Serikali, shughulikieni akina 'Sheikh Ponda' haraka sana

Status
Not open for further replies.
Tatizo ni waislam wenyewe..mimi ni mkristo na nimesoma na waislam wengi tu na wamefaulu vizuri na wapo BOT,TRA wengine wanafanya UN Agencies,sijaona waislamu wakikandamizwa tatizo lililopo ni wazazi hawapendi kupeleka mtoto shule,ni rahisi kupima mtoto wa kiislam atachapwa kwa kutokwenda madrasa na sio shule!!!!hili lipo wazi!!!mfumo wa wazazi wa kiislamu si mzuri kwa kweli wanahitaji kubadilika...hawana mpango na shule...Nimebahatika kukulia katika mazingira ya waislamu wengi katika jamii na nimeona watyoto wengi wenzangu wakiacha shule kwa sababu mbalimbali,madawa ya kulevya,umalaya,mimba za mapema,ulevi wa wazazi na kutojali shule.Jiulize lifuatalo..Chukua mfano familia mbili zenye maisha magumu na dini tofauti..Utaona familia ya kikristo inapambana ili mtoto/watoto wao wasome lakini wenzetu hawana hata habari na shule Je Utaulaumu mfumo au Ujinga wa Baadhi ya watu?Sheikh Ponda na mwenzie waulize watoto wao wamewapeleka shule?Pata jibu kisha rudi kwa thread hii.


Yapo majibu humu humu ndani.
Soma na tuwasiliane Insha Allah.
 
Hebu soma hii:

"Hivi sasa kuna vitabu viwili vilivyoandikwa na Wakristo wenyewe vinavyothibitisha kuwa Wakristo wametumia nyadhifa zao katika serikali kuuhujumu Uislam na Waislam. Jan P van Bergen katika kitabu chake, Development and Religion in Tanzania,(1981) [1] ametoboa siri kuhusu uadui aliokuwa nao Rais Mstaafu, Nyerere dhidi ya Uislam na Waislam. Kitabu kinaeleza kwa ufasaha jinsi Nyerere wakati alipokuwa madarakani alivyokuwa akifanya mikutano ya siri na viongozi wa Kanisa kuweka mikakati ya kuupa nguvu Ukristo. Katika mikutano hiyo Nyerere aliwahakikishia viongozi wa Kanisa kuwa anaaunga mkono Ukristo. Kitabu hicho kinaeleza jinsi Nyerere alivyotimiza ahadi yake hiyo kwa Kanisa kwa kuhakikisha kuwa anawapa Wakristo nafasi za juu katika serikali na chama. Kitabu hiki kilikuwa kinauzwa Catholic Bookshop, Dar es Salaam. Lakini ilipokuja kudhihirikia Kanisa kuwa kitabu hiki kilikuwa kinatoa habari nyeti na siri za Kanisa kuhusu njama dhidi ya Waislam, kwa haraka sana kikaacha kuuzwa. [1] Hadi hivi sasa kitabu hicho ni marufuku kuletwa tena Tanzania.

Kitabu cha pili ni cha Dr John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985 (1992). [1] Kitabu hiki kinaeleza njama ndani ya serikali kuuhujumu Uislam. Sivalon anafichua kuwa kuanzia mwaka 1961 baada ya Tanganyika kupata uhuru, Kanisa lilikuwa na hofu mbili. Hofu ya kwanza ilikuwa umoja wa madhehebu za Kiislam kati ya Sunni, Bohora, Ismailia na Ithnasheri. Hofu ya pili ilikuwa kuhamishwa kwa makao makuu ya EAMWS kutoka Mombasa kuja Dar es Salaam. Kanisa lilikuwa linahofu kuwa mali walizokuwanazo Waasia Waislam zikitiwa katika harakati za Waislam ambao walikuwa na nguvu kubwa katika uwanja wa siasa zitaathiri maslahi ya Ukristo katika Afrika ya Mashariki. Kwa ajili hii Kanisa likatanganza kuwa Uislam ni adui wake na ikaanza mikakati ya hujma dhidi ya Uislam ili kuudhoofisha."

Ndugu yangu ikiwa unaishi kwenye nyumba ya nyasi usipendepende kucheza na kibiriti.
Naamini hata tukifika 2030(kama bado Mungu ametuweka hai) utakuwa unatumia hizi reference zako fake...
 
Nasikitika kusema kuwa wewe ndio inaonekana ni mgeni sana kwa Ponda kama unadhani anatafuta umaarufu kwako. ur very wrong. Tatizo lenu huwa mtu mkisha muona ni muislam hata kama anaongea vitu ambavyo ni sahihi basi mfumo huwasukuma kumuona anachoongea ni kuchochea vurugu. Hivi kuhusu NECTA uliwaelewa vizuri? Au umekurupuka tu?

Kwanza nikuulize ivi unajua kama NECTA baada ya waislam kulalamika kuwa matokeo ya Islamic knoledge kwa F6 waliomaliza mwaka huu yalikuwa yamechakachuliwa, walikiri na kutoa mengine tena kimya kimya na angalia utayaona kwenye website, sasa nauliza kama somo moja tena linalowahusu waislam linachakachuliwa hivyo je masomo mengine itakuwaje? Kama una akiri timamu jitahidi kumuelewa mtu anapozungumza kitu kisha umujibu kwa hoja unayohisi ni bora. inshort kuhusu matokeo hayo ya islamic knoledge ilionekana perfomance kitaifa hakuna mwanafunzi aliyekuwa amepata A,B wala C na mwanafunzi wa mwanzo kitaifa aliaanza na alama D tena walikuwa wachache na F nyingi sana baada ya kutoa fact Baraza likakiri na kutoa matokeo mapya, mfano kuna shule after new result of that subject imepanda kitaifa kwa nafasi 109, halafu watu wakiongea wewe unakurupuka nakusema wanachochea vurugu.

Hivi kwani umesikia wako dhidi ya wananchi au wako dhidi ya serikali? Acha ukapopo mkuu. kama wewe unamuona waziri ni dili ktk wizara basi akina ponda wakimalizana na ndalichako na wewe uanze na kawambwa, unaonaje.

Ama suala lingine ambalo una shaka nalo ni lipi kuhusu sensa? kinachotakiwa ni kuwa sensa pia itujue sisi wa watanzania kwa mujibu wa Imani zetu , where is the problem? watu wanasoma lakini kuelimika inakuwa isue


Kwa nn ni Muhimu kujua Imani zetu,taarifa hiyo itatusaidia vp Kupanga Maendeleo?
Tukijua Wakristo ni Wengi kuliko Waislamu inatusaidia nn? Kwamba kundi godo liongeze juhudi ya Kuzaa?
 
Serikali ipi? Hii ya JK onayowabembeleza uamsho warudi kwenye 'ajenda yao ya msingi' badala ya kuwafutia usajili!!!!
 
Wakati mwingine tunapojaraibu kuchangia hoja tumwangalie mtoa mada au hoja ni mtu wa namna gani.
Mtu kama ponda ni mtu wa aina gani , ana uwezo wa aina gani , elimu yake ni kiasi gani ndipo tuweze kuanza kulumbana ama kuelimisha , la sivyo tutakuwa tunabishana na vichaa kwa kujaribu kuonyesa ukweli ambao hawana uwezo wa kuujua
je maswala ya elimu kweli yanaweza kuongelewa na ponda na rafiki zake. Ponda ana ufahamu wa kuongelea maswala ya elimu ? Je anazo data zakuweza kuongelea jambo hili. Unaweza kutumia maswala ya udini kufikia lengo unalotaka hii haijalishi msomi kama kighoma malima au mfilisi kama ponda wote hawana hoja ya kushadadia mambo wasemayo.
Dini ya kikristo hasa katoliki iliwekeza sana katika nyanja ya elimu na afya. Huu ndio ukweli na bado inaendelea kufanya hivyo. Na matokeo yake yanaonekana,
tuache historia maana ukianza kusema mambo ya nyerere wengine hatutakuelewa, kwa sasa yeyote anayewekeza vizuri kwenye elimu matunda tunayaona, shule ya feza inaonekana , nadhani ni kati ya shule nzuri kitaifa nayo ni ya waislamu
sasa ponda anachosema ni waislamu kupata vyeo au kuwekeza katika elimu.
Hata kamaviongozi wote wangekuwa waislamu kama mtoto wako hutamsomesha shule nzuri necta haitamchagua bw ponda
matatizo ya watu kama ponda ni elimu ndogo tumsamee bure
 
Kwa ni nani anayetunga mitihani ya Islamic knowlegde na kuandaa marking scheme zake kama si waumini wa dini husika? Likewise Muislamu hawezi kutunga mtihani wa Bible knowledge. Mbona haingii akilini kama kufeli kwa waislamu katika somo linalohusu dini yao kumetokana na Ukristo?
Acheni kulalamikia mambo ambayo yanatokana na ubovu wa management ya shule au taasisi mnazoendesha,mmepewa majengo ya serikali kule Morogoro myatumie kama chuo chenu, mbona wakristo hawalalamiki juu ya hilo? Inavyoonekana hata ile plan ya kujenga vyuo vikuu vya kwenu hamna.Mnategemea nini kama si kulalamika karne kadhaa zijazo?
Hebu ingia kwenye website ya NECTA, cheki perfomance ya shule zifuatazo; Marian girls, St. Francis,St. Joseph Millenium, Maua seminary,na nyingine nyingi zinamilikiwa na makanisa,halafu cheki shule kadhaa zinazomilikiwa na taasisi za kiislamu utaona tofauti. Sasa fikiria miaka 15 ijayo madaktari, watawala,waalimu,wahandisi nk watakuwa akina nani? Ni hawa wanaofanya vizuri sasa na hii si kwa sababu ni wakristu,ni ubora wa elimu inayotolewa na shule husika.
 
Kwa ni nani anayetunga mitihani ya Islamic knowlegde na kuandaa marking scheme zake kama si waumini wa dini husika? Likewise Muislamu hawezi kutunga mtihani wa Bible knowledge. Mbona haingii akilini kama kufeli kwa waislamu katika somo linalohusu dini yao kumetokana na Ukristo?
Acheni kulalamikia mambo ambayo yanatokana na ubovu wa management ya shule au taasisi mnazoendesha,mmepewa majengo ya serikali kule Morogoro myatumie kama chuo chenu, mbona wakristo hawalalamiki juu ya hilo? Inavyoonekana hata ile plan ya kujenga vyuo vikuu vya kwenu hamna.Mnategemea nini kama si kulalamika karne kadhaa zijazo?
Hebu ingia kwenye website ya NECTA, cheki perfomance ya shule zifuatazo; Marian girls, St. Francis,St. Joseph Millenium, Maua seminary,na nyingine nyingi zinamilikiwa na makanisa,halafu cheki shule kadhaa zinazomilikiwa na taasisi za kiislamu utaona tofauti. Sasa fikiria miaka 15 ijayo madaktari, watawala,waalimu,wahandisi nk watakuwa akina nani? Ni hawa wanaofanya vizuri sasa na hii si kwa sababu ni wakristu,ni ubora wa elimu inayotolewa na shule husika.
kwani hasa wanalalamikia nini jamani? waseme basi, kama mitihani wanaongelea mitihani yote au ile ya kiislam tu ambayo naamini waliomark watakuwa waislam wenzao...tatizoo nini hapo hadi kutuletea fujo kwenye kisiwa hiki cha amani?
 
Tunakokwenda sasa ni kubaya. Tatizo hawa wenzetu wamekuwa walalamikaji na si watendaji. Wakati wenzao wakristu wanapanga Mipango inayopangika na kuitekeleza kikamilifu, tena kimya kimya bila kujitangaza kwenye vyombo vya habari, wao wanakazana kupiga fitna na majungu kwenye media, kwamba wanaonewa sana kuliko wote dunia nzima. Badilikeni, fanyeni kazi kwa juhudi. Eboo!
 
udini hawajaunza wao ,aliyeunza ni baba wa ukafiri tanzania mtakatifu julius kambarage nyerere,sema leo watu wameamka na kusema ukweli na makafiri walikuwa hawajajiandaa kusikia ukweli huo either kwa kutokujua au kwa kibli chao.Tutasema mpaka kieleweke
 
Naiasa serikali ichukue haraka hatua za kudhibiti siasa kali za kidini huku bara kama ambazo tayari zimezusha vurugu Zanzibar. Sheikh Ponda na mujahidina wenzake pia wanakusudia kuleta vurugu kama za Zanzibar kwa kisingizio cha NECTA na sensa ya watu na makazi. Nimewaona leo asubuhi CHANNEL TEN katika kipindi cha baragumu ponda na mwenzie simkumbuki jina wakitoka mapovu na alot of unfounded claims.

Kwa kifupi ni watu waliokusudia kuivuruga nchi kwa udini, ninaloweza kuwaambia na nina hakika nalo haitatokea siku nchi hii ikaongozwa kidini kama anavyotaka ponda na wenzie. Tatizo lililopo NECTA kwa mujibu wa waheshimiwa hawa ni uwepo wa katibu mtendaji mkristo na mwenyekiti wa bodi mkristo, lakini waziri wa elimu na katibu mkuu wake kuwa waislamu si tatizo hata kidogo.

Dini zetu zinakuwa na maana na manufaa kwa waumini wake na taifa kwa ujumla kama zinajishughulisha na masuala ya maendeleo ya kijamii ya waumini wake. Kama dhehebu linafumbia macho masuala ya elimu na afya za wafuasi wake ni wazi litakumbwa na matatizo, mi mwislamu lakini sisiti na siogopi kuwasifia wenzetu wakristo na hasa wakatoliki kwa jinsi wanavyowekeza katika masuala ya afya na elimu kwa kujenga hospitali na shule na vyuo kadha wa kadha. Sisi tuna chuo kikuu kimoja tu na si cha kujenga wenyewe bali kupewa bure na serikali wenzetu wamejenga wenyewe vyuo takribani kumi, ni vipi tunataka tufanane na watu kama hao? Angalia uendeshaji wa shule zao mfano Kifungilo, marian, St Francis hivi kweli unaweza linganisha na uendeshaji wa Kinondoni muslim, haramain au jumuiya? Waislamu wenzangu tunaokitakia mema kizazi chetu tupeleke wanetu kwenye shule za kweli zenye walimu,vifaa na usimamizi wa kutosha bila kujali wamiliki wake ni wa ibada gani.

Tuwaandalie wanetu mazingira mazuri ya ushindani hapo baadaye kwa kuwapa elimu bora. Mwenzie Ponda anadai eti hospitali za kikristu zinabagua, katoa mfano wa KCMC kuwa mgonjwa ukifika unaaulizwa unatoka usharika gani, uongo wa mwaka huu. Mzee wangu kalazwa zaidi ya mara tatu hospitali hiyo na kupatiwa huduma nzuri sana za upasuaji wa kibofu na hata mara moja hakuwahi kuulizwa dini yake.

Mtu anayejiita kiongozi wa kidini kutoa madai ya uongo kama haya anajifedhehesha binafsi ambalo si jambo baya sana bali anafedhehesha dhehebu analojidai kulipigania.
Eti wanadai waislam wasusie sensa kwa kuwa hakuna kipengele cha dini ya mtu,what a nonsense and hypocricy!!!!!! hivi kipengele hicho kina maana gani kuwepo na kiukweli kama kingekuwepo anadhani wa kwanza kuandamana kukipinga ni akina nani kama sio huyo ponda na wanafiki wengine??? kipengele hicho hakikuwekwa kukwepa shari za ponda na wengine wenye mtizamo kama wake...aache kujishauaaaaaaaaaaaaaaaa!!! ghrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrh!!!!
 
[h=2]Waislam: Watoto wetu wanafelishwa[/h]Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania imecharuka na kueleza kuwa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta) limekuwa likifelisha wanafunzi wa imani ya dini hiyo.

Jumuiya na taasisi hizo zimemtuhumu Katibu Mtendaji wa Necta, Joyce Ndalichako na watendaji wengine wa baraza hilo kwa madai kuwa wamekuwa wakihujumu matokeo ya mitihani ya wanafunzi wa Kiislamu.

Aidha, wamelaani vikali uvunjaji wa heshima kwa kuchoma moto makanisa wakati wa vurugu zilizotokea visiwani Zanzibar ambapo zimeitaka serikali kuunda tume huru kutoka pande zote makanisa, serikali na kikundi cha Uamsho ili kuwapata waliohusika na uhalifu huo.

Kauli hiyo imetolewa jana kwenye mkutano wa kuzindua waraka wa maoni ya Waislamu katika mchakato wa katiba mpya uliowashirikisha Waislamu wa jiji la Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Baraza Kuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ramadhani Sanza, akizungumza katika mkutano huo alisema kila mwaka wanafunzi wa Kiislamu wamekuwa na matokeo mabaya hali inayotia mashaka kwamba yanachakachuliwa na Necta.

"Ufaulu mkubwa umekuwa ni kwa wanafunzi wa Kikristo huku wa Kiislamu wakionekana kufanya vibaya, tunajua huo ni mpango maalum unaofanywa na Necta wa kuwadidimiza kitaalum watoto wa Kiislamu na uislamu kwa ujumla," alisema Sanza.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Kiislamu Tanzania, Shabani Mapeyo, alisema Waislamu wanalaami vikali kuchoma moto makanisa wakati wa vurugu zilizotokea visiwani Zanzibar ambapo wameitaka serikali kuunda tume huru kutoka pande zote makanisa, serikali na kikundi cha Uamsho ili kuwapata waliohusika na uhalifu huo.

Mapeyo alisema kila upande uliohusika na kadhia hiyo kwa maana ya Wakristo, Waislamu na Serikali ushushe munkari na badala yake busara itumike ili kumpata muhusika wa uhalifu huo.

Mapeyo alisema atakayebainika kuhusika na jambo hilo achukuliwe hatua kali bila ya kujali wadhifa wake iwe katika chama, dini ama serikali.

"Fitina iliyopandikizwa baina ya Wakristo na Waislamu, Watanzania Bara na Wazanzibar zisipoangaliwa kwa umakini zinaweza kuvuka mipaka na kuenea nchi nzima na kuharibu hali ya nchi, hivyo ndugu zangu Waislamu tuwe makini tusije tukachokozwa na tukaingia katika vurugu hizo kirahisi," alisema Mapeyo.

Naye Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda, akizungumzia suala la sensa, alitaka iundwe tume huru ambayo inawashirikisha Waislamu na Wakristo kabla ya Juni 20 mwaka huu.

NIPASHE ilimtafuta Dk. Ndalichako juu ya madai hayo, alisema angezungumza na mwandishi wa habari hizi leo. CHANZO: NIPASHE
Nimewakumbuka sana wale manafunzi wa form vi ndanda waliogoma kufanya mitihani pamoja na juhudi kubwa za naibu waziri wa elimu kuwahimiza wafanye mtihani huo...wenyewe waliona kulala msikitini ni dili...
 
Mimi ni mkristo lakini jina langu la kiislam. Nilifaulu sehemu zote na kazi ninayo na jina hilohilo la kiislamu. Ubaguzi wa dini ktk elimu tanzania hakuna.
Mheshimuni yule katibu wa baraza, siyo joyce ndalichako, ni doktor joyce ndalichako.

huo ni udaktari wa kutibu wanyama? au ni ule wa Falsafa(PhD) wanaotunukiwa watu kila kukicha?
 
Mohamed Said
wachangiaji wengi wamekushambulia kwasababu unaleta reference za uongo na uchochezi. Jifunze kuwa mkweli.

Mwembechai killing 1998
rais-Ally Hassan Mwinyi
Makam- Omar Juma
Igp- Omar Mahita

nyerere anaigiaje hapo?
Huyo professor wako atakuwa wa divinity, haya ndiyo madhara ya elimu ya kupeana unafiki tu.
 
Kwa nn ni Muhimu kujua Imani zetu,taarifa hiyo itatusaidia vp Kupanga Maendeleo?
Tukijua Wakristo ni Wengi kuliko Waislamu inatusaidia nn? Kwamba kundi godo liongeze juhudi ya Kuzaa?

Masikini wee basi mantiki sahihi ya sensa huijui. Nenda kwenye website ya waroma utakuta idadi ya watanzania kwa mujibu wa imani zao kisha urudi uniambie kama umeelewa au la.
 
Mohamed Said,

Deep down your heart, do you believe waislamu wanaonewa wasiweze kusoma? Kama una evidence kama hizo, na siyo here say this here say that, zilete jamvini. Tukianza kuendesha mambo yetu kwa kuhadithiwa tu tunaweza kabisa kufanya makosa makubwa kwenye maamuzi yetu. Tulianza kuleta chokochoko kwenye utaifa wetu, hakuna atakayesalimika maana ndivyo hovyo tulivyo.

Umaskini kweli ni kitu kibaya sana na kama hatujui namna ya kupigana na umaskini, ndiyo haya malalamiko yasiyokwisha.

Naamini katika maisha yangu nimekutana na watu wengi wema na ninawaheshimu sana ambao sio wa dini wala imani yangu. Ntafanya makosa kuchukia kila mtu wakati wenye kutuletea matatizo ni watu wachache tu.
Mkuu Ndahani, huyo mzee Mohamed Saidi na kundi lake ni watu hatari sana katika jamii ya wapenda amani ni mtu wa kupuuzwa kabisa, kwa umri wake mkubwa alipaswa kuwajengea vijana wa kiislam kujiamini na kusonga mbele kujisomea nakujiletea maarifa na sio kuanza kunung'unika kwamba wanaonewa na wakristo.
 
na walipobanwa sana kuhusu UONGO waliosema kuhusu KCMC kutibu watu kwa udini wakabaki wanang'atang'ata maneno, wallikua hawajui kuwa kuna wanaJF wanasikiliza kipindi, tumewachapa maswali wakalamba matapishi
 
Usimwamushe alie lala ukimwamusha utalala wewe, wakati wao wanpiga kelele za uzushi wenyeakili wanafanya mambo
 
Mkuu Ndahani, huyo mzee Mohamed Saidi na kundi lake ni watu hatari sana katika jamii ya wapenda amani ni mtu wa kupuuzwa kabisa, kwa umri wake mkubwa alipaswa kuwajengea vijana wa kiislam kujiamini na kusonga mbele kujisomea nakujiletea maarifa na sio kuanza kunung'unika kwamba wanaonewa na wakristo.

Bwana Gwalihenzi na tuanze na hii:

Tafadhali soma kipande hiki kutoka kitabu cha Prof. Hamza Mustafa Njozi, "Mwembechai Killings..."

"In 1987 the then Minister for Education and Culture the late Professor Kighoma Malima discovered that deserving Muslim candidates were deliberately being denied access to secondary education.(It is curious to note that throughout his 25 - year rule, Nyerere had always appointed a Christian to head the Ministry of Education and a Muslim to head the Ministry of Home Affairs.)

The trick used by the Christian dominated panel was to select the candidates after decoding their examination numbers. Professor Malima directed the panel to select and announce the results using examination numbers only. In that year the percentage of selected Muslim candidates rose by 40 per cent! He alerted the president about the matter and suggested a thorough investigation be carried out. He was branded "Mujahidina" and removed from that portfolio and the selection panel reverted to its old system. He repeated those charges at a public rally in Dar es Salaam in 1995. Any government which is "fiercely secular" would certainly wish to know the truth of the matter.

Apparently there was no need for the government to investigate the obvious. On July 7, 1999 Muslim leaders paid a courtesy call to President Mkapa at the State House in Dar es Salaam. In the course of their informal discussions Muslims raised the issue of decoding examination numbers. According to my informant the president was clearly surprised. When he asked his Minister for Education and Culture who also attended the talks, the minister confirmed the Muslims' account. As a result one of the numerous but supposed "isolated" cases came to light in January 1999.

A Muslim candidate one Adam Ramadhani Kindenge of Gilman Rutihinda primary school was not selected. His father disputed the fairness of the selection process and demanded to be shown the scripts. It was an embarrassing case. Christian candidates with lower points were selected and Adam who had higher points was left out. No one in the ministry could hazard an explanation. The case was disconcerting in view of Kitwana Kondo's question in Parliament. But it was a case which like others in the past the ministry managed to suppress. For details see Ramadhani Kindenge's two letters to the Ministry of Education and Culture (1999).

Despite protests from Muslims, the same ministry had also successfully managed to hide from many unsuspecting Tanzanians another discomfiting letter bearing Ref. No. E10/MMC-1/183 of 9 June, 1998 from the Morogoro Municipal Education Officer directing all Headteachers to submit to that office the names of all Standard Seven Catholic students! When a weekly Muslim newspaper An-Nuur confronted the ministry with that letter the spokesperson was too embarrassed to comment. He promised however to investigate the matter. A time-tested device of dropping a hot potato!

Adam Kindenge's case above is not an isolated one. Muslims have a long list of such cases. The name of a selected Muslim candidate, Kopa Abdallah of Kichangani primary school, in Kilosa was in 1983 unfairly cancelled out in favour of a Christian, Mr. Anthony Samirani who scored less points. Mr. Kopa is today employed as a driver. Was it merely a case of corruption? In his long career as a Secondary School Headmaster and later as a high ranking civil servant, Mr. Bori Lilla was twice confronted with incredible discoveries of religious discrimination in the country. Mr. Bori Lilla is today one of the highly respected Muslim elders in the country and is affectionately referred to as "Mzee Lilla".

He told me and he has repeated this account to many others that he was once in the marking and selection committee and was mistaken for a Christian. After marking the scripts he decoded and recorded the names according to their pass marks, and there were as many Muslims as there were Christians. A fellow panelist who was a Christian saw the list and was very furious, he said in a loud voice, "Wewe huoni kama orodha yako ina Waislamu wengi sana, au wewe ni mgeni nini hapa?" (Don't you see that your list has so many Muslims, or could it be that you are a new comer here?). Mzee Lilla says that he responded in an equally loud voice, "Mimi siyo mgeni, mimi ni Muislamu". The room was gripped with an eerie silence.

Mzee Lilla witnessed the second revelation of deliberate religious discrimination when he was in the selection panel for allocating High School places for deserving Ordinary Level candidates. It was during the Islamic holy month of Ramadhan and they had almost finished their task when Christian panelists broke for lunch. The panel had only two Muslims who stayed behind. The other Muslim panelist, Mr. Abdulrahman Mwalongo, was writing something and needed a ruler which was in the Chairperson's draw.

When he opened it he found along with the ruler, a list of 25 First class Muslim candidates who had not yet been allocated any place in High Schools while all their Christian counterparts had already been placed. And the panel's chairperson who was also a Reverend had not even hinted that there was such a list. Mwalongo is from the Hehe ethnic group. And the Hehe are known in Tanzania as fierce warriors. When their colleagues returned, Mwalongo reminded the chairperson about the list in his draw. He brushed aside Mwalongo's concern saying that those candidates would be taken care of later.

Quite unexpectedly,Mwalongo banged his table so forcefully that all members were taken aback. Shaking with rage Mwalongo told the chairperson no business would take place in that room before the allocation of the 25 Muslim students. The chairperson backed down and those students were placed. In July 1997 I cross-checked Mzee Lilla's account with Mwalongo himself. He confirmed the story. As I am writing this book, both of them are still alive and can easily be contacted for further details."

Baada ya kuonekana ukweli huu katika kitabu serikali ya Benjamin Mkapa ilikipiga marufuku.
 
Kwanza nimshukuru sana sheikh PONDA,kwa kuwafikishia ujumbe hao MAKAFIRI wa NECTA kwa kutufelisha kwa makusudi ktk somo la dini yetu tu...... kwani hii inadhihirisha wazi kuwa WAKRISTO ndio vinara wa kuleta UDINI na ndio maana mnatunyima elima......namaliza kwa kusema kuwa sisi WAISLAM tutaendelea kudai haki zetu mpaka kieleweke na pia tunakualikeni ktk maandamano siku ya ijumaa.......thanks
 
Mohamed Said
wachangiaji wengi wamekushambulia kwasababu unaleta reference za uongo na uchochezi. Jifunze kuwa mkweli.

Mwembechai killing 1998
rais-Ally Hassan Mwinyi
Makam- Omar Juma
Igp- Omar Mahita

nyerere anaigiaje hapo?
Huyo professor wako atakuwa wa divinity, haya ndiyo madhara ya elimu ya kupeana unafiki tu.

Bwana Adolay,

Hii debate yaweza ikawa nzuri sana ikiwa tu tutajituliza na kuzungumza kistaarabu.

Hakika Ally Hassan Mwinyi alikuwa rais na hao wote walikuwapo ila sioni vipi wanaingia katika hili.

Kuhusu Nyerere.
Huyu ataihitaji tufanye debate yake peke yake.
Nimeandika kitabu kizima na Nyerere anaongoza katika farahasha (index) yangu.

Prof. Njozi ni wa literature.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom