Serikali na Hatima ya ATCL

Awali ya yote mwandishi awatendee haki baadhi ya wajumbe wa kamati ambao hawakutambulishwa kwa jamii kwa hadhi zao kitaaluma. Ninavyofahamu mimi Marcelina Chijoriga na Mussa Assad ni ma-Dk. pia waliobobea kwenye fani za biashara na uhasibu. Kwanini wengine mf. Dk. Ibrahim Juma, Dk. Gideon Kaunda, na Dk. Hamis Kibola wametambulishwa kwa U-Dk na wengine siyo? Anyway, hilo ni jambo dogo lakini lina umuhimu wake katika uchambuzi wa mambo ili kujua uzito na uwezo wa wanatume dhidi ya kazi waliyopewa na waziri. Pili, tunaomba kamati iliyoteuliwa itutendee haki watanzania. Watumie taaluma zao, busara zao na uzalendo wao kutupatia ripoti yenye mshiko itakayomfanya waziri na wizara husika kufikia maamuzi ya maana kwa shirika letu la ndege. Matatizo ya shirika hili yamepigiwa mayowe mwaka mzima kabla ya huduma zake kufungwa rasmi mwishoni mwa mwaka jana. Menejimenti iliyopo iliyajua matatizo hao yaliyokuwa yanapigiwa makelele lakini hatukuona dalili zozote za jitihada za makusudi za kulinusuru shirika hili zaidi ya ufisadi wa kununua mashangingi zaidi kwa mkopo wa Stanbic bank ili menejimenti iendelee kutanua mtaani huku shirika linadidimia polepole. Tume iliyoundwa itutendee haki. Isimfumbie macho kiongozi yeyote katika menejimenti. Ituletee ripoti iliyoenda shule. Tunatumaini wao wana tume wameenda shule, tunatarajia ripoti iliyoenda shule kama ile ya Dk. Mwakyembe. Imefika wakati tuiokoe nchi yetu badala ya kulindana kijinga. Tutatungulize uzalendo kwa taifa na maendeleo yake.
 
Awali ya yote mwandishi awatendee haki baadhi ya wajumbe wa kamati ambao hawakutambulishwa kwa jamii kwa hadhi zao kitaaluma. Ninavyofahamu mimi Marcelina Chijoriga na Mussa Assad ni ma-Dk. pia waliobobea kwenye fani za biashara na uhasibu. Kwanini wengine mf. Dk. Ibrahim Juma, Dk. Gideon Kaunda, na Dk. Hamis Kibola wametambulishwa kwa U-Dk na wengine siyo? Anyway, hilo ni jambo dogo lakini lina umuhimu wake katika uchambuzi wa mambo ili kujua uzito na uwezo wa wanatume dhidi ya kazi waliyopewa na waziri. Pili, tunaomba kamati iliyoteuliwa itutendee haki watanzania. Watumie taaluma zao, busara zao na uzalendo wao kutupatia ripoti yenye mshiko itakayomfanya waziri na wizara husika kufikia maamuzi ya maana kwa shirika letu la ndege. Matatizo ya shirika hili yamepigiwa mayowe mwaka mzima kabla ya huduma zake kufungwa rasmi mwishoni mwa mwaka jana. Menejimenti iliyopo iliyajua matatizo hao yaliyokuwa yanapigiwa makelele lakini hatukuona dalili zozote za jitihada za makusudi za kulinusuru shirika hili zaidi ya ufisadi wa kununua mashangingi zaidi kwa mkopo wa Stanbic bank ili menejimenti iendelee kutanua mtaani huku shirika linadidimia polepole. Tume iliyoundwa itutendee haki. Isimfumbie macho kiongozi yeyote katika menejimenti. Ituletee ripoti iliyoenda shule. Tunatumaini wao wana tume wameenda shule, tunatarajia ripoti iliyoenda shule kama ile ya Dk. Mwakyembe. Imefika wakati tuiokoe nchi yetu badala ya kulindana kijinga. Tutatungulize uzalendo kwa taifa na maendeleo yake.

Una maana tume zote zilizopita zilizoshindwa kufanya kazi vizuri ni kwa sababu wajumbe wake walikuwa hawajasoma? Au una maana tume zote zilizokuwa na wajumbe wasomi zimefanya kazi vizuri? Ripoti iliyoandialiwa na tume ya mwakyembe ambayo unaiita imeenda shule, unadhani iliandaliwa na ma-dk kama wewe unavyodhani? Unafahamu maana ya to "be schooled" na "to be educated". Kwenda shule ni sehemu ndogo tu inayomfanya mtu awe na uwezo wa kufanya kazi vizuri. Mbona tuna wasomi wengi wezi tu na wanafanya kazi zisizoenda shule, na mbona kuna wasio wasomi wanafanya kazi nzuri zilizoenda shule. Au unataka kusema nini mkuu?
 
Una maana tume zote zilizopita zilizoshindwa kufanya kazi vizuri ni kwa sababu wajumbe wake walikuwa hawajasoma? Au una maana tume zote zilizokuwa na wajumbe wasomi zimefanya kazi vizuri? Ripoti iliyoandialiwa na tume ya mwakyembe ambayo unaiita imeenda shule, unadhani iliandaliwa na ma-dk kama wewe unavyodhani? Unafahamu maana ya to "be schooled" na "to be educated". Kwenda shule ni sehemu ndogo tu inayomfanya mtu awe na uwezo wa kufanya kazi vizuri. Mbona tuna wasomi wengi wezi tu na wanafanya kazi zisizoenda shule, na mbona kuna wasio wasomi wanafanya kazi nzuri zilizoenda shule. Au unataka kusema nini mkuu?

Mkuu Bongolander asante kwa maoni yako. Kwamba nina maana gani tayari limeshajibiwa kwenye post yenyewe niliyoibandika. Ungesoma kwa nia ya kuelewa ungepata majibu ndani ya post yenyewe. Walau sentensi ya mwisho tu inakupa jibu. Ni hii hapa "Tutatungulize uzalendo kwa taifa na maendeleo yake.". Mkuu, hawa jamaa wanadaiwa kutoa ripoti ya uchunguzi wao. Hii ni karne nyingine, hivyo ripoti upende usipende lazima iandaliwe kisayansi. Hapo ndipo kunapokuja phrase "iliyoenda shule". Siyo barua ya mjukuu kwenda kwa babu. Wataalamu wetu hawa ni ma-Dk na tunaamini kipengele hicho kitathaminiwa. Lakini, la pili, ni kuwa uchunguzi wowote unahitaji mbinu na uwezo wa kuchanganua mambo kimantiki. Hapo pia utaalamu husika unahitajika. Ndiyo maana waziri ameteua watu anaodhani wana uwezo huo ili watuletee ripoti "iliyoenda shule". Kumbuka ripoti hizi zitahifadhiwa, tunataka kuhifadhi kwenye kumbukumbu kitu "kilichoenda shule". Udokta ni kivumishi tu, haina maana kuwa mwenye PhD pekee ndiye mwenye uwezo huo, la hasha. Yeyote mwenye profession yake anaweza kuyafanya haya. Lakini hawa walioteuliwa wana PhD, hivyo nimetumia maneno ya "kwenda shule" ili iwe angalisho tangu mapema kuwa tunawadai zaidi katika ripoti yao. Tatu, ni ukweli kuwa wanaweza kutuletea ripoti "iliyenda shule"lakini ni ya uongo kwa lengo la kulindana. Hapo ndipo nikatoa angalisho kuwa "Tutatungulize uzalendo kwa taifa na maendeleo yake.". Kama umesoma vizuri post yangu utaona mahali nimesema "mtutendee haki watanzania". Sasa wakitoa ripoti ya uongo maana yake "hawajaelimika"pamoja na kuwa na kiwango cha juu cha taaluma katika level ya PhD. Hapo "shule" haitakuwa imewasaidia, yaani watakuwa bado "hawajaelimika". Mtu aliyeelimika anaitumia shule kwa ajili ya kuleta maendeleo, kukuza utu wake mbele ya jamii na heshima. Wote waliowatangulia iwapo walitoa ripoti zilizo "enda shule" lakini za uongo basi "hawajaelimika", au elimu yao haina maana kwa jamii. Unajua, unapotaka mtu akufanyie kazi nzuri unayoitarajia, basi kwanza tanguliza kumuonyesha kuwa unamjali, unaitambua taaluma yake au uwezo wake nk. ili kumjenga kisaikolojia na kumwaminisha kuwa unategemea makubwa toka kwake. Naye atajitahidi kukuletea kazi nzuri. Hiko ndicho kilichofanyika kwenye post yangu. Sina maana kuwa u-dk wao ni jibu la kila kitu na kuwa wengine wote kwenye kamati nyingine ni wapuuzi kwa kuwa hawakuwa na u-dk. Sina maana hiyo hata kidogo. Ni kwa misingi hii nimeitaja ripoti ya Dk. Mwakyembe kuwa imeenda "shule" kwasababu imetanguliza maslahi ya taifa mbele, na wala si kwasababu wajumbe wake wote wana PhD. Natambua wengine hawakuwa na PhD, lakini walikuwa na profession zao muhimu, na wamezitumia vyema kwa kutanguliza maendeleo ya taifa. Ni vema kusoma "post"kwa umakini mkuu.
 
Ninachojua ATCL ni shirika la umma sawa na mashirika mengine ya umma, linapaswa kuwa chini ya kamishna wa mashirika ya umma aliyeko wizara ya fedha na mmiliki wa mashirika ya umma ni TR ndiye anayejua hisa za serikali na uendeshaji wake kwa kila shirika.

Sasa hii Dr.Shukuru kuonekana ndio mdhibiti wa ATCL hapo ndo kuna matatizo. Nilitegemea CAG akisaidiwa na consulting firm atakayoona inafaa ndo wangefanya kazi ya ku-evalute worthness ya ATCL and new way forward. Tukumbuke 100% shares za ATCL ni za serikali. Hivyo TR na CAG wana dhamana ya kulinda rasilimali hii kwa niaba ya watanzania wote.

Tuiangalie hii kamati! ukiondoa Mtesigwa Maugo sidhani kama kuna mwingine anaejua chochote kuhusu biashara ya Airlines. huyu profesa wa mipango miji sijui mchango wake utakuwaje katika hii kamati!
 
Sikubaliani na Dr.Shukuru kuwa management ya ATCL ikikaa pembeni shirika lisingeenda. Ingekuwa jambo la busara kama Mattaka na Nyangányi wangekaa pembeni na management mpya ya muda ingeteuliwa. Kazi hiyo ilifanyika NMB, CRDB, NBC na mpaka sasa mashirika hayo yanajiendesha kwa faida kubwa.

Tatizo la ATCL sio human capital wala working capital! ni corporate management. Hivi unahitaji kuwa na knowledge gani kujua kuwa management yenye ndege 3 ina staff 300 na vx 6 makao makuu kuwa hiyo management haifai!

unahitaji knowledge gani kuona management inayokodi ndege ambayo haina wataalamu wake kuwa haifai! unahitaji knowledge gani kujua kuwa mtaji wa 17.5bn umeisha kwa miaka miwili tu! Hivi hatukujifunza kutoka Egle Air, Air Express, Community Airline?

Tuliwahi mshauri Diallo hapa JF juu ya Community Airline tukaonekana wapika majungu! sasa kafuata ushauri wetu ameleta ndege moja ya abiria 6 na nyingine ya abiria 10 zinafanya safari za mwanza - bukoba na Dar - Zanj.
 
Mheshimiwa kawambwa nakuomba kwa heshima na taadhima wasilisha kwenye baraza la mawaziri hoja ya kuivunja atcl. Ebu tuondolee watanzania mzigo huu tunaoubeba bila sababu na kwa maslahi ya watu wachache
 
PriceCoopers imepeleka wafanyakazi ATCL akiongozwa na Mkuu wa idara ya fedha, mkuu wa ukaguzi ndani, hivyo hawa watendaji wakuu wamekuwa kwa muda mrefu wanapeleka kazi kwa mwajiri wao wa zamani. Hou ni Eliasaf Methew, William Haji (kaondoka) na dada wa kichaga binti Lyimo wa Kimara.

Kuna rushwa tupu inanuka ATCL katika mambo ya procurement.
 
Mkiwapeleka majina yao for confirmation huko bungeni watapitishwa tu kwani hao wabunge wenyewe nao siwamekubuhu kwa mshiko ndio maana hawataki kuachia boards za mashirika ingawa serikali yao inasema it is agaist good governance. Akiteuwa muungwana wabunge wa ccm watamconfirm bila wasi wasi, si mliona wakati wa uchaguzi wao wa wajumbe wa NEC wengine walichaguliwa wakiwa wagonjwa wamelazwa hospitalini lakini muungwana aliwafanyia kampeni kiainaaina wakachaguluwa kuwa wajumbe in absentia!!! CCM na serikali yake kama wasemavyo wao, INA WENYEWE!!
 
Pundamili07,
Yote uliyoandika ni PUMBA. Wewe si serikali. Serikali inajua ukweli wote wa hili sakata ndiyo maana imekaa kimya baada ya kupokea report ya uongozi wa ATC! Resonse ya serikali nadhani umeishaisikia kutoka kwa waziri wako mhusika kukiri kuwa ATC Haikupewa mtaji kama serikali ilivyoahidi na haikulipa madeni yalioachwa na SOUTH AFRICA ambapo imesababbisha kasheshe na mabenki yaliyowakopesha. Sijui mwenzangu wewe unasikiliza redio mbao au hata TV huna???? Hata kama unataka kuuza nyanya lazima uinvest hela ili utengeneze pesa. TUNAZUNGUMZIA MTAJI WA KUENDESHA SHIRIKA MATAKA NA NYANGANYI WALILOKABIDHIWA BILA HATA NDEGE MOJA KUWA ANGANI. WHAT THE HELL ARE YOU TALKING ABOUT, REJEA HOTUBA ZA BAJETI WAKATI NYANGANYI AKIWA WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI NA UTAFUTE KIPENGELE KILICHOSEMA KUWA MASHIRIKA YALIYOCHINI YAKE YALIKUWA YAKIENDESHWA KWA HASARA. YOU NEED TO GO BACK TO SCHOOL AND LEARN HOW TO PUT YOUR FACTS TOGETHER MEN! KAMA UNAJIFANYA MJUAJI SANA UNGEJUA NANI KALIFILISI HILI SHIRIKA!!!!
 
The government has injected 2.5bn/- into the crisis-ridden Air Tanzania Company Limited (ATCL) a



ATCL management earlier submitted application worth 3.3bn/-to put it back on track. But the Company’s Board Chairman, Mr Mustapha Nyang’anyi, has been quoted as saying about 92bn/- was needed to revamp operations of ATCL. T




On ATCL’s debts, Dr Kawambwa said it owes South African Airways (SAA) $4.2m, various service providers and suppliers 9.1bn/- and the government about 17.5bn/-. But he explained that the government’s debts had been transferred as capital of the company.

This math doesnt add up!! Whats the point of wasting more money on this things if they are just delaying its death??
 
Pundamili07,
Yote uliyoandika ni PUMBA. Wewe si serikali. Serikali inajua ukweli wote wa hili sakata ndiyo maana imekaa kimya baada ya kupokea report ya uongozi wa ATC! Resonse ya serikali nadhani umeishaisikia kutoka kwa waziri wako mhusika kukiri kuwa ATC Haikupewa mtaji kama serikali ilivyoahidi na haikulipa madeni yalioachwa na SOUTH AFRICA ambapo imesababbisha kasheshe na mabenki yaliyowakopesha. Sijui mwenzangu wewe unasikiliza redio mbao au hata TV huna???? Hata kama unataka kuuza nyanya lazima uinvest hela ili utengeneze pesa. TUNAZUNGUMZIA MTAJI WA KUENDESHA SHIRIKA MATAKA NA NYANGANYI WALILOKABIDHIWA BILA HATA NDEGE MOJA KUWA ANGANI. WHAT THE HELL ARE YOU TALKING ABOUT, REJEA HOTUBA ZA BAJETI WAKATI NYANGANYI AKIWA WAZIRI WA MAWASILIANO NA UCHUKUZI NA UTAFUTE KIPENGELE KILICHOSEMA KUWA MASHIRIKA YALIYOCHINI YAKE YALIKUWA YAKIENDESHWA KWA HASARA. YOU NEED TO GO BACK TO SCHOOL AND LEARN HOW TO PUT YOUR FACTS TOGETHER MEN! KAMA UNAJIFANYA MJUAJI SANA UNGEJUA NANI KALIFILISI HILI SHIRIKA!!!!

I agree with you kuwa ninaweza kuandika yale ambayo hutaki kuyasikia masikioni mwako. Lakini kwa vile hili jukwaa ni jukwaa huru kwa yeyote kutoa views zake kwa kadri ya vile anavyoona na kujiamini nitaendelea kufanya hivyo.

Nilichokifanya ni kutoa ushauri na maangalizo juu ya ATCL, sasa kama wewe unao ushauri mbadala basi utoe hapa ili ATCL iweze kufaidika na hatimaye watanzania wote.

Kulalamikia maoni yangu bila ya kuja na mbadala wake haitosaidia chochote na wala haiwezi kugeuza what I wrote.

Lete hoja na wala si maneno matupu, maneno matupu hayavunji mfupa

Kama nimesema Bodi na Management vinapaswa kuondoka na kuwa timu ya mpito hilo ni wazo langu basing on the facts I have shown. Najua kuwa it pains hasa pale wanaoguswa labda ni maswahiba wako, I am sorry I can't help, tuna mkoma nyani mchana kweupeeee!!!!
 
WATUELEZE HUYU ALIKUWA KAMA NANI HUKO MAREKANI NA NANI ALIKUWA ANAMLIPA MSHAHARA???\\Dear All,First of all I would like to introduce myself, I willbe your Resident CustomerSupport Manager on site for your Airline, my name isRicardo M. Galhardo.Please be advise that this email is the Air Tanzaniamail account for you to provideme with all issues that you might have day by day,this mail box is open 24/7, forthe time been I have only one contact that is at yourdisposal also 24/7 and is hasfollows: +351 969025814.Please be free to contact me if you have any issue anyquery at all.If you would be so kind to provide the email accountand mobile to any persons inthe company if needed for any issue concerning Airbus.For the time been this is all that I can say, it willbe very gratifying for me tosee and meet everybody personally when I arrive inTanzania.Thanks for your understanding and comprehension,Best regards,Ricardo GalhardoResident Customer Support Manager
 
Source Nipashe

Hii ndo Tanzania zaidi ya uijuavyo usanii mtupu na kama hakuna uzalishaji wafanyakazi wanalipwa na nini? Hivi nchi hii watanganyika hapa napo mpaka katiba mpya ndo tuanue haya kweli?
 
Source Nipashe

Hii ndo Tanzania zaidi ya uijuavyo usanii mtupu
Wananua leo? Mbona umewahi kukaa miaka takribani mitatu ikiwa haina ndege inayoruka lakini wafanyakazi kibao wakiwa wanalipwa wakiwemo wakurugenzi lukuki!
 
Wananua leo? Mbona umewahi kukaa miaka takribani mitatu ikiwa haina ndege inayoruka lakini wafanyakazi kibao wakiwa wanalipwa wakiwemo wakurugenzi lukuki!

Nchi letu la wajinga limejaa wapumb..v linaongozwa na wapumb..v! kazi tunayo. MAGAMBAS hawana uwezo wa kututoa hapa tulipo!
 
Mbona haya mashirika ya Tanzania kichefuchefu? Waziri nundu yuko wapi apigwe maswali kama ya Waziri Fedha jana bungeni?
 
WELCOME TO AIR TANZANIA
Good morning, Ladies and Gentlemen. This is yr captain MAFURU. On behalf of Air Tanzania Ltd, I’m welcoming both seated and standing passengers on board of Air Tanzania Boeing 767. We apologize for the six-hour delay in taking off, it was due to bad weather and some bad traffic from Tegeta to the Airport, Dala Dala’s are all full in the morning hours and traffic not moving. This is flight 712 From Dar es Salaam to Mwanza. Landing there is not guaranteed, but we will end up somewhere in the Lake Zone. And, if luck is in our favor, we may even be landing on your village!
Air Tanzania has an excellent safety-record. In fact, our safety standards are so high, that even pick-pockets, snatchers and bandits are afraid to fly with us!
It is with pleasure; I announce that, starting this year, over 30% of our passengers have reached their destination If our engines are too noisy for you, on passenger request, we can arrange to turn them off! To make your free fall to earth pleasant and memorable, we serve complimentary KONYAGI and Our favorite local brew MNAZI, you can also get GONGO if you promise not to drink more than half a bottle. For our not-so-religious passengers, we are the only airline who can help you find out if there really is a God!
We regret to inform you, that today's in-flight movie will not be shown as we could not record it from the ITV due to UEFA Champions League live broadcasting. However, we have bought 10 copies of SANI Magazines and 12 copies of NIPASHE to supplement the movie. There is no smoking allowed in this airplane. Any smoke U see in the
cabin is only the early warning system on the engines telling us to slow down or our stewards might be making TEA for the cockpit crews including myself In order to catch important landmarks, we try to fly as close as possible for the best view. If however, we go a little too close, do let us know. Our enthusiastic co-pilot sometimes flies right through the landmark! Kindly be seated, keep your seat in an upright position for take-off and fasten your seat belt. For those of you who can't find a seat-belt, kindly fasten your own belt to the arm of your seat. And, for those of you who can't find a seat, do not hesitate to get in touch with a stewardess who will explain how to fasten yourself on the overhead lockers." "Thanking you all for choosing Air-Tanzania to fly for the first and probably the last time."
that savagery...
 
Back
Top Bottom