|
| |
|
|
| |
|
wanaandaa makazi yao bora maana wanajua 2015 wengi saana wataishia jela baada ya CDM kuchukua nchi.
Umenikumbusha joke kama hii:wanaandaa makazi yao bora maana wanajua 2015 wengi saana wataishia jela baada ya CDM kuchukua nchi.
Tanzania yangu huwa haiishiwi vituko. Baada ya ukarabati na ujenzi wa nyumba kubwa na ya kisasa zaidi ya kuhifadhia maiti katika nchi za SADDC, sasa tunawapiga bao jirani zetu kwa kuhakikisha kila wilaya inajitosheleza na kujitegemea kwa kuwa na gereza lake yenyewe....
Magereza nchini yaelemewa
na Ghisa Abby, Morogoro
MAGEREZA nchini zinakabiliwa na msongamano wa wahalifu kutokana na kuwapo 38,000 wakati magereza hayo yana uwezo wa kuchukua waharifu 29,522.
Hayo yalibainishwa jana mjini hapa na Kamishana Jenerali wa Magereza, Augustino Nanyaro, baada ya kuwavisha nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Nne maofisa na askari magereza 37 katika sherehe iliyofanyika katika viwanja vya gereza la Mtego wa Simba Kingorwila mkoani Morogoro.
Alisema kukosekana kwa magereza katika baadhi ya wilaya kunachangia kwa kiasi kikubwa msongamano huo ambapo wahalifu wake wanalazimika kuwekwa katika magereza za wilaya za jirani.
Alisema ili kukabiliana na msongamano huo, wanatarajia kujenga magereza 39 katika wilaya ambazo hazina magereza.
Aidha, alisema wameweka mkakati na vyombo vya dola kupunguza msongamano huo kwa mahabusu ambao kesi zao zinaweza kufanyiwa upelelezi haraka na kutolewa hukumu badala ya kuchukua muda mrefu.
Alisema mara nyingi msongamano huo husababishwa na mahabusu ambao kesi zao ziko katika hatua za upelelezi.
Source:Tanzania Daima 6.6.2012