wa mkasi TX Bilal wengi tunamfahamu jinsi alivyokua anauchukia muungano, sasa hivi mmmh!!!!!
 
View attachment 165829
RAI YA MZEE ABOUD JUMBE


Ukiachilia mbali kitabu chake cha THE PARTNERSHIP, Mzee Aboud Jumbe Mwinyi, aliyewahi kuwa Rais wa Zanzibar, Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na Makamu Wa Kwanza wa Rais wa Tanzania kabla ya kushinikizwa kujiuzuluna chama mwaka 1984 kutokana na msimamo wake wa serikali tatu, ameandika pia kitabu kingine kinachoitwa TUISHI BILA KUBAGUANA.

Kwenye kitabu hicho kilichochapishwa mwaka 2003 Mzee Jumbe anaeleza mengi kuhusu kuvuliwa kwake nyazifa za uongozi kwenye chama na serikali. Fuatana nami nikupe machache;

KIKAONI DODOMA

"…Siku tatu za kwanza za mkutano, Jumanne hadi Alhamis, ni wajumbe wachache tu, wote wakiwa kutoka Tanzania visiwani, ndio waliosimama mmoja baada ya mmoja kulalamika na kushambulia kule walikokuita 'kupenda kwangu na kunyima madaraka, kutosikiliza shauri wala maoni, kujifanyia nitakavyo, kutoipenda CCM na Azimio la Arusha na madai mengine kama hayo'…" ( uk 15)

KUJIUZULU

"….Siku ya Jumamosi, baada ya kumuachia Ramadhani Haji (aliyekuwa Waziri Kiongozi) kutoa maelezo yake, ndipo mimi nilipochambua tuhuma zilizotolewa. Nilipomaliza nikashauri niruhusiwe kuacha shughuli zote za chama na serikali"

BAADA YA KIKAO

"….Nilipowasili nilikofikia, si muda walifika Mabwana Kawawa na Sokoine wakifuatiwa muda mfupi na Mwalimu Nyerere. Niliambiwa kwa vile niliacha madaraka kwa mdomo hakuna ushahidi, bora kufanya uthibitisho kwa maandishi.
Kwa kutotaka 'kuchafua hali ya hewa' niliandika kuacha madaraka ya Makamu Mwenyekiti wa chama na Makamu wa wa Rais wa Muungano, nikampa aliyekuwa mpiga taipu wangu achape. Mwalimu aliponiuliza kuhusu Zanzibar nilimwahidi kufanya hivyo nikifika Zanzibar"

HAIFAI KWENDA ZANZIBAR!

"...Hapo ndipo aliponiambia ingekuwa bora kwa 'sasa' kutokwenda Pemba (Nilikotaka kumpeleka kwao mke wangu niliyekuwa nimefuatana naye ) wala kwenda Unguja na kwa hiyo niandike na kuacha kwangu shughuli za Zanzibar. Kwa kuona wazi wasiwasi uliojidhihirisha, nilikubali yote."

ULINZI MKALI

"...Tulipofika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam na kukuta ulinzi mkali wa Jeshi na Polisi, wakiwepo mkuu wa jeshi na mkuu wa jeshi la polisi, nilishindwa kabisa kuelewa sababu na maana ya yote hayo yalikuwa ni ya nini au kwa nini? Mpaka leo hakuna aliyenielimisha na bado niko ujingani" (uk 17)

SIMU IMEKATWA!

"....Nilipwerewa nilipofika nyumbani Mjimwema na kutaka kupiga simu Unguja. Niliona, kabla ya kutangazwa yaliyotokea, niwatulize wake zangu na wanangu Unguja angalau wajue tu nilikuwa salama Mjimwema. Niligundua simu hazifanyi kazi! Hapo nilimshukuru Mwenyezi Mungu nikamwachia yeye na kukaa kusubiri maajabu mengine huku nikiwaza 'Tunakwenda wapi'?"

SERIKALI TATU

"....Mfumo wa serikali tatu ndio umekuwa msimamo wangu na ndio mtizamo wangu uliopingwa vikali na chama..."

MAHUBIRI YA KUUVUNJA MUUNGANO!

"....Wenye kuhubiri kuuvunja muungano, watambue kuwa hawawezi kufanya hivyo kienyeji… Huu ni muungano wa Watanzania, si wa chama hiki au kile. Wote wenye umri wa miaka ishirini na tisa na chini ya hapo ambao naamini ndio wengi, hawajawahi kuwa chochote isipokuwa Watanzania.
Kabla ya kuwanyang’anya au kuwafutia utanzania wao, wana haki ya kushirikishwa kuamua nasaba yao. Hii inamaana itapaswa kufanyika kura ya maoni ili Watanzania wenyewe ndio waamue kuvunja au kubadili mfumo wa Muungano.
Kisheria na kwa mujibu wa katiba, si jambo dogo au jepesi kuvunja Muungano, kama inavyoonekana baadhi ya viongozi kudhani. Lazima Watanzania kuangalia, kutafakari kwa makini na kujuana kwa yakini tunatoka wapi, kwa nini tuliungana, tumefika wapi na sasa tunataka au hatutaki nini, au tunataka kwenda wapi."

RAI YAKE

"....Katika zoezi hili (kuhusu Muungano), wanasiasa na Watanzania kwa ujumla wanapaswa wawe wakweli, wenye busara na zaidi kuliko yote ni uaminifu. Miaka 100 ijayo hapatakuwa, sio tu katika hili bali kote duniani, hata mmoja miongoni mwa walio duniani leo na hata akiwepo hatakuwa na lake. Bali, vizazi vyetu vitakuwepo. Mazao ya mbegu tunazoatika au kupanda leo itabidi kuvunwa na vizazi vyetu kesho"

Kwa uchambuzi/simulizi kuhusu vitabu na waandishi endelea kutembelea ukurasa wetu wa "Kitabu Nilichosoma" (
https://www.facebook.com/KitabuNilichosoma?hc_location=timeline )
Au piga 0653619906 ( Ado) kwa taarifa kuhusu vinakopatikana vitabu vya historia, siasa nk
Kauli mbiu yetu ni KITABU NI SILAHA

Hivyo vitabu tuambie hapahapa kuwa vinapatikana wapi na si kupigiana simu baadaye!
 
Mzee jumbe alidai serikali 3 wakati wazanzibari walisha mchoka na kumchukia ndio maana akataka kurudisha mapenzi yake kwa wananchi wa znz kupitia hoja ya serikali 3 kitu ambacho hakiendani na katiba ya ccm na hasa Nyerere.Na alilifanya hilo hilo kama kutaka kuwalaghai wznz ili aendelee kuishi maisha urais. Fuatilia jumbe aliupata urais mwaka gani na alidai serikali 3 mwaka gani utagundua kama sio muumin wa serikali 3 bali ni mtu mfa maji tuu.m/zimunguu amsameh

Siasa evolves. Kwanini Jumbe awe na mawazo yaleyale ya 1972?
 
Back
Top Bottom