ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Kuna taarifa kuwa kufuatia fedha nyingi zilizotengwa katika bajeti ya mwaka 2011/12 kutumika kwa shughuli za maazimisho ya miaka 50 ya Uhuru ambazo hazikuwa na tija, Serikali kupitia Hazina imekata zaidi ya asilimia 50 ya Bajeti za Idara na Wizara zake pasipo kueleza fedha hizo ambzo zilitengwa kwa kazi za maendeleo zinahitajika kurejeshwa Hazina kwa kazi ipi. Hatua hii imeelezwa kuwa itaathiri kwa kiasi kikubwa sana ugharimiaji wa shughuli za maendeleo ..hivi karibuni watanzania wategemee hali mbaya.
Kuna taarifa kuwa katika bajeti iliyopitishwa na Bunge kwa mwaka 2011/12 Serikali ilitioa mgao awamu moja tu katika Wizar zake ambao ulifanyika Mwezi Agosti 2011 na sasa imeamua kurejesha Hazina sehemu ya fedha hizo zilizotengwa kwenye Bajeti ya Serikali.
Ikumbukwe kuwa hata ile Bajeti ya maazimisho ya Uhuru haikuwahi kupitishwa Bungeni. Hivyo yawezekana kabisa ilitoka katika fedha zilizotengwa kwa ajili ya Maendeleo.
Kuna taarifa kuwa katika bajeti iliyopitishwa na Bunge kwa mwaka 2011/12 Serikali ilitioa mgao awamu moja tu katika Wizar zake ambao ulifanyika Mwezi Agosti 2011 na sasa imeamua kurejesha Hazina sehemu ya fedha hizo zilizotengwa kwenye Bajeti ya Serikali.
Ikumbukwe kuwa hata ile Bajeti ya maazimisho ya Uhuru haikuwahi kupitishwa Bungeni. Hivyo yawezekana kabisa ilitoka katika fedha zilizotengwa kwa ajili ya Maendeleo.