Elba
JF-Expert Member
- Sep 11, 2010
- 382
- 104
SERIKALI imesema mchakato wa mabadiliko ya Katiba utaanza hivi karibuni na itahakikisha kuwa Katiba mpya inapatikana mwaka 2014.
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Oliver Mhaiki, alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala inayoongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana, iliyotaka kufahamu jinsi serikali ilivyojipanga kwa mchakato huo.
Alisema maandalizi ya kuanza kwa mchakato huo yamekamilika na tayari muswada wake umeshapita katika vikao husika na kwamba kinachosubiriwa kwa sasa ni kufikishwa bungeni.
Mchakato wa katiba itakayotokana na ridhaa ya wananchi utakamilika baada ya miaka miwili kutoka sasa. Wizara ilishaandaa waraka kuhusu suala hilo na ulishafikishwa katika kikao cha kamati ya ufundi ya serikali inayoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, kwa hatua zaidi.
Kamati ya Luhanjo ilishaujadili waraka na iliupeleka katika kikao cha baraza la mawaziri ambalo lilishaketi na kuupitisha waraka huo hatua inayofuatia sasa ni waraka huo kupitiwa kama muswada kwa ajili ya kuwasilishwa kati ya mwezi Juni au lile Bunge la Novemba, alisema Mhaiki.
Ufafanuzi huo ulitokana na maswali yaliyoulizwa na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Angellah Kairuki na Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi), ambao kimsingi walitaka kujua Katiba mpya itapatikana lini na kutaka kujua nini kinaendelea tangu Rais Jakaya Kikwete atoe tamko lake kuhusu suala hilo.
Source: Tanzania Daima
Wanajamvi, siamini kama sisiem inaanza kuchimba kaburi lake!
Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria na Katiba, Oliver Mhaiki, alipokuwa akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Sheria, Katiba na Utawala inayoongozwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Pindi Chana, iliyotaka kufahamu jinsi serikali ilivyojipanga kwa mchakato huo.
Alisema maandalizi ya kuanza kwa mchakato huo yamekamilika na tayari muswada wake umeshapita katika vikao husika na kwamba kinachosubiriwa kwa sasa ni kufikishwa bungeni.
Mchakato wa katiba itakayotokana na ridhaa ya wananchi utakamilika baada ya miaka miwili kutoka sasa. Wizara ilishaandaa waraka kuhusu suala hilo na ulishafikishwa katika kikao cha kamati ya ufundi ya serikali inayoongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, kwa hatua zaidi.
Kamati ya Luhanjo ilishaujadili waraka na iliupeleka katika kikao cha baraza la mawaziri ambalo lilishaketi na kuupitisha waraka huo hatua inayofuatia sasa ni waraka huo kupitiwa kama muswada kwa ajili ya kuwasilishwa kati ya mwezi Juni au lile Bunge la Novemba, alisema Mhaiki.
Ufafanuzi huo ulitokana na maswali yaliyoulizwa na Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Angellah Kairuki na Mbunge wa Jimbo la Muhambwe, Felix Mkosamali (NCCR-Mageuzi), ambao kimsingi walitaka kujua Katiba mpya itapatikana lini na kutaka kujua nini kinaendelea tangu Rais Jakaya Kikwete atoe tamko lake kuhusu suala hilo.
Source: Tanzania Daima
Wanajamvi, siamini kama sisiem inaanza kuchimba kaburi lake!