VIKWAZO
JF-Expert Member
- Apr 9, 2011
- 1,899
- 580
SERIKALI imesema Tanzania ina kilometa 6,318 za barabara za lami kwa nchi nzima.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe alisema kilometa hizo za barabara za lami ni miongoni mwa kilometa 86,472 za barabara zote zilizo kwenye mtandao wa barabara nchini.
Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM) aliyetaka kufahamu sababu za Serikali kushindwa kuweka lami barabara inayokwenda katika Wilaya ya Chamwino ambako ni nyumbani kwa Waziri Mkuu mstaafu, Samwel Malecela kama njia ya kumuenzi.
Dk. Mwakyembe amewaeleza wabunge mjini Dodoma kuwa, Serikali imejipanga ifikapo mwaka 2017/2018 iwe imekamilisha kuunganisha makao makuu ya mikoa kwa barabara za lami na baada ya hapo itaangalia barabara nyingine.
Akijibu swali la msingi la Lusinde, aliyetaka kufahamu lini Serikali itatengeneza barabara ya lami kutoka Dodoma mjini hadi Hospitali Teule ya Mvumi yenye kilometa 40, alisema kwa sasa Serikali haina mpango wa kuweka lami barabara hiyo.
Alisema, Wakala wa Barabara (Tanroads) ataendelea kuifanyia matengenezo barabara ya Dodoma hadi Mvumi kwa kiwango cha changarawe ili iendelee kupitika kwa urahisi majira yote ya mwaka.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk. Harrison Mwakyembe alisema kilometa hizo za barabara za lami ni miongoni mwa kilometa 86,472 za barabara zote zilizo kwenye mtandao wa barabara nchini.
Alikuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde (CCM) aliyetaka kufahamu sababu za Serikali kushindwa kuweka lami barabara inayokwenda katika Wilaya ya Chamwino ambako ni nyumbani kwa Waziri Mkuu mstaafu, Samwel Malecela kama njia ya kumuenzi.
Dk. Mwakyembe amewaeleza wabunge mjini Dodoma kuwa, Serikali imejipanga ifikapo mwaka 2017/2018 iwe imekamilisha kuunganisha makao makuu ya mikoa kwa barabara za lami na baada ya hapo itaangalia barabara nyingine.
Akijibu swali la msingi la Lusinde, aliyetaka kufahamu lini Serikali itatengeneza barabara ya lami kutoka Dodoma mjini hadi Hospitali Teule ya Mvumi yenye kilometa 40, alisema kwa sasa Serikali haina mpango wa kuweka lami barabara hiyo.
Alisema, Wakala wa Barabara (Tanroads) ataendelea kuifanyia matengenezo barabara ya Dodoma hadi Mvumi kwa kiwango cha changarawe ili iendelee kupitika kwa urahisi majira yote ya mwaka.