Serikali kujenga kiwanda kipya cha matairi, kuitosa General Tyre ya Arusha

Kwani hutuwezi kubadili tekinolojia iliyotumiwa na General tyre kwa kuiboresha na kufanya iwe ya kisasa kama anavyotaka? Kuna haja gani ya kuanza kujenga kiwanda kipya Wakati tayari tunacho kingine kinachohitaji uboreshaji tu?kila tunapoukaribia ukweli serikali inajitokeza na kupindisha! Kwa nini? Kwa faida ya nani?
Haswaa
 
Kiukwel cc watanzania cjuw tuache uchama kwenye mambo ya kimaendeleo kikijengwa hçho kipya gharama yake ninafuu cn kulikokukiboresha kwn ukisema ukiboreshe ni lazima kifumuliwe upya kila k2 coast yake ni heli kujenga kipya
 
Structure ya kuendana na mashine mpya, rewiring, re plumbing na ku repair majengo kuanzia roof mpaka milango, security systems inaweza kuwa ni busara kuanza kujenga majengo mapya.

Lakini itakuwa ni busara zaidi kama watajenga hapo hapo yalipo ya zamani, kuyabomoa ya zamani na kujenga mapya.
Ni sound za siasa hakuna kipya wala GT
 
Tungeachana na hii mipango ya kujenga matairi, coz hatutakuwa competitive na itatuchukua muda sana pia inawezekana tusipate kabisa faida. Initial costs zitakuwa kubwa sana halafu sidhani kama tutaweza ku match with competitors wenye technology kubwa na wapo kwenye economies of scale.. Unless tunataka kuchoma pesa za walipa kodi. (my opinion though)
Wewe unashauri nini...tuanze na kipi na tuache kipi?
 
Rais anaendeleza ubaguzi wa kisiasa

Uwe na akiba ya maneno Ndugu,Ubaguzi gani uko hapo? Imetamkwa kinajengwa wapi? Arusha unaifahamu vizuri au unaongea tu..! Mhe Lema aliishauri serikali kwamba mahali kilipo Kiwanda si salama kwa sasa kulingana na mazingira ya sasa ya Jiji kukua na kupanuka, kwamba Eneo hilo lenye makazi ya watu kwa sasa likipimwa viwanja na kuuzwa Serikali itajipatia Fedha, na kama una uelewa wa Mambo viwanda hujengwa nje ya mji sio katikati yaliko makazi ya watu, Usitangulize chuki kwa kila jambo inalofanya serikali.
 
Tungeachana na hii mipango ya kujenga matairi, coz hatutakuwa competitive na itatuchukua muda sana pia inawezekana tusipate kabisa faida. Initial costs zitakuwa kubwa sana halafu sidhani kama tutaweza ku match with competitors wenye technology kubwa na wapo kwenye economies of scale.. Unless tunataka kuchoma pesa za walipa kodi. (my opinion though)
Nahisi una hoja nzuri ila je unashauri hiyo hela ielekezwe wapi kwingine?
 
Watu wanagusa hapa, wanaacha,
wanagusa paleeee wanakimbia,
wanashika huku wanaondoka.
Jamani miaka inakimbia hiii mjue....maana Biotech Product pale Kibaha imedoda,General Tyre inaoza,leo wanakuja na lingine......
 
Kwani hutuwezi kubadili tekinolojia iliyotumiwa na General tyre kwa kuiboresha na kufanya iwe ya kisasa kama anavyotaka? Kuna haja gani ya kuanza kujenga kiwanda kipya Wakati tayari tunacho kingine kinachohitaji uboreshaji tu?kila tunapoukaribia ukweli serikali inajitokeza na kupindisha! Kwa nini? Kwa faida ya nani?
Hapo kuna 10% ya wakubwa!
 
General Tyre waliitangaza kwa mbwembwe sana Okt 2015,
Umesahau waliambiwa watapewa ajira na mikopo....leo wanaambiwa wavivu hawataki kufanya kazi wanashinda kwenye pool! Walishawahi kupewa hizo kazi wakakataa? Wanaambiwa wakalime! Hivi unaanzaje kulima tu! Kilimo cha aina gani cha kisasa cha umwagiliaji au cha kusubiri neema mvua!! Kipindi kuandaa mashamba hadi kuvuna unaishije huko shambani?? Hakuna mpango wowote kuwasaidia hao vijana kupata mashamba kuandaa kulima mbegu bore mbolea hadi utaalam! Wanasema tu hawataki kazi! Tutajuta!!
 
Uwe na akiba ya maneno Ndugu,Ubaguzi gani uko hapo? Imetamkwa kinajengwa wapi? Arusha unaifahamu vizuri au unaongea tu..! Mhe Lema aliishauri serikali kwamba mahali kilipo Kiwanda si salama kwa sasa kulingana na mazingira ya sasa ya Jiji kukua na kupanuka, kwamba Eneo hilo lenye makazi ya watu kwa sasa likipimwa viwanja na kuuzwa Serikali itajipatia Fedha, na kama una uelewa wa Mambo viwanda hujengwa nje ya mji sio katikati yaliko makazi ya watu, Usitangulize chuki kwa kila jambo inalofanya serikali.
Sawa ila Arusha ni kubwa sana, ndani ya Arusha si kuna nje ya mji? Mfano kule kilipoamia kiwanda cha A to Z
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom