Serikali nzima kitanzini!

Yani ukipiga mahesabu ya haraka haraka ya hela zinazo potea kwa rushwa nadhani unaweza jiuliza Tanzania ni masikini kwa hesabu zipi.
 
Yani ukipiga mahesabu ya haraka haraka ya hela zinazo potea kwa rushwa nadhani unaweza jiuliza Tanzania ni masikini kwa hesabu zipi.

Nchi yetu si maskini Mkuu bali tuna "Viongozi" (huwa nasikia vibaya sana kuwaita Viongozi) ambao ni mafisadi ambao wanahamishia utajiri wote wa nchi yetu mifukoni mwao. Wale wote wanaojiita ni Viongozi na ambao wamewahi kushika nafasi za juu kabisa za uongozi ndani ya nchi yetu hawakuwa mabilionea miaka michache tu iliyopita lakini leo hii baada ya ufisadi mkubwa waliofanya kuhusu Rada, Richmond/Dowans, Ndege ya Rais, Helicopters na magari ya jeshi, Kiwira Coal Mining, NBC, Mikataba ya madini, EPA, Meremeta, Kagoda n.k. wengi wao ni matajiri wakubwa sana na wana assets nyingi sana ndani na nje ya nchi. Unaona hata Wabunge wanachukua chao mapema inabidi kila Wizara katika kipindi cha bajeti itenge "bulungutu" la karibu shilingi bilioni moja ili kuhakikisha tu bajeti zao zinapitishwa na "waheshimiwa" Wabunge.
 
Back
Top Bottom