Serikali ni mali ya watu, na watu ni mali ya Mungu

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,928
3,225
EE ndio habari ndio hiyo!!

Serikali ni mali ya watu wa hiyo nchi wanamoishi. Na Watu wameumbwa na Mungu.

Watu wanalelewa kiroho na DIni zao. Dini ni Daraja kati ya Mungu na watu.

Na watu ndo walioiweka serikali madarakani kupitia chama fulani. Kwa hiyo Chama na serikali hawana mamlaka au uwezo wa kukemea Dini wasitoe waraka.

Pili Serikali Au tuseme chama kimeonyesha udhaifu na waraka umeonyesha mahali udhaifu ulipo.
Mtu akijamba inatakiwa aambiwe umejamba. Huyo aliyejamba ajiangalie labda kuna mavi anatakiwa akanye.

Au Mtu kajinyea na ananuka, kwa nini asiambiwe akajitawaze?

Mawaziri na wabunge hasa wa chama tawala wamekuwa wafalme na watanzania walio wengi (95%) ni watumwa. Hawa wafalme wajejitwalia haki zote.

Tanzania hakuna uhuru wala Amani. Ni Bora kipindi cha ukoloni kuliko Utumwa.

Kwa hiyo wacha Maaskofu na Waislam waelimishe Wafuasi wao ili wajue haki zao na wajikomboe kupitia sanduku la kura 2010.

Karibuni
 
Back
Top Bottom