MIUNDOMBINU
JF-Expert Member
- Apr 14, 2010
- 465
- 96
Serikali inatarajia kuunda chombo cha kudhibiti riba za mikopo katika taasisi za fedha nchini ili kuwaondolea mzigo wananchi wa kutozwa riba kubwa.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Fedha, Yusuf Omari Mzee wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mbozi Mashariki (CCM), Godfrey Zambi.
Alisema kuna upungufu mkubwa katika kudhibiti riba hizo na kuahidi kuwa katika kipindi kifupi kijacho Serikali itaunda chombo hicho.
Katika swali lake la nyongeza, Zambi alihoji ni kwa nini taasisi za Serikali zitumike kama wakala wa watumishi katika suala la mikopo kwenye taasisi hizo ambazo zinatoza riba kubwa.
Vilevile alihoji nchi gani ambayo inaacha taasisi za kifedha kukopesha kama wanavyotaka kama ilivyo nchini.
Awali katika swali la msingi la mbunge huyo, alitaka kufahamu je, Serikali haioni kwamba taasisi hizo zinawanyonya wananchi kuliko kuwasaidia.
Pia alitaka kujua ni chombo gani hasa cha Serikali kinachodhibiti mwenendo wa taasisi hizo hasa katika riba? Akijibu swali hilo, Mzee, alisema kuwepo kwa taasisi nyingi zinazohusiana na utoaji wa mikopo, kunawapa uwanja mpana wananchi wa kuchagua taasisi zinazokidhi mahitaji yao na huduma bora.
Kuhusu suala la riba kubwa, alisema jambo la msingi ni kuhakikisha idadi ya taasisi zinazokopesha zinaongezeka ili kutoa huduma kwa ushindani.
Alisema hatua nyingine ni kuwa na chombo kitachosimamia mwenendo mzima wa shughuli za taasisi hizo.
" Hii ndio njia muafaka ya kuleta suluhisho katika taasisi hizi pamoja na tatizo la riba, alisema.
CHANZO: NIPASHE
Hayo yalisemwa jana na Naibu Waziri wa Fedha, Yusuf Omari Mzee wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mbozi Mashariki (CCM), Godfrey Zambi.
Alisema kuna upungufu mkubwa katika kudhibiti riba hizo na kuahidi kuwa katika kipindi kifupi kijacho Serikali itaunda chombo hicho.
Katika swali lake la nyongeza, Zambi alihoji ni kwa nini taasisi za Serikali zitumike kama wakala wa watumishi katika suala la mikopo kwenye taasisi hizo ambazo zinatoza riba kubwa.
Vilevile alihoji nchi gani ambayo inaacha taasisi za kifedha kukopesha kama wanavyotaka kama ilivyo nchini.
Awali katika swali la msingi la mbunge huyo, alitaka kufahamu je, Serikali haioni kwamba taasisi hizo zinawanyonya wananchi kuliko kuwasaidia.
Pia alitaka kujua ni chombo gani hasa cha Serikali kinachodhibiti mwenendo wa taasisi hizo hasa katika riba? Akijibu swali hilo, Mzee, alisema kuwepo kwa taasisi nyingi zinazohusiana na utoaji wa mikopo, kunawapa uwanja mpana wananchi wa kuchagua taasisi zinazokidhi mahitaji yao na huduma bora.
Kuhusu suala la riba kubwa, alisema jambo la msingi ni kuhakikisha idadi ya taasisi zinazokopesha zinaongezeka ili kutoa huduma kwa ushindani.
Alisema hatua nyingine ni kuwa na chombo kitachosimamia mwenendo mzima wa shughuli za taasisi hizo.
" Hii ndio njia muafaka ya kuleta suluhisho katika taasisi hizi pamoja na tatizo la riba, alisema.
CHANZO: NIPASHE