Serikali kuwashirikisha Watanzania wa ughaibuni kujenga uchumi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Serikali kuwashirikisha Watanzania wa ughaibuni kujenga uchumi

2008-04-20 11:44:29
Na Mwandishi Maalum, London

Rais Jakaya Kikwete amesema serikali inatambua hazina kubwa ya uwezo wa kitaalam, nguvu kazi na hata uwezo wa kuwekeza walionao Watanzania wanaoishi ughaibuni.

Kwa kutambua hazina hiyo, alisema serikali imeunda kamati maalum ya kuangalia namna ya kuwashirikisha Watanzania hao katika kujenga na kuendeleza uchumi wa nchi katika mfumo rasmi pamoja na masuala mengine yanayohusu ustawi wa Watanzania hao hapa nchini.

Rais alisema hayo katika hotua yake iliyosomwa kwa niaba yake na Makamu wa Rais Dk. Ali Mohammed Shein, katika ufunguzi wa kongamano la kwanza la Watanzania wanaoishi Uingereza, lililofanyika Ijumaa mjini London, Uingereza.

Rais Kikwete aliwaeleza Watanzania hao kuwa idadi ya Watanzania wanaohamia nje kutafuta maslahi bora na kwa sababu nyingine, inazidi kuongezeka jambo ambalo linatoa changamoto kwa serikali kufikiria na kupanga namna ya kuwashirikisha watu hao katika maendeleo ya taifa.

``Hali hii inatoa changamoto kubwa kwetu sisi tulioko serikalini katika kubuni na kuandaa mikakati na sera za kuwatambua Watanzania hao na hatimae kuweka utaratibu wa kuwahamasisha ili waweze kuchangia kwa ukamilifu katika maendeleo ya taifa.

``Umoja wa Afrika ambao mimi ni Mwenyekiti wake, ulitangaza tangu mwaka 2003 kutambua Waafrika waishio nje ya bara letu kuwa jimbo rasmi.

Uamuzi huo ulitokana na mchango mkubwa wa Waafrika waishio ughaibuni katika uchumi wa nchi zao,`` alisema.

Kutokana na umuhimu huo, Rais Kikwete alisema kuanzia sasa serikali imeamua kuwahesabu Watanzania hao kama mkoa rasmi wa nchi na mipango ya maendeleo inapoandaliwa, itazingatia hilo pia.

Rais Kikwete alifafanua kuwa, Kamati Maalum iliyoundwa na serikali kwa sasa inaangalia masuala matatu ambayo kwanza ni kuwashirikisha Watanzania hao katika kujenga na kuendeleza uchumi wa nchi katika mfumo rasmi.

Alisema suala la pili ni la kufanya mchakato wa marekebisho ya sheria zinazohusiana na marejesho ya fedha na mikopo kwa watu waishio nje ili utaratibu wa Watanzania hao kufungua akaunti maalum zitakazorahisisha utumaji wa fedha nyumbani kwa kutumia mfumo rasmi.

Kwa mujibu wa Rais, jambo la tatu ni kupitia upya sheria ya uraia ili kuona uwezekano wa kuruhusu uraia wa nchi mbili na pia aliahidi kamati hiyo itapitia pia mapendekezo yatakayotolewa na mkutano huo.

Akitumia takwimu za Benki ya Dunia kuhusu mchango wa watu wanaoishi nje kwa nchi zao Rais Kikwete alisema watanzania wako nyuma wakilinganishwa na majirani zao wa Kenya.

``Hata majirani zetu wa Kenya, hupata mapato ya kutosha yatokanayo na raia wao waishio nje.

Kwa mujibu wa Benki ya Dunia, Kenya mwaka 2006 iliingiza dola za Kimarekani bilioni moja, ikilinganishwa na dola milioni moja tu zilizorejeshwa Tanzania na Watanzania waishio ughaibuni,`` alisema.

Kuhusu kilio cha Watanzania hao cha kukosekana vivutio vya kuwahamasisha kuwekeza nyumbani, Rais aliwapa changamoto ya kuorodhesha mapendekezo ya vivutio ambavyo wao wanadhani vinafaa, na kuahidi serikali kuyafanyia kazi.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Bi. Mwanaidi Sinare Maajar, akizungumza katika kongamano hilo, alisema miongoni mwa madhumuni ya Jumuiya ya Watanzania wanaoishi Uingereza ni pamoja na kupata takwimu sahihi za Watanzania hao wa Uingereza na kufahamu shughuli wanazozifanya.

Kusudio jingine ni kuwahamasisha kurejesha fedha nchini Tanzania, kuhamasisha kampuni za nje zinazofanya shughuli zao Tanzania, kuajiri Watanzania walio nje wenye sifa zinazotakiwa na kuwaweka Watanzania walio nje karibu na serikali yao.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio Uingereza, Bw. Abubakar Faraji, alisema mkutano huo ni wa aina yake na kwamba umefungua njia katika kuiunga mkono kauli ya Rais Kikwete ya kuwataka Watanzania kuwekeza nyumbani.

Bw. Faraji alizishukuru kampuni zilizochangia kufanikisha mkutano huo za ZANTEL, TIGO, VODACOM, Benki za Posta, CRDB, Commercial Bank of Afrika, Western Union, Kampuni ya KPMG, Cargo Stars na Shirika la ndege Kenya Airways.

SOURCE: Nipashe
 
Sijui ripoti hiyo ya WB anayozungumzia Kikwete ni ipi, maana hapa chini ripoti ya WB inaonyesha Watanzania walio nje mwaka 2006 walituma kiasi cha $14 million na siyo $1 million kama alivyosema JK. Pia kwa maoni yangu si sawa kulinganisha kiasi kikubwa kinachopelekwa na Wakenya na Waganda ambao wameanza kuhamia nchi za nje miaka mingi iliyopita ukilinganisha na Watanzania ambao wamenza kufanya hivyo kati ya miaka 15 mpaka 20 iliyopita, pia asilimia ya Watanzania walio nje ukilinganisha na population yetu ni ndogo sana kuliko ya Wakenya au Waganda.

Kenya tops in migrant cash remittances

By BENON HERBERT OLUKA
Special Correspondent
THE EAST AFRICAN

A World Bank report has named Kenya and Uganda among sub-Sahara Africa's top 10 recipients of migrant remittances for the second year running.

The report, titled Migration and Remittances Factbook 2008, says Kenya was the second highest recipient of remittances in 2007 with $1.3 billion, up from the $1.1 billion that the country received in 2006.

Nigeria was the highest recipient, with $3.3 billion. Other recipients in the top 10 were Sudan with $1.2 billion, Senegal and Uganda with $0.9 billion each, South Africa $0.7 billion, Lesotho $0.4 billion, Mauritius $0.2 billion, Togo $0.2 billion and Mali $0.2 billion.

The report provides snapshots of statistics on migration, recorded remittances flows, and skilled emigration for 194 countries and 13 regional income groups.

Inward remittances for all developing countries stood at $10.3 billion in 2006 and $10.8 billion in 2007, accounting for less than 2 per cent of their average gross domestic product.

In the case of Kenya, says the report, the remittances in 2006, all of which came from workers, constituted 5.3 per cent of the country's GDP.

According to the report, by 2005, Kenya's immigrant population was 1 per cent of the country's total population. Uganda, on the other hand, emerged the fifth highest recipient of migrant remittances in 2007 with $0.9 billion, up by $0.1 billion from 2006 when it also featured among sub-Saharan Africa's top 10 remittance recipients.

For Uganda, where the immigrant population is 0.5 per cent of the total population, inward remittances constituted 8.7 per cent of the GDP in 2006. The report says that remittances to both Uganda and Kenya have risen steadily over the past seven years. In 2000, inward remittances to Uganda stood at $238 million, while those to Kenya were at $538 million.

For Tanzania, the inward remittances, currently accounting for 0.1 per cent of the GDP, have stagnated at $14 million for both 2006 and 2007 – having fallen by $4 million from $18 million in 2005.

Rwanda's inward remittances, which accounted for 0.8 per cent of the country's GDP in 2006, have also stagnated at $21 million since 2005 - having risen from $10 million of 2004. Rwanda's migrant population is 2.2 per cent of the country's total population.

A statement from the World Bank said that for 2007, recorded remittances worldwide were estimated at $318 billion, of which $240 billion went to developing countries.

The report lists the world's top five recipients of migrant remittances in 2007 as India ($27 billion), which also had the world's largest migration population of 5.7 million; China ($25.7 billion); Mexico ($425 billion); Philippines ($17 billion) and France (12.5 billion).

In many countries, remittances provide a lifeline for the poor," says Dilip Ratha, a senior World Bank economist, and co-author of the factbook with Zhimei Xhu.

"They are often an essential source of foreign exchange and a stabilising force for the economy in turbulent times."

For many sub-Saharan countries, however, the remittance figures are also an indicator of the high levels of brain drain that have deprived these countries of some of their finest brains.

In Uganda, for instance, statistics showed a ratio of one doctor to 13,000 people, while that of nurses is 1:1,818 people, even as hundreds of Ugandan medical practitioners are working outside the country.

The World Bank report also notes that, in 2000, the emigration rate for people with tertiary education stood at 26.3 per cent in Kenya, 21.6 per cent in Uganda, 19.9 per cent in Burundi, 19 per cent in Rwanda and 15.8 per cent in Tanzania.

The report further notes that while international immigration is dominated by the voluntary movement of people, there were 13.5 million refugees and asylum seekers, constituting about 7 per cent of global immigrants, in 2005.

"The share of refugees was 14.3 per cent in low-income countries - over five times as large as in high-income European countries," says the report.
 
Back
Top Bottom